Tuesday, January 8, 2013

UDHAIFU WA WAKANDARASI WAZAWA KATIKA KAZI ZA UJENZI.
Barabara ya IPO IPO - KIHONDA MAGOROFANI

Umekuwa ni wimbo kuwa kazi nyingi za ujenzi wanapewa wakandarasi kutoka nchi za nje wakati wakandarasi wazawa wakinyimwa kazi.Malalamiko haya yanasikika kila mahali lakini je,sisi wazawa kazi zetu zinaridhisha???.
 
Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ina mkakati mzuri wa kuboresha barabara zake ili ziweze kupitika kirahisi ili kurahisisha  mawasiliano katika maeneo mbali mbali.Miongoni mwa barabara hizo ni ile ya IPOIPO - KIHONDA MAGOROFANI ambayo ilijengwa kwa kiwango cha lami.Ili kusikiliza kilio cha wakandarasi wazawa kuwa hawapewi kazi Manispaa ikampa kazi mkandarasi aitwaye:MAGINGA BUSINESS HOLDINGS CO Ltd,S.L.P. 1523,DODOMA.





Lakini kazi hii ilikuwa chini ya usimamizi wa MHANDISI WA MANISPAA YA MOROGORO,kitu cha kushangaza nikwamba tangu kazi hii ikamilike haina miezi hata mitatu (3) lakini kwa mvua kidogo zilizonyesha tarehe 05/01/2013 zimebomoa barabara hii vibaya sana kiasi cha zile 'slabs' kuondoshwa na mvua pembezoni mwa barabara.

Swali langu ni je,barabara hii itadumu kweli?
Watanzania tuacheni kulalamika tu,tuwajibike na tuwe makini na kazi tunazofanya ili tuweze kuuza soko letu kitaifa na kimataifa.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...