Thursday, April 11, 2013

KUKITHILI KWA UCHAFU SOKO LA JIJI LA ARUSHA

Soko Kuu la jijini Arusha, limekithiri kwa takataka zinazotoa harufu mbaya  ambayo inalalamikiwa na baadhi ya wafanyabiashara kuwa inahatarisha usalama wa afya zao.

Wafanyabiashara hao wakiwemo wanaomiliki maduka yanayolizunguka soko hilo, waliliambia gazeti hili kwamba takataka hizo zinatupwa nje ya soko.

Hata hivyo walalamikaji hao hawakutaka majina yao yatajwe lakini walisema takataka  hizo zimerundikwa kwa  muda mrefu  bila ya kuzolewa na mamlaka zinazohusika.
Wafanyabiashara hao walisema katika kipindi hiki ambacho mvua zimekuwa zikinyesha mfululizo mkoani humo,  wamekuwa wakizishuhudia taka hizo zikioza na hatimaye kutoa harufu mbaya.
Mkuu wa soko hilo, John Lugiza alikiri kuhusu kuwapo kwa taka hizo na kwamba ni  kero hata kwa uongozi wa soko hilo.

Alisema kutokuzolewa kwa takataka hizo kunasababishwa na  gari kushindwa kuingia ndani ya soko na kwamba dampo la Muriet nalo  limejaa maji.


Habari hii kwa hisani ya Mwananchi.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...