Sunday, April 21, 2013

NJIA YA YANGA KUTWAA UBINGWA WA LIGI KUU YAZIDI KUTAKATA,YAILAZA JKT RUVU 3-0

Fuatana nami ujue nini kilikuwa kinatokea hatu kwa hatua kama ifuatavyo:-
Mpira unamalizika Yanga 3 - 0 JKT

Dk 90+4 Mgosi anachezewa faulo na Yondani nje kidogo ya eneo la hatari la Yanga. Faulo inapigwa na mpira unaokolewa na kuwa kona. Yanga 3-0 JKT

Dk 90+1 Nizar anapiga shuti kali linalopanguliwa na kipa wa JKT, Dihile.

Dk 89 Mwamuzi wa akiba Idd Soud anaonyesha bango kwa mpira umeongezwa dakika 5

Mara yangu ya mwisho kumuona Said Mohamed kwenye uwanja huu ni mwaka jana alipoingia kama sub kuchukua nafasi ya Yaw Berko kwenye mchezo ambao yanga walifungwa mabao 5:0 na Simba

Dk 86 Yanga inafanya mabadiliko ametoka Barthez ameingia Said Mohamed.
Dk 86 Inaonekana Barthez hawezi kuendelea na Said Mohamed anapasha misuli moto kujiandaa kuingia.

Dk 84 Kipa wa Yanga, Barthez anaanguka mwenyewe na mpira unaendelea kusimama ili Barthez atibiwe.

Dk 83 Mpira unasimama kwa muda baada ya Msuva kuchezewa rafu na Zahor Pazi. Yanga 3-0 JKT.

Dk 80 Jerry Tegete anaingia badala ya Hamis Kiiza

Dk 78 JKT wanafanya mabadiliko ametoka Ally Mkanga ameingia Charles Thadei.

Dk 76 JKT wamefanya mabadiliko ametoka Hassan Kikutwa ameingia Sosthenes Manyasi.

Dk 76 JKT wamefanya mabadiliko ametoka Hassan Kikutwa ameingia Sosthenes Manyasi.

Dk 75 Chuji wa Yanga anamchezea faulo Hussein Bunu wa JKT.

Dk 73 Msuva anachezewa faulo na Nashon Naftal nje kidogo ya eneo la hatari la JKT. Faulo inapigwa JKT wanaokoa. Yanga 3-0 JKT

Leo Yanga wametoa burudani kwa mashabiki walioingia uwanjani kwa soka safi

Shuti kali la Chuji linadakwa na kipa wa JKT

Goaaaaaaaaaaaal Nizar Khalfan anaipatia Yanga goli la 3

Dk 62 Mgosi anachezewa faulo na Kelvin Yondani.

JKT wanafanya mabadiliko anatoka Amos Mgisa anaingia Abdallah Bunu

Gooooooooal Free kick iliyopigwa na luhende imeunganishwa na Hamis Kiiza kwa kichwa

Dk 57 yanga wanapata faulo baaada ya Msuva kufanyiwa madhambi

Dk 55 Ally Nkanga analimwa kadi ya njano baada ya kumfanyia madhambi Nizar

Dk 53 Kiiza wa Yanga anashindwa kuunga vizuri pasi ya Domayo kwa shuti lake kutoka nje ya eneo la hatari la JKT.

Dk 49 JKT wanapiga kona na Yanga wanaokoa.

Dk 49 JKT wanapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari. Faulo inapigwa lakini Cannavaro anautoa nje mpira na kuwa kona.

Dk 48 Mgosi anapiga shuti hafifu na Barthez anaudaka mpira.

Kipindi cha pili cha mchezo kimeanza, JKT Ruvu 0 - 1 Young Africans

Dk 45 HALF TIME! Yanga 1-0 JKT

Simon Msuva anaipatia yanga bao hapa

Dk 41 Stanley Nkomola anapiga kona lakini kipa Barthez anaokoa.

Dk 39 Mgosi anamchezea faulo Cannavaro.

Dk 36 JKT wanapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari la Yanga. Faulo inapigwa na mabeki wa Yanga wanaokoa.

