Tuesday, November 27, 2012

MAAJABU YA KIDUNIA YANAYOTEKETEZWA.

MAAJABU YA KIDUNIA YANAYOTEKETEZWA.

ULUGURU BUSH-SHRIKE – Ndege anayepatikana Milima ya Uluguru pekee Duniani
Ndege huyu ni ndege ajulikanaye kwa jina la kitaalamu kama Malaconotus alius mwenye ukubwa wa sm 22- 24 ambaye hupatikana katika safu za milima ya Uluguru Tanzania. Mwaka 1999-2000, sensa ilikadiria kuwepo jumla ya jozi 1,200 sawa na ndege 2,400 (Burgess et al. 2001); tafiti nyingine za mwaka 2006 and 2007 zote zilionesha kuwa idadi ya ndege hawa haikubadilika (J. John in litt. 2007).

Jambo la kusikitisha, ndege hawa wanauwawa na wanazidi kupungua idadi yake kutokana na uchafuzi wa mazingira unaoendelea katika safu za milima hii ya Uluguru kwa kuchoma moto ovyo.
Wananchi wote wanaoishi karibu na safu hizi za milima ya Uluguru washirikiane katika kuhifadhi mazingira na kuwalinda hawa ndege adimu duniani ili tuweze kukuza uchumi wetu na kupata fedha za kigeni kupitia utalii.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...