Tuesday, June 4, 2013

REMEDIAL PROGRAMME - SAINT AUGUSTIN UNIVERSITY OF TANZANIA.

  
                                                        TANGAZO
Chuo cha Mtakatifu Agustino Tanzania kinawatangazia nafasi za kujiunga na Remedial Programme kwa mwaka wa masomo 2013/2014.Kozi hii ni kwaajili ya wale wote ambao alama zao hazifiki kiwango cha 4.5 katika kidato cha sita, ili kuwawezesha kupata elimu ya ziada iwasaidie kuendana na wanafunzi wenzao walio pata alama za 4.5 katika kidato cha sita.

Sifa za Muombaji:
1. Awe amemaliza kidato cha sita.

2. Awe na Principal Points kuanzia 2.5 hadi 4 kwenye masomo mawili ya kidato cha sita (mfano: EE, DE, CE, DD, EEE na masomo mengine kuwa na S).

3. Gharama ni Tshs. 390,000/= (Tuition Fee) kwa miezi 3, malazi (accommodation) ni Tshs. 70,000/=, chakula ni kujitegemea.

4. Wale wote wenye sifa hizo watakao chaguliwa na TCU kuja SAUT watatakiwa kufika chuoni miezi mitatu kabla ya tarehe ya kujiunga chuoni kwaajili ya kuanza masomo ya remedial.

5. Kozi hii itaanza tarehe 3/7/2013.

Fomu zinapatikana ofisi ya Admissions na kwenye tovuti (www.saut.ac.tz). Baada ya kumaliza kujaza fomu zirudishwe ofisi ya Admissions-SAUT. Wahitimu wataruhusiwa kujiunga na vyuo vyote vilivyo chini ya SAUT.

Wote mnakaribishwa.

Admissions Officer

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...