Showing posts with label MTAANI KWETU. Show all posts
Showing posts with label MTAANI KWETU. Show all posts

Thursday, January 9, 2014

NYUMBA YATEKETEA KWA MOTO KUTOKANA NA HITIRAFU YA UMEME - MOROGORO.

Wananchi wakiwa wanajaribu kuvunja dirisha ili waweze kuzima moto .

Nyumba moja ailiyotambulika kuwa mmiliki wake ni Mama Mkambala mtaa wa Uhuru Manispaa ya Morogoro, jana jioni iliteketea kwa moto baada ya kutokea hitirafu ya umeme. Kutokana na juhudi zilizofanywa na Wananchi kwa kushirikiana na Kikosi cha zima moto, moto uliweza kudhibitiwa usiweze kusambaa kwenye nyumba za jirani. Katika kazi hiyo ya kuzima moto changamoto ilikuwa ni namna ya kuingia ndani ya nyumba baada ya nyumba hiyo kuwa imefungwa.
Hata hivyo, thamani halisi ya mali zilizoteketea bado haijafahamika na hakuna majeruhi yeyote kutokana na moto huo.

Wednesday, May 8, 2013

MTOTO WA MIAKA 3 AKUTWA AMEKUFA MTO MOROGORO.


Mtoto mwenye umri wa miaka 3 aitwaye Issa Iddi amekutwa amekufa katika mtkondo wa mto Morogoro eneo la Mafisa karibu na Mabwawa ya majitaka yanayomilikwa na MORUWASA.Tukio hilo limetokea leo asubuhi ambapo wakulima wa mpunga wamekuta maiti ya mtoto huyo imenasa.
Maiti ya mtoto Issa Iddi aliyekutwa amekufa mto morogoro.
Bofya Read more kuendelea.

Sunday, April 21, 2013

Breaking news: HUDUMA ZA USAFIRI WA TRENI DAR KUANZA JUMATATU APRILI 22.

 Huduma za usafiri wa treni katikati ya jiji la dar es salaam zinatarajiwa kuanza tena Jumatatu Aprili 22 kufuatia kukamilika kwa Ukarabati wa reli katika eneo lililokuwa limeharibiwa na mvua zilizonyesha hivi karibuni na kwamba hakuna badiliko la nauli.
Taarifa kamili tutawaletea baadae.

Friday, April 19, 2013

TANGAZO KUTOKA KWA DIAMOND JUU YA WATU WANAOTUMIA SOCIAL NETWORK KUFANYA UTAPELI KUPITIA JINA LAKE

Katika mtandao wa kijamii wa Msanii maarufu Diamond,ametoa tangazo linalotaadhalisha wanachi wasije tapeliwa.
Tangazo lenyewe hili hapa:-
 
"Napenda kuwataharifu fans wangu kuwa...kuna tabia imekuwa
 ikijotekeza kwenye social networks.
Tabia hiyo imekuwa ya kitapeli ya kufungua account
mbalimbali kupitia social networks
na kuanza kutuma massage za ajabu.....jambo ambalo
mimi binafsi sipendezwi nalo.....
nimelivumilia lakini nikaona isiwe vibaya nikiwajuza tena
 kuwa mkipata ujumbe wowote
kupitia social network kupitia jina langu kuomba
 msaada mtambue kabisa
si kweli......Jambo lolote kuhusiana na mimi binafsi utapata
 updates zangu kupitia
Account yangu ya facebook by Diamond platnumz ambayo ipo
 connected na tweeter
&Instangram pekee......lakini vinginevyo
sintousika na tuhuma zozote.....

Binafsi nimeshangzwa na ujumbe huu wa mtu ambae anatumia account facebook kwa jina
la Diamond platnum,kwa kuwasambazia ujumbe ufuatao:

KARIBU KTK PARTY YA KIMYA KIMYA YA KUMSHUKURU MAMA YANGU MPENDWA MAMA NASEEB.
KADI YA MWALIKO INAPATIKANA ATRIUM HOTEL BAADA YA KUTOA MCHANGO WAKO
ITAFANYIKA KTK MJENGO WANGU MPYA WA KISASA ULIOPO TEGETA NEXT WEEK.
THIS PARTY IS 4 ONLY INVITED PEOPLE..COZ IS SUPRIZING CELEBRATION PARTY
KADI ZINATOLEWA KUANZIA SAA 10JIONI HADI SAA3 USIKU MARA BAADA YA KUPOKELEWA MCHANGO WAKO.
MCHANGO NI KIASI CHOCHOTE NA UTUMWE KTK NAMBA YANGU YA TIGO.
KARIBU..
078889889 hy ndo namba yake
NB: MARA UTUMAPO MCHANGO WAKO UTAPOKEA SMS YENYE NENO LA SIRI AMBALO UNATAKIWA KUFIKA NALO KWA MUHUSIKA NA KULITAJA.
NIMEWEKA MCHANGO KUPUNGUZA IDADI YA WATU...
Niliuzunika sana kwa mambo kama haya bado kuendelea kufanyika kwenye social networks......
ni hayo tu my truly fans wa Diamond i hope mmeninyaka wote....... PEACE & LOVE"