Dk35 Hamis kiiza anakosa bao la wazi

Dk 31 Yanga inapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari la JKT. David Luhende anamtengea Haruna Niyonzima lakini shuti lake linawababatiza mabeki wa JKT na mpira unaokolewa.

Dk 30 yanga wanapata kona nyingine Dihile anaokoa

Dk 26 Kwa mara ya tatu ndani ya dakika nne zilizopita mabeki wa Yanga wanamwekea Mgosi mtego wa kuotea naye anashindwa kung'amua hali hiyo na mara nyingi anajikuta akiwa ameotea.

Dk 26 Kwa mara ya tatu ndani ya dakika nne zilizopita mabeki wa Yanga wanamwekea Mgosi mtego wa kuotea naye anashindwa kung'amua hali hiyo na mara nyingi anajikuta akiwa ameotea.

Dk 24 Mussa Mgosi wa JKT anaipangua ngome ya Yanga lakini shuti lake linadakwa na kipa Ally Mustapha 'Barthez'.

Almanusura Nadir aipatie yanga bao kutokana na faulo ya Luhende

Dk 22 yanga wanapata faulo nje kidogo ya eneo la hatari

Dk 19 Athuman Idd Chuji wa Yanga anapiga shuti kali langoni kwa JKT lakini mpira unatoka nje kidogo ya lango.

Dk 18 Zahor Pazi wa JKT anachezewa faulo nje kidogo ya eneo la hatari la Yanga. Faulo inapigwa lakini mpira unatoka nje.

Dk 16 Yanga wanapata kona baada ya Damas Makwaya kuutoa nje mpira. Kona inapigwa na Dihile anaudaka mpira.

Dk 15 Kipa Dihile wa JKT anaudaka mpira wa krosi uliokuwa ukiwaniwa na Kiiza.

Dk 13 JKT wameanza kumiliki mpira na kuisumbua ngome ya Yanga. Yanga 0-0 JKT

Dk 12 Yanga inapata kona lakini kipa wa JKT, Shaaban Dihile anaudaka mpira.

Dk 10 Hamis Kiiza wa Yanga anamiliki mpira vizuri akipokea pasi ya Frank Domayo lakini mwamuzi Oden Mbaga anasema Kiiza ameoteaM

Yanga wanacheza vizuri sana hasa kwenye eneo la kiungo.

Dk 8 Mbuyu Twite wa Yanga anapiga shuti kali langoni kwa JKT lakini mpira unatoka juu kidogo ya mlingoti.

DIHILE AMENYANYUKA ANAPIGA FAULO

Shambulio hilo limesababisha golikipa wa JKT Dihile kuumia yupo chini anatibiwa

Dk ya tatu kona ya Luhende imesababisha kizaazaa kwenye lango la jkt ruvu

Yanga wanapata kona na inapigwa na David Luhende

Musa mgosi anamlazimisha Cannavari kuutoa nje mnamo dk 2

Mpira umeanza hapa taifa Yanga SC 0-0 JKT

Muda wowote kuanzia sasa soka litaanza na yanga ndo wanaanzisha kipute

Makame Rashid alifariki mwanzoni mwa juma hili,alikuwa mdau mkubwa wa soka

Wachezaji wanasimama kuomboleza kifo Makame rashid

JKT Ruvu line up: Shabani Dihile, Hassan Kikutwa, Stanley Mkomola, Madenge Ramadhan, Damas Makwaya, Nashon Naftar, Amos Mgisa, Ally Mkanga, Mussa Mgosi, Zahor Pazi na Haruna Adolph.


Kikosi cha Yanga

1.Ally Mustafa 'Barthez'
2.Mbuyu Twite
3.David Luhende
4.Nadir Haroub 'Cannavaro'
5.Kelvin Yondani
6. Athunman Idd 'Chuji'
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo
9.Hamis Kiiza
10.Nizar Khalfani
11.Haruna Niyonzima


Subs:
1.Said Mohamed
2.Shadrack Nsajigwa
3.Oscar Joshua
4.Salum Telela
5.Nurdin Bakari
6.Said Bahanuzi
7.Jerson Tegete
 
CHANZO,SHAFII DAUDA

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...