Wednesday, July 17, 2013

KAULI YA ZITTO KABWE ASUBUHI YA LEO.

CHADEMA na NCCR-M tuna jumla ya madiwani 13 katika halmashauri ya Wilaya Uvinza. Ni mamlaka mpya inaanza tarehe 20 Julai, 2013. CCM ina madiwani 8 tu, hivyo a clear majority kwa upinzani. CHADEMA ina madiwani 7, NCCR-M 5 + Mbunge 1.
Leo sekretariat za vyama vyetu zinakaa kuamua chama gani kati ya CHADEMA na NCCR-M kitoe Mwenyekiti, makamu na wenyeviti wa Kamati. Nimewaambia madiwani wetu kwamba Ni lazima kuhakikisha Halmashauri hii inaongozwa na Upinzani. Tukiendekeza tamaa zetu za kisiasa CCM watapita katikati yetu. CCM wakichukua Halmashauri ya Uvinza yenye madiwani wengi wa upinzani itakuwa Ni usaliti mkubwa Kwa wananchi. Nimewasihi viongozi wa vyama vyote 2 kuwa na hekima na kuzingatia matakwa ya wananchi waliotoa ridhaa mwaka 2010 na hivyo CHADEMA na NCCR-M kuongoza Halmashauri ya Wilaya Uvinza. Ni jaribio la demokrasia, Hekima na Maamuzi.
Source: Zitto Kabwe Social media.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...