Monday, April 22, 2013

UPINZANI SYRIA WAIONYA HEZBOLLAH

Upinzani nchini Syria umelitaka kundi la wanamgambo nchini Lebanon la Hezbollah kuwaondoa wapiganaji wake kutoka Syria. Wanaharakati wamesema kuwa majeshi ya serikali yanayoungwa mkono na watu wenye silaha wenye mafungamano na kundi hilo la Hezbollah, jana Jumapili walipambana na waasi wakitaka kuvidhibiti vijiji kadhaa karibu na mpaka wa Lebanon na Syria. Muungano wa upinzani wa Syria, umeonya kuwa kujihusisha kwa Hezbollah katika vita vya Syria kunaweza kusababisha hatari kubwa katika eneo hilo. Wakati huo huo, kiongozi wa muungano huo, Mouaz al-Khatib, jana amewasilisha barua ya kujiuzulu. Taarifa hizo zimetolewa kwenye ukurasa wa kijamii wa muungano huo, katika mtandao wake wa Facebook. Ama kwa upande mwingine, wanaharakati wameorodhesha majina ya watu 80 waliouawa katika mashambulizi yaliyofanywa na majeshi ya serikali kwa siku tano zilizopita.

CHANZO:IDHAA YA KISWAHILI YA UJERUMANI

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...