Saturday, April 13, 2013

Breaking news: GARI LA MASAMA LAPATA AJARI ENEO LA WAWI NA MTU MMOJA AFARIKI DUNIA

Habari zilizotufikia hivi punde, gari la kampuni ya Masama limepata ajari na mtu mmoja ameripotiwa kufa na wengine kupatata majeraha kadhaa.
Habari kamili tutawaletea kadiri tutakavyokuwa tunazipata.

Friday, April 12, 2013

KATIKA SAKATA LA KUPANDISHWA KWA NAULI,SUMATRA YAKAMATA MAGARI 75 KWA KUPANDISHA NAULI KABLA YA MUDA


 Wakati nauli mpya zikianza kutumika leo, Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchikavu (Sumatra) imekamata magari ya kubeba abiria (daladala) 75 katika operesheni maalum iliyoanza mwanzoni mwa wiki hii katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

Uamuzi wa kukamata magari hayo umekuja baada ya kuwepo kwa malalamiko ya baadhi ya abiria ya kutozwa nauli kubwa kuliko iliyotangazwa na Serikali kuwa zianze kutumika leo.

Waziri wa Uchukuzi, Harrison Mwakyembe alisema jana mjini Dodoma kuwa ongezeko la viwango vipya vya nauli si tatizo, la muhimu ni wahusika kufuata vigezo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Mfawidhi Kanda ya Mashariki wa Sumatra, Conrad Shio alisema kuwa,daladala zilizokamatwa zilikuwa na makosa mbalimbali yakiwemo kukatisha ruti, kutoza nauli, kuiba ruti na kufanya biashara ya kusafirisha abiria bila ya kuwa na kibali.

Alisema kutokana na hali hiyo wamiliki wa daladala zilizokamatwa wametakiwa kwenda na mikataba ya madereva wapya, ili wale wa zamani waweze kukaguliwa na Jeshi la Polisi Tanzania juu ya uhalali wa leseni zao.

“Tumepata malalamiko ya daladala 105 ambazo zimekuwa zikivunja sheria ya usafiri barabarani, ambapo daladala 75 tayari tumezikamata,” alisema Shio.
Aliongeza kati ya hizo, daladala 36 zilikatisha ruti, wakati 18 ziliiba ruti na 21 zilitoza nauli kubwa, jambo ambalo limewafanya wazichukulie hatua.
Alisema kuna nyingine zimebeba abiria bila ya kuwa na kibali, ambapo wamiliki wake wamechukuliwa hatua za kisheria.

Alisema kutokana na hali hiyo, wamiliki wa daladala hizo wametakiwa kulipa faini na kwenda na mikataba ya madereva wapya ili madereva waliofanya makosa wachukuliwe hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani. Alisema daladala ambazo zilikuwa zinafanya kazi bila ya kibali hasa nyakati za usiku katika baadhi ya maeneo zimepelekwa kwenye yadi ya Serikali ili wamiliki wake waweze kuchukuliwa hatua za kisheria kwa sababu ni kosa kubeba abiria wakati huna kibali cha usafirishaji.

Alisema kuwa, ili kupunguza ukubwa wa tatizo, wamelifanya zoezi hilo kuwa endelevu ikiwa ni pamoja na kuwataka madereva wa vyombo vya usafiri kufuata sheria na taratibu zilizowekwa ili kupunguza malalamiko. Alisema kutokana na hali hiyo Sumatra itaendelea kukamata magari ambayo yataonekana yanaendelea kuvunja sheria kwa makusudi.

Habari hii ni kwa mujibu wa Mwananchi

Tuesday, April 2, 2013

UKOSEFU WA MAJI NA KIBONZO CHA MASOUD KIPANYA LEO

Hii ni habari iliyokatika mfumo wa kibonzo,lakini kutokana na hali halisi ilivyo huko mitaani maeneo mengi ya Tanzania kibonzo hiki kinaweza kuwa kweli.

Thursday, March 28, 2013

TETE BEACH PUB KUWAKA MOTO PASAKA HII NA Y2K SOUND

Sikukuu ya Pasaka Y2K SOUND MOROGORO itawasha moto katika viwanja vya Tete Beach Pub iliyoko Kihonda- Mazimbu road.

