Wednesday, November 14, 2012

KINANA AUKWAA UKATIBU MKUU CCM

 KINANA AUKWAA UKATIBU MKUU CCM
 Mkutano mkuu wa 8 wa Chama Cha Mapinduzi NEC mjini Dodoma, ambao ndo uko ukingoni umempitisha Abdulhaman Kinana kuwa katibu mkuu wa chama  tawala.


Pia mkutano huo umemchagua kwa 100% Katibu Mkuu wa zamani, Philip Mangula, kuwa Makamu Mwenyekiti, akirithi mikoba ya Pius Msekwa.

Naye Mwigulu Nchemba amechaguliwa kuwa naibu katibu mkuu wa chama hicho upande wa bara na Vuai Ali Vuai upande wa Zanzibar.

Wengine waliofanikiwa kupita kwenye secretarieti ya chama hicho ni pamoja na Asha Rose Migiro ambaye amechaguliwa kushughulikia masuala ya kimataifa na Zakhia Meghji amechaguliwa kushika nafasi ya uweka hazina.

Nape Nnauye ameendelea kushikilia nafasi yake katibu na uenezi wa chama hicho.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...