Wednesday, January 30, 2013

MVUA ZILIZONYESHA JANA MOROGORO


Bwawa la Mindu

Jana kulinyesha mvua kubwa sana Mjini Morogoro kiasi cha kuwasababishia madhara baadhi ya wakazi wa Manispaa wanaoishi mabondeni ikiwa ni pamoja na kusombwa kwa baadhi ya nyumba.
Mkazi wa Morogoro akifurahi baada ya mvua kