Wednesday, March 6, 2013

UBORA WA MAJI WALETA KIZAAZAA MORO,MBUNGE AITEMBELEA MORUWASA KUJIONEA HALI HALISI.

Mbunge wa Morogoro Mjini Mh.Azizi Abood.
Wakazi wa Manispaa ya Morogoro jana walimvamia Mbunge wao Mh.Azizi Abood wakilalamikia ubora wa maji yaliyosambazwa mtaani kwao kuwa yalikuwa chini ya kiwango.Kutokana na malalamiko hayo ilimlazimu mbunge wa Morogoro Mjini kufanya ziara ya ghafla katika ofisi za Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira MORUWASA ili kujua kulikoni.
Gari la Mh.Mbunge alipowasili MORUWASA.
Akielezea sababu zilizopelekea kupungua ubora wa maji Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA Ndg.John K.Mtaita alisema hali hiyo ilitokana ukarabati wa sehemu ya kutibia maji Mafiga na usafishaji wa machujio ya maji.Hata hivyo,mkurugenzi huyo aliwaahidi wakazi wa Morogoro kuwa ubora wa maji utaimarika maradufu baada ya mradi wa ukarabati wa miundombinu utakapokamilika.
Mafundi wakiendelea na matengenezo ya bomba Msamvu stendi ya Dodoma.
 Hata hivyo,mbunge huyo aliweza kutembelea hata eneo la Msamvu ambapo bomba linatengenezwa ili wakazi wa Kihonda waweze kupunguziwa adha ya ukosefu wa maji.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...