Sunday, April 21, 2013

MTUHUMIWA WA BOSTON HAWEZI KUHOJIWA KUTOKANA NA KUUMIA VIBAYA.

Meya wa Boston amesema wakuu wa Marekani pengine hawataweza kabisa kumhoji mshukiwa wa shambulio la bomu katika Boston marathon kwa sababu ya jinsi alivoumia.

Mshukiwa huyo, Dzhokar Tsarnaev, anatibiwa kwenye hospitali moja ya mjini Boston, ambayo ilieleza kuwa hali yake ni mbaya.

Alikamatwa Ijumaa wakati wa msako ambapo kaka ake aliuliwa na polisi.
Meya Tom Menino alipohojiwa na televisheni ya Marekani alisema anafikiri mashambulio hayo yalifanywa na ndugu hao wa kiume peke yao, na pengine hawakupanga kufanya mashambulio mengine.

CHANZO:BBC

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...