MaDj waliobobea wa Y2K Sound akiwemo Dj.R,Dj.Shebi zee, Dj.Parein watakuwa wanabengisha na kuwaburudisha wakazi wa Morogoro.

Katika burudani hiyo, mtu atahitajika kununua kinywaji tuu na kuendelea kuburudika.

Tuesday, March 26, 2013

WANANCHI WA KIBAHA WALIGOMEA GARI LA HALMASHAURI LISIMWAGE TAKA

Wakazi wa Kibaha kwa Mfipa wakilisimamia gari lisimwage taka.
Wakazi wa Kibaha kwa Mfipa waliligomea gari la Halmashauri ya Mji Kibaha lenye nambari za usajili SM 3231 lisimwage taka katika eneo lao kutokana na kuwa taka hizo zinamwagwa juu ya calvat na zinasababisha kuzibisha calvat hilo na kufanya maji yajae kwenye makazi ya watu.
Gari la H/Mji lililozuiliwa kumwaga taka na wakazi wa Kibaha kwa Mfipa.
 Wakazi hao wamefikia hatua hiyo baada ya gari hilo kushindwa kwenda machimbo eneo ndiko yanakomwaga taka hizo baada ya barabara ya kwenda huko kujazwa vifusi na kusababisha magari yasiweze kupita.
Calvat la maji ya mvua
 Uchunguzi wa blogu hii umebaini kuwa maji katika calvat yanasafiri kwa taabu sana baada ya taka ngumu kujaa katika mkondo wa maji.

Monday, March 25, 2013

GARI LAFUNGA BARABARA YA DAR - MORO KWA MASAA KADHAA RUVU BAGAMOYO

Askari polisi wakisimamia usalama
Gari roli lenye namba za usajiri T451ARW liligongana na roli lenye namba za usajiri T475BNA eneo la Ruvu Wilaya ya Bagamoyo na kusababisha foleni kwa magari yanayotoka chalinze kwenda Dar na kutoka dar kwenda Chalinze.Foleni hiyo ilidumu kwa takribani muda usiopungua masaa matatu.
Foleni baada ya gari kuziba barabara
Kivutio zaidi ni pale vijana wapao 7 waliokuwa wakipakiza chokaa huku wakiwa hawana hata mask za kuzuia vumbi lisiwadhuru.
Vijana wakipakia chokaa




Wednesday, March 20, 2013

SAMAKI WA MAJITAKA WAHISIWA KUUZWA KWA WATU MJINI MOROGORO


Katika hali ya kushangaza na kusikitisha, nikwamba vijana wenyeji wa Manispaa ya Morogoro wamekutwa wakikusanya samaki aina ya kambale katika mabwawa ya majitaka yanayotolewa tope ya Mafisa.
 Walipoulizwa wakasema wanaenda kula lakini uwalakini unakuja pale walipoonekana kukazana kukusanya samaki wengi na kwenda kuwasafisha.
 Wito wangu kwa wakazi wa Morogoro kuweni makini na samaki wanaouziwa na watu mitaani na kwa wale wenye mabucha kuweni waaminifu kwa kutonunua samaki watakao letwa kwao na vijana wa mtaani.
Na maafisa afya kuweni makini kwa kukagua samaki wanaouzwa kwenye mabucha na mitaani.

Wednesday, November 14, 2012

UKUAJI WA TEKNOLOJIA





UKUAJI WA TEKNOLOJIA
Ndg.wanamichezo,wabunifu wameweza kuwatolea simu ambazo zinaendana kimichezo.Hii ni simu ambayo inaumbile la mpira lakini inashika mtandao vizuri sana na ni rahisi kubebeka,ina nafasi ya kuweka line mbili.Yeyote atakayeihitaji tuwasiliane.

Tuesday, November 13, 2012

UBUNIFU.COM


Huu ni ubunifu uliopatikana mji kasoro bahari Morogoro,huyu kabadirisha piki pikiya tairi 2 na kuifanya daladala kwa kuiongezea kikapu nyuma na kuifunga turubai ili abiria wasiweze kunyeshewa mvua wala kupigwa jua.
Watanzania tunatakiwa kuendeleza vipaji tulivyikuwa navyo ili tuweze kuendelea.

Tuesday, November 6, 2012

Y2K SOUND - WAZEE WA KUWAPOTEZA.

Y2K SOUND - WAZEE WA KUWAPOTEZA.
Kwa mahitaji ya muziki katika shughuri mbali mbali ikiwa ni pamoja na harusi,send off,kitchen party,graduations,tafrija,shughuri za kidini, kisiasa n.wasiliana ya Y2K SOUND MOROGORO watakuhudumia.
Mawasiliano: 0755674418/0714628954

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...