Tuesday, November 6, 2012

UHARIBIFU WA MAZINGIRA.
Matumizi ya nishati ya misitu katika viwanda vyetu hata Morogoro yanazidi kuongezeka kiasi kwamba viwanda vingine vinatumia kuni kuendeshea mitambo ili kukwepa gharama za umeme.Kiwanda kimojawapo kinachotumia  kuni kuendeshea mitambo yake ni 21st Century Textiles Ltd.
Haya ni magogo yaliyorundikwa kusubiria kutumika.Jamani,kutengeneza msitu inaweza kutuchukua muda si chini ya miaka kumi lakini ufyekaji unaweza kufanyika ndani ya siku kadhaa tu.Kibaya zaidi hawa wanaokata miti ukiwauliza wamepanda mingapi utaambiwa hawajapanda mti hata mmoja.
Watanzania tuamke,tutunze mazingira yetu ili hata vizazi vijavyo vikute hizi rasilimali tulizonazo.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...