Wednesday, November 19, 2014

Bill Gates kusaidia kupambana na Ebola.

Mfuko wa Bill na Melinda Gates umeahidi kutoa kiasi cha dola milioni 5.7 kwa ajili ya mradi kusaidia matibabu dhidi ya maradhi ya Ebola nchini Guinea na nchi nyingine zilizoathiriwa na ugonjwa huo.
Mfuko huo pia umesema msaada huo utasaidia kutathimini dawa za majaribio.
Zaidi ya Watu 5,000 wamepoteza maisha kutokana na Ebola, karibu wote kutoka Afrika Magharibi.
Mpaka sasa hakuna dawa iliyoidhinishwa wala chanjo ya kupambana na Virusi vya Ebola,matibabu ya hospitalini hutolewa kwa kuwapa wagonjwa maji ili kufunga kuharisha na dawa za kupambana na vijidudu.
Hata hivyo kuna chanjo kadhaa za majaribio na dawa za kutibu maradhi ya Ebola, lakini hazijajaribiwa kwa ajili ya kuona usalama wake na namna zinavyofanya kazi.
Shirika la Madaktari wasio na mipaka, MSF linatarajia kuanzisha majaribio ya tiba Afrika Magharibi mwezi Desemba.
Mfuko huo unamilikiwa na mwanzilishi wa kampuni ya Microsoft Bill Gates na mkewe Melinda umesema kuwa utafanya kazi na washirika kadhaa kwa ajili ya kutengeneza tiba.
Tiba hiyo itatumia damu iliyotolewa na watu waliopona maradhi ya Ebola.
Akiongea mwanzoni mwa mwezi huu, Bill Gates alisema utafiti zaidi kuhusu Ebola unahitajika .

Chanzo: BBC

Monday, November 3, 2014

JOB VACANCIES - BOT.

JOB VACANCIES ADVERTISEMENT - TIRDO

JOB VACANCIES FOR DRIVERS - DAWASCO

Jaji Mstaafu Warioba adhalilishwa mdahalo wa Katiba

Waziri Mkuu mstaafu Joseph Warioba akisaidiwa kutolewa katika vurugu
Katika mazingira ya kutatanisha, siku ya Jumapili vurugu zimekatisha mdahalo uliokuwa ukiendelea kujadili mchakato wa katiba mpya ya Tanzania huku baadhi ya watu wakipigwa na kujeruhiwa.
Mdahalo huo uliokuwa ukitangazwa moja kwa moja kupitia redio na televisheni ulivurugika kutokana na kundi la vijana wapatao 20 kuanza kumzomea aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, alipokuwa akiwasilisha mada yake.

EXPECTED GRADUANTS 2013/2014 - SAUT.

Click here (Bofya hapa)

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...