Monday, May 20, 2013

WATU 31 WAUAWA KATIKA SHAMBULIO LA BOMU IRAQ.


Kiasi  watu  20 wameuwawa  katika  wimbi  la  mashambulio  ya mabomu  yaliyowekwa  katika  magari  katika  wilaya  inayoishi waumini  wengi  wa  madhehebu  ya  Shia  katika  mji  mkuu  wa  Iraq , Baghdad, leo.  Watu   wengine  11  wameuwawa  katika mashambulio  katika  mji  wa  kusini  wa  Basra.  Watu  kadha wameuwawa  katika  mashambulio  katika  muda  wa  wiki  moja iliyopita   wakati  hali  ya  wasi  wasi  inaongezeka   kati  ya Waislamu  wa  madhehebu  ya  Sunni  ambao  ni  wachache  nchini humo  na  Washia  waliowengi, ambao  hivi  sasa  wanashikilia madaraka  ya  serikali  ya nchi  hiyo. Idadi  ya  mashambulio imepanda  mno  tangu majeshi  ya  Marekani  kuondolewa  Desemba mwaka  2011.
Polisi  na  wafanyakazi  wa  Hospitali  wamesema  kuwa mashambulio  manane  ya  mabomu  yaliyotegwa  katika  magari katika  wilaya  ya  Washia  mjini  Baghdad , yamesababisha  vifo vya  watu  wapatao  20  leo.

Source: DW

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...