Tuesday, November 6, 2012

HATARI! HATARI! HATARI!
Hii ni hatari kwa wakazi wa Manispaa ya Morogoro wanaonunua maji kutoka kwenye magari yanayouza maji mitaani.Magari haya badala ya kununua maji katika vioski vya kuuzia maji vilivyo mjini yanaenda eneo la Mindu darajani na kuchota maji yasiyo tibiwa na kwenda kuwauzia wananchi.
Kibaya zaidi nikwamba magari hayo yameandikwa majisafi hivyo wananchi wanayaamini kumbe mambo ni tofauti.
Kulikuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi kuwa MORUWASA inasambaza maji yasiyosafi na salama baada ya kutumia maji kutoka kwenye magari hayo yanayowadanganya watu kuwa wamenunua maji kutoka MORUWASA.Mojawapo ni gari T 706 AAF lililoandikwa majisafi,naomba wahusika wafatilie suala hili kwa karibu ili kunusuru afya za wananchi.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...