Wednesday, March 20, 2013

SAMAKI WA MAJITAKA WAHISIWA KUUZWA KWA WATU MJINI MOROGORO


Katika hali ya kushangaza na kusikitisha, nikwamba vijana wenyeji wa Manispaa ya Morogoro wamekutwa wakikusanya samaki aina ya kambale katika mabwawa ya majitaka yanayotolewa tope ya Mafisa.
 Walipoulizwa wakasema wanaenda kula lakini uwalakini unakuja pale walipoonekana kukazana kukusanya samaki wengi na kwenda kuwasafisha.
 Wito wangu kwa wakazi wa Morogoro kuweni makini na samaki wanaouziwa na watu mitaani na kwa wale wenye mabucha kuweni waaminifu kwa kutonunua samaki watakao letwa kwao na vijana wa mtaani.
Na maafisa afya kuweni makini kwa kukagua samaki wanaouzwa kwenye mabucha na mitaani.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...