Friday, March 8, 2013

UHAMASISHAJI JUU UTUNZAJI WA RASILIMALI MAJI BONDE LA WAMI/RUVU

Afisa Maendeleo ya Jamii Bonde la Wami/Ruvu Bi.Nickbar Mwanana Ally akitoa mada wakati wa uelimishaji juu ya zana shirikishi katika usimamizi wa pamoja wa rasilimali maji katika Shule ya Msingi Kisemu-Mtamba Morogoro vijijini.
Katika kuhakikisha rasilimali maji inakuwa endelevu,Bonde la Wami/Ruvu linafanya jitihada za kuwahamasisha na kuwaelimisha wanchi wa Mikoa ya Dodoma,Morogoro,Pwani,Tanga na Dar es salaam juu ya utunzaji wa rasilimali hiyo.
Wakazi wa Morogoro vijijini kutoka vijiji 13 wakishiriki mafunzo katika shule ya msingi Kisemu-Mtamba

Ofisi ya Bonde la Wami/Ruvu inaendesha mpango wa ZANA SHIRIKISHI KATIKA USIMAMIZI WA PAMOJA WA RASILIMALI MAJI.Mpango huu unaendeshwa katika vijiji vyote na wananchi wanahamasishwa kushiriki katika shughuli za utunzaji vyanzo vya maji.
Miti jamii ya Misederea ambayo wakazi wengi wa Morogoro vijijini na Mvomero wameipanda kwa wingi karibu na vyanzo vya maji bila kuelimishwa wapi mahali bora pakupanda.Ukweli nikwamba miti hii ni hatari kuipanda karibu na vyanzo vya maji maana inanyonya maji kwa kasi sana.
Maofisa wa ofisi za Bonde la Wami/Ruvu wakichota maji katika moja ya chanzo cha maji Morogoro vijijini.Vyanzo vya maji vikitunza vizuri ni hazina ya sasa na kwa kizazi kijacho.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...