Friday, March 15, 2013

UCHIMBAJI HARAMU WA MADINI KANDO MWA MTO RUVU

Wakazi wa kijiji cha Kibangile, Morogoro vijijini wakiwa wanaendelea na uchimbaji haramu wa madini.
 Kumekuwa na kasumba ya wananchi kulalamika kuwa mara mvua hamna, mara jua kali na pia tumekuwa tukiwasikia viongozi na wataalamu mbali mbali wakitueleza kuwa kuna mabadiliko ya tabia nchi ulimwenguni kote, lakini ukija kuchunguza zaidi utangundua kuwa tatizo hilo linaanzia kwa mtu mmoja mmoja hadi kikundi hatimaye kidunia.
Uchimbaji madini kando mwa mto Ruvu
Uharibifu wa mazingira mmojawapo unaoendelea ni uchimbaji haramu wa madini unaoendelea hasa kando kando mwa mito na zaidi mto Ruvu ambao ni mto tegemezi wa vyanzo vya maji kwa mikoa ya Pwani na Dar es salaam ambapo kingo za mto zinaharibiwa na kusababisha maji kusambaa na kuleta mafuriko ikinyesha mvua.
Ofisi ya Bonde la Wami/Ruvu imekuwa na juhudi mbali mbali katika kuhakikisha uchimbaji haramu wa madini hauendelei katika kingo za mito ili kuifanya rasilimali maji inakuwa endelevu.
Uharibifu wa kingo za mto
Mfano ni uchimbaji unaoendelea katika kijiji cha KIBANGILE Wilaya ya Morogoro Vijijini ambako makundi ya watu yamekutwa wakichimba madini, hapa swali ni je,viongozi wa vijiji na kata hawawaoni au nao wanashirikiana nao katika kazi hiyo?

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...