Monday, June 24, 2013

WATU 10 WAMEUAWA HOTELINI- PAKISTAN.


Watu 10 wameuawa katika hoteli,kaskazini mwa   Pakistan ikiwa pamoja na watalii tisa .
Watu waliokuwa na silaha waliivamia kambi moja ya  sehemu hiyo ya Nanga Parbat na kuwaua  watalii hao.
Kwa mujibu wa taarifa, waliouawa walikuwa raia wa Ukraine,Urusi na China.
Msaidizi wa watalii,mwenyeji wa sehemu hiyo pia aliuawa.
Marekani pia imethibitisha kwamba raia wake mmoja alikuwa miongoni mwa waliouawa.
Washambuliaji 15 waliojifanya kuwa ni polisi waliivamia kambi hiyo katika jimbo la Gilgit-Baltistan
Kwa mujibu wa taarifa za mashirika ya habari, Taliban wamedai kuhusika na mashambulio hayo.
Msemaji wao ameeleza kuwa watu hao wameuliwa  kulipiza kisasi kifo cha makamu kiongozi wa Taliban ,Wali ur Rehman alieuliwa katika shambulio la  mwezi uliopita lililofanywa na ndege ya Marekani inayoruka bila ya rubani.

Source: DW

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...