Tuesday, March 26, 2013

WANANCHI WA KIBAHA WALIGOMEA GARI LA HALMASHAURI LISIMWAGE TAKA

Wakazi wa Kibaha kwa Mfipa wakilisimamia gari lisimwage taka.
Wakazi wa Kibaha kwa Mfipa waliligomea gari la Halmashauri ya Mji Kibaha lenye nambari za usajili SM 3231 lisimwage taka katika eneo lao kutokana na kuwa taka hizo zinamwagwa juu ya calvat na zinasababisha kuzibisha calvat hilo na kufanya maji yajae kwenye makazi ya watu.
Gari la H/Mji lililozuiliwa kumwaga taka na wakazi wa Kibaha kwa Mfipa.
 Wakazi hao wamefikia hatua hiyo baada ya gari hilo kushindwa kwenda machimbo eneo ndiko yanakomwaga taka hizo baada ya barabara ya kwenda huko kujazwa vifusi na kusababisha magari yasiweze kupita.
Calvat la maji ya mvua
 Uchunguzi wa blogu hii umebaini kuwa maji katika calvat yanasafiri kwa taabu sana baada ya taka ngumu kujaa katika mkondo wa maji.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...