Tuesday, November 6, 2012

UZEMBE KAZINI.
Hapa ni mchezo wa makida unachezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro katika suala zima la utupaji wa taka ngumu.Jambo la kusikitisha nikwamba magari yanamwaga taka hadi barabarani baada ya kujizibia barabara ya kuingia dampo.
Swali langu ni,je,muhusika wa taka ngumu huwa anatembelea dampo hili? Na kama anatembelea ni  hatua gani kazichukua katika kutatua tatizo hili?
Jambo jingine la kusikitisha nikwamba magari haya ya takangumu yameanza kumwaga taka hizo nje ya uzio kwa uzunguka uzio huo na kuzichoma moto nje ya dampo.
Jamani,tujali afya za wananchi popote tulipo na tujenge utamaduni wa uhifadhi na utunzaji wa mazingira.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...