Wednesday, June 5, 2013

MAMA MANGWEA HALI TETE WAKATI MWILI WA MAREHEMU UKISUBIRIWA.

Mama mzazi wa marehemu Albet Mangwea Bi.Denisia Mangwea akiwa kitandani nyumbani kwake kihonda mazimbu road muda mfupi baada ya kutoka hospital ya mkoa wa Morogoro alikokuwa amelazwa baada ya kuanguka ghafla baada ya kuelezwa kwamba mwili wa mwanae ulishindwa kuwasili nchini juzi kama ilivyolipotiwa awali.

Leo blog hii ilifika tena nyumbani kwa mfiwa huyo kwa lengo la kumjulia hali na kujua hali ya maandalizi ambapo alipohojiwa alidai kwamba bado afya yake haijatengemaa.

Hata hivyo alisema vyovyote itajkavyo kuwa ni razima ashiriki kikamilifu ibada na mazishi ya mwane kitinda mimba.

 Albaet aliyekufa ghafla nchini Afrika kusini jumanne ya wiki iliyopita.Mwili wa msanii huyo unatarajiwa kuzikwa jirani na kaburi la marehemu baba yake Mzee Keneth Mangwea kwenye makaburi ya Kihonda yaliyopo nje ya kanisa la Mtakatifu Monica kesho Alhamisi.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...