Thursday, August 15, 2013

KAULI YA ZITTO KABWE JUU YA VIONGOZI KUWEKA WAZI MALI NA MADENI YAO.

Mbunge wa Kigoma kaskazini mh.Zitto Kabwe katoa maoni yake juu ya uhakiki wa mali na madeni ya viongozi kama ifuatavyo:-
" 'Uwazi wa mali na madeni ya viongozi ni moja ya hatua muhimu kupambana na ufisadi' nimemwambia leo Mama Salome Kaganda wa Sekretariat ya Maadili ya Umma.
Wanasiasa tunajaza fomu kutangaza mali na madeni yetu. Fomu hizo haziwekwi wazi kwa wananchi. Utajuaje kama Kiongozi kasema uwongo? Utawezaje kupambana na uzushi na uwongo dhidi ya viongozi waadilifu lakini wanachafuliwa na wapinzani wake kisiasa? Suluhisho moja tu. UWAZI. Daftari la mali na madeni ya viongozi liwe wazi kwa wananchi. Fomu za mali na madeni ya viongozi wa umma ziwe online. Kiongozi asiyetaka mali na madeni yake kujulikana, akauze vitumbua aache uongozi, hakuna atakayemgusa!
"
Source:Zitto Social media.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...