Tuesday, November 6, 2012

FAHARI YA MOROGORO ISIYOTHAMINIWA.
Mji wa Morogoro umezungukwa na milima ya Uluguru ambayo ina vivutio mbali mbali ikiwa ni pamoja na wanyama adimu aina ya MBEGA.Milima hii ni tegemeo kubwa la vyanzo vya maji katika mikoa ya Morogoro,Pwani na Dar es salaam.Bwawa la Mindu ambalo linategemewa na wakazi wa Manispaa ya Morogoro linaloundwa na mito mitano yote inaanzia katika safu za milima ya Uluguru.
Milima hii kipindi cha miaka ya sabini maji yalikuwa yakitiririka milimani lakini kama inavyoonekana watu wameivamia milima hii na kuendesha shughuri mbali mbali kama kilimo na uwindaji wa wanyama.Kutokana na uharibifu huo kwa sasa hali ya maji inazidi kuwa mbaya.
Jamani tushirikiane wote katika kurudisha hali ya milima hii ya Uluguru.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...