Showing posts with label KIDIGITALI. Show all posts
Showing posts with label KIDIGITALI. Show all posts

Thursday, March 28, 2013

MENEJA MASOKO WA KAMPUNI YA VINGAMUZI VYA STAR TIMES APANDISHWA KIZIMBANI KWA UDANGANYIFU


Meneja Masoko wa Kampuni ya ving’amuzi ya Startimes, David Kisaka (37) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, kujibu shtaka la kujipatia vitu kwa njia ya udanganyifu.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Nassoro Katuga alidai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 5, mwaka huu eneo la Akiba, Wilaya ya Ilala.
Katuga alidai siku hiyo ya tukio katika eneo hilo, mshtakiwa kwa njia ya udanganyifu alijipatia ving’amuzi 110 na Antena 30 za StarTimes vikiwa na thamani ya Sh8.4 milioni mali ya Jonathan Mkanaka.
Antena ya nje inayotumika na vingamuzi vya Startimes
 Mshtakiwa alikana shtaka na hakimu Joyce Minde aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 22, mwaka huu itakapotajwa tena. Mshtakiwa yupo nje ya dhamana baada ya kupata wadhamini wawili wa kuamina ambao walisaini bondi ya Sh6 milioni.

Habari  hii ni kwa hisani ya Mwananchi.

Wednesday, March 27, 2013

KIJANA UMRI WA MIAKA 17 AGUNDUA PROGRAMU YA SIMU IITWAYO SUMMLY NA KUWAUZIA YAHOO

Nick D'Aloisio kijana aliyegundua programu
Ni kijana aitwaye Nick D'Aloisio aliyegundua programu ya habari kwenye simu za mkononi iitwayo SUMMLY aliyoigundua Desemba 2011. Baada ya kugundua programu hiyo ameweza kuingia mkataba na kampuni ya YAHOO na atakuwa anafanya kazi katika Kampuni hiyo huku aendelea na masomo yake ya kidato cha 6.
Hata hivyo, kwenye blogu yake,ameweza kuandika maneno yafuatayo kuhusiana na programu hiyo:-
 
" In true Summly fashion, I will keep this short and sweet.

I am delighted to announce Summly has signed an agreement to be acquired by Yahoo!. Our vision is to simplify how we get information and we are thrilled to continue this mission with Yahoo!’s global scale and expertise. After spending some time on campus, I discovered that Yahoo! has an inspirational goal to make people’s daily routines entertaining and meaningful, and mobile will be a central part of that vision.  For us, it’s the perfect fit.

When I founded Summly at 15, I would have never imagined being in this position so suddenly. I’d personally like to thank Li Ka-Shing and Horizons Ventures for having the foresight to back a teenager pursuing his dream. Also to our investors, advisors and of course the fantastic team for believing in the potential of Summly. Without you all, this never would have been possible. I’d also like to thank my family, friends and school for supporting me.

Most importantly, thank you to our wonderful users who have helped contribute to us receiving Apple’s Best Apps of 2012 award for Intuitive Touch! We will be removing Summly from the App Store today but expect our summarization technology will soon return to multiple Yahoo! products - see this as a ‘power nap’ so to speak.

With over 90 million summaries read in just a few short months, this is just the beginning for our technology. As we move towards a more refined, liberated and intelligent mobile web, summaries will continue to help navigate through our ever expanding information universe.

Sincerely,

Nick
Founder"

Hata sisi Watanzania tuige mfano wa kijana huyu na tuweze kuvumbua vitu mbali mbali.

Monday, December 31, 2012


DAR ES SALAAM YATOLEWA KAFARA KWENYE DIJITALI.

Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Prof.Makame Mbarawa.


MKOA wa Dar es Salaam saa 6 kamili usiku wa leo unakuwa wa kwanza kuzimiwa mitambo ya analojia ya utangazaji wa televisheni kwa ajili ya kupokea mfumo mpya wa digitali.

Ikumbukwe kuwa hatua hiyo ya kuhama kutoka analojia kwenda digitali ni utekelezaji wa makubaliano ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa katika hotuba yake ya jana kuashiria uzimaji wa mitambo ya analojia, alisema uzimaji kwa zamu unalenga kuepusha usumbufu kwa wananchi wa Tanzania.

Mbarawa alisema kuwa mchakato huo wa uzimaji wa mitambo utafanyika kama ifuatavyo: Januari 31, 2013 Dodoma na Tanga. Mkoani Mwanza Februari 28, 2013 na Kilimanjaro (Moshi) na Arusha Machi 31, 2013.

Mkoa wa saba kuingia kwenye mfumo wa digitali utakuwa Mbeya ambao mitambo itazimwa Aprili 30, 2013. Utaratibu wa kuzima mitambo ya analojia utakuwa kwa maeneo yenye matangazo ya digitali na kwa yasiyo na miundombinu ya digitali hayatazimwa.

Taarifa ya Waziri inaonesha kwamba miundombinu ya mitambo ya digitali imeenea katika mikoa minane pekee. Mabadiliko hayo yanahusu matangazo kwa njia ya utangazaji wa satelaiti, waya (cable) na redio.

Aidha imeelezwa kwamba watoa huduma za miundombinu ya digitali wamejipanga kusimika mitambo hiyo katika mikoa mingine minane ndani ya miezi minane ijayo.
Lakini kwa upande wa pili wa shilingi,baadhi ya wananchi wanalalamikia ving'amuzi vingine vunakatakata sana mawasiliano,lakini naona ni changamoto.


LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...