Monday, April 22, 2013

HATRICK YA ROBIN VAN PERSIE YATOSHA KUWAPA UBINGWA MAN UNITED.

Robin van persie akifunga goli la 3 (Hatrick)
Ilikuwa ni dakika ya kwanza RVP alipoipatia timu ya Man United goli la kwanza dhidi ya timu ya Aston Villa katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza mchezo uliopigwa katika uwanja wa Old trafford.
Ni dakika ya 12 Van Persie tena akaipatia timu yake goli la pili.Goli la tatu lilifungwa na Van persie tena ikiwa ni dakika ya 32.Magoli yote yalipatikana katika kipindi cha kwanza.Kutokana na kufunga magoli hayo matatu,Van Persie alitoka uwanjani na mpira baada ya kupiga Hatrick.
RVP akishangilia goli.
Van Persie alionekana kuwa mwimba katika ngome ya Aston  Villa baada ya kuwasumbua vyakutosha mabeki wa timu hiyo.
Na huu ndo msimamo baada ya matokeo hayo hapo juu:-

Club Pld Pts
Man Utd 34 84
Man City 33 68
Arsenal 34 63
Chelsea 33 62
Tottenham 33 61
Everton 34 56
Liverpool 34 51
West Brom 33 45
Swansea 33 42
West Ham 34 42
Fulham 34 40
Southampton 34 39
Norwich 34 38
Sunderland 34 37
Stoke 34 37
Newcastle 34 37
Aston Villa 34 34
Wigan 33 31
QPR 34 24
Reading 34 24

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...