Tuesday, July 2, 2013

MATUKIO KAMILI YA SIKU YA KWANZA YA ZIARA YA OBAMA TANZANIA.

Rais Barack Obama wa nchini Marekani na Mkewe Michelle Obama wakiwa sambamba
na watoto zao,wakiwasili chana huu kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa
wa Mwalimu Nyerere,jijini Dar es Salaam mchana huu kwa ziara ya siku
mbili hapa nchini.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Barrack Obama wa Marekani
muda mfupi baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius
Nyerere jijini Dar es Salaam mchana wa leo. Kulia ni Mke wa Rais Mama
Salma Kikwete.

Rais Dkt.Jakaya Kikwete akiwa na mgeni wake Rais Barrack Obama wa Marekani
muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa
Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo mchana.nyuma ya Rais na
mgeni wake ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na mke wa Rais wa Marekani
Mama Michelle Obama.

Rais Barrack Obama akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa na jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ).

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa
Marekani Rais wa Zanzibar Dr.Ali Mohamed Shein muda mfupi baada ya
kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini
Dar es Salaam leo mchana.Huku Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Mke wa
Rais wa Marekani Michelle Obama Wakiangalia.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa
Marekani makamu wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Iddi muda mfupi baada ya
Rais huyo wa Marekani kuwasili nchini kwa Ziara ya kikazi ya siku
mbili.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa
Marekani makamu wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Iddi muda mfupi baada ya
Rais huyo wa Marekani kuwasili nchini kwa Ziara ya kikazi ya siku
mbili.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange akisalimiana
na Rais Barrack Obama katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere jijini
Dar es Salaam jana.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiwaongoza wageni wao Rais Barrack Obama wa Marekani na mkewe Michelle kuangalia ngoma mbalimbali
za utamaduni muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Mwalimu Nyerere kwa ziara ya siku mbili nchini.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiwaongoza wageni wao Rais Barrack Obama wa Marekani na mkewe Michelle kuangalia ngoma mbalimbali
za utamaduni muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Mwalimu Nyerere kwa ziara ya siku mbili nchini.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais Barrack Obama wa Marekani
wakifurahia na kufuata mapigo ya ngoma za utamaduni katika uwanja wa
Ndege wa Mwalimu jijini Dar es Salaam jana mchana wakati wa mapokezi ya
kiongozi huyo wa Marekani na ujumbe wake.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiwatambulisha baadhi ya viongozi waandamizi
wa serikali kwa Rais Barrack Obama na mkewe katika uwanja wa ndege wa
Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam jana.Picha na Freddy
Maro,Ikulu.
Rais Barack Obama wa Marekani na mkewe Michelle Obama wakipokewa kwa Shangwe Ikulu,Jijini Dar es salaam mchana wa jana


Rais Barack Obama wa Marekani na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakipokewa kwa Shangwe Ikulu,Jijini Dar es salaam jana.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongozana na mgeni wake,Rais Barack Obama wa Marekani wakati walipokuwa wakielekea sehemu iliyoandaliwa kwa ajili ya kukutana na kuzungumza na Waandishi wa habari Ikulu,Jijini Dar es salaam jana.






Obama akipanda mti Ikulu ya Tanzania jana.


No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...