Monday, July 1, 2013

MISRI HALI TETE,RAIS ATAKIWA KUJIUZULU HADI KUFIKiA KESHO.

Umoja wa vyama vya upinzani unaompinga Rais Mohammed Morsi wa Misri, umemtaka Rais huyo kujiuzulu hadi kufikia kesho au atarajie uasi zaidi,na hii ikiwa ni mwaka mmoja tangu aingie madarakani. Siku ya jana ilimalizika kwa kuwashuhudia watu wakimiminika mitaani kwenye mji mkuu, Cairo. Wapinzani wanalituhumu kundi la Udugu wa Kiislamu la Rais Morsi kwa kuyateka mapinduzi ya umma, kupitia ushindi kwenye uchaguzi, kujilimbikizia madaraka na kutaka kuweka Sharia ya Kiislamu. Waandamanaji wengine wanasema wamevunjwa moyo na mgogoro wa kiuchumi. Maafisa wa usalama wanasema ofisi tatu za chama cha Udugu wa Kiislamu zilichomwa moto na waandamanaji kwenye jimbo la Nile Delta. Zaidi ya wafuasi 20,000 wa Rais Morsi pia walikusanyika karibu na kasri ya Rais mjini Cairo kumuunga mkono kiongozi huyo.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...