Thursday, March 28, 2013

MENEJA MASOKO WA KAMPUNI YA VINGAMUZI VYA STAR TIMES APANDISHWA KIZIMBANI KWA UDANGANYIFU


Meneja Masoko wa Kampuni ya ving’amuzi ya Startimes, David Kisaka (37) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, kujibu shtaka la kujipatia vitu kwa njia ya udanganyifu.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Nassoro Katuga alidai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 5, mwaka huu eneo la Akiba, Wilaya ya Ilala.
Katuga alidai siku hiyo ya tukio katika eneo hilo, mshtakiwa kwa njia ya udanganyifu alijipatia ving’amuzi 110 na Antena 30 za StarTimes vikiwa na thamani ya Sh8.4 milioni mali ya Jonathan Mkanaka.
Antena ya nje inayotumika na vingamuzi vya Startimes
 Mshtakiwa alikana shtaka na hakimu Joyce Minde aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 22, mwaka huu itakapotajwa tena. Mshtakiwa yupo nje ya dhamana baada ya kupata wadhamini wawili wa kuamina ambao walisaini bondi ya Sh6 milioni.

Habari  hii ni kwa hisani ya Mwananchi.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...