Monday, June 10, 2013

MKUU WA MAJESHI LIBYA AJIUZURU.

Mkuu wa majeshi nchini Libya Youseff al Man Gous amejiuzulu siku moja baada ya ghasia mashariki mwa mji wa Benghazi kusababisha vifo vya watu 31.Ghasia hizo zilizuka siku ya Jumamosi wakati waandamanaji walipovamia kambi ya kundi la wanamgambo wanaojulikana Shield wanaoiunga mkono serikali.Kundi hilo pia ndilo lililo na jukumu la  kulinda amani katika eneo hilo la Benghazi.Waandamanaji hao walikuwa wanataka wanamgambo hao wakabidhi madaraka ya kiusalama kwa  kikosi rasmi cha usalama cha Libya na wasalimishe silaha zao. Bunge la kitaifa la Libya limetangaza kujiuzulu kwa Youseff  ambaye ameshutumiwa kwa kuchelewa kuunda jeshi la kitaifa na kutangaza pia siku tatu za maombolezi.

Source:DW

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...