Thursday, March 14, 2013

PAPA MPYA APATIKANA HUKO VATICAN

Papa Jorge Mario Bergoglio akisalimiana na Papa aliyejiuzulu.
Hatimaye ile kazi ya kumchagua papa mrithi wa Papa Benedict XVI aliyejiuzulu mwezi Februari imekamilika baada ya Kadinali Jorge Mario Bergoglio kuchaguliwa na  anakuwa mtu wa kwanza kutoka Amerika kusini kuchaguliwa kuwa Papa na  mara tu baada ya kuchaguliwa alichagua jina la Papa Francis I. Awali moshi mweupe ulishuhudiwa ukifuka kutoka kwenye dohani katika kanisa la Sistine Chapel na kufuatiwa na kengele kupigwa.
Papa Fransisco I alipojitokeza kwa mara ya kwanza huko Vatikani
Makadinali 115 wamekuwa faraghani tangu siku ya Jumanne alasiri na wakaanza mchakato wao kwa kupiga kura mara nne kwa siku.
Maelfu ya watu kutoka sehemu mbali mbali duniani walikuwa wamekusanyika katika ukumbi wa Kanisa la St Peter tangu siku ya Jumanne. Muda mfupi kabla ya Kadinali Bergoglio kujitokeza , maelfu ya watu walionekana wakikimbia kuelekea ukumbi wa St Peters ili kuweza kumshuhudia Papa mpya akitangazwa

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...