Wednesday, August 28, 2013

KALI KUTOKA SINGIDA:Wakazi wadai dawa za Kichocho na Minyoo zinawaongezea nguvu za kiume.

Mganga mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Dorothy Gwajima akitoa ufafanuzi wa masuala ya afya kwa waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) waliomtembelea ofisini kwake.
Baadhi ya wananchi wanaomeza dawa za kutibu kichocho na minyoo ya tumbo kupitia mpango wa kudhibiti magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele nchini (NTD), wanadai zinawasaidia kuongeza nguvu za kiume wakati wa tendo la kujamiana.
Mratibu wa mpango huo mkoa wa Singida Yuda Machumu, amesema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari wanaohudhuria mafunzo ya siku nne mjini Singida ya uandishi sahihi wa taarifa zinazohusiana na masuala ya afya.
Amesema kuwa baadhi ya wananchi hao wakishatumia dawa hizo hurudi tena kwa wagawa dawa wakihitaji kupatiwa tena dawa, kwa madai kwamba zinawasaidia sana kuwaongezea nguvu wakati wa kujamiana.
Machumu amesema kuwa tatizo hilo haliwahusu wanaume pekee bali wanawake pia ambao katika halmashauri ya wailaya ya Singida, baadhi yao hufika kwa wagawa dawa kuomba dawa hizo, wakidai zinawasaidia sana kuongeza nguvu ya mwili mara baada ya kumeza.
Akizungumzia tatizo hilo, Machumu amesema siyo kweli kuwa dawa hizo zinaongeza nguvu za kiume, hali hiyo hujitokeza baada ya kuwa dawa hizo zimeua vimelea wa maradhi hayo mwilini ikiwemo wale wa minyoo na kichocho, hivyo mwili kuwa na nguvu mpya.
Kwa mujibu wa Machumu katika kipindi cha mwaka jana, mpango huo ulihudumia zaidi ya watu 850,000 sawa na asilimia 71 ya lengo la kuhudumia watu 1,205,159 kwa mkoa wa Singida.

CHANZO MO BLOG

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...