Friday, April 12, 2013

RAIS KIKWETE AFUNGA SEMINA KWA MAWAZIRI NA MAKATIBU WAKUU DODOMA

Rais wa Tanzania Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akifunga semina.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete afunga semina kwa
Mawaziri na Makatibu wakuu  katika ukumbi wa St Gaspar mjini Dodoma ikiwa na mpango wa kupanga mikakati ya utekelezaji wa mfumo mpya wa kusimamia utekelezaji, ufuatiliaji na tathmini ya miradi ya maendeleo . Mfumo huo unaanza kutekelezwa  kwa kutumia uzoefu wa Performance Management and Delivery Unit (PEMANDU) ya Malaysia. 


Mfumo huu utajumuisha uanzishwaji wa taasisi ya President’s Delivery Bureau (PDB) ambayo itafanya kazi kwa karibu na Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango. Katika mfumo huu, uchambuzi wa kina wa kimaabara (labs) utafanyika ili kuandaa programu za utekelezaji wa miradi ya maendeleo. 

Awamu ya kwanza ya labs ilizinduliwa rasmi na Rais Kikwete  tarehe 22 Februari, 2013 na kukamilika Aprili, 2013. Maeneo ya awamu ya kwanza ya labs yanahusisha elimu, kilimo, nishati, mapato, maji na miundombinu ya uchukuzi.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...