Friday, April 12, 2013

UKWELI KUHUSU LADY JAYDEE KUANZISHA KITUO CHA REDIO


Kutokana na uvumi na taarifa mbali mbali kuhusu mpango wa Lady Jaydee kuanzisha kituo cha redio kiitwacho KWANZA FM leo mhusika (Jidee) kaweka mambo hazarani na kusema kuwa kwanza taarifa hizo zilikuwa ni uzushi kutokana na tarehe hiyo zilipotoka kuwa ni siku ya wajinga.

Ameweka bayana maneno hayo usiku wa leo wakati akifanya mahojiano (Interview) katika kituo cha televisheni cha Channel ten. Mahojiano hayo yalikuwa ni kati ya Jay dee na Dj Tass. Lakini lady Jaydee amesema kutokana na mwitikio aliouona kwa watu ameamua kuwa na mpango huo wa kuanzisha kituo hicho cha redio.

Kuhusu wimbo wake wa Joto hasira, amesema ameutunga na kuuimba kwa kumlenga mtu ambaye hakuwa tayari kumtaja.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...