Friday, June 21, 2013

MAFURIKO YAUA WATU ZAIDI YA 300 INDIA.

Makundi ya waokoaji yanaendelea kuwatafuta walionusurika katika mafuriko yaliotokea katika jimbo la Uttarakhand nchini India leo, huku maafisa wakisema karibu watu 300 wamekufa.
Taarifa zinasema zaidi ya watu 13,800 wamepotea na wengine 62,800 wangali wamenasa katika maeneo hayo  karibu na miji ya shughuli za  hija za  waumini wa kihindu ya  Badrinath na Kedarth.
Picha za televisheni zimeonyesha watu wakipanda mabonde, huku wakisaidiwa na wanajseshi. Hadi sasa karibu watu 56,000 wameokolewa.

Source: DW

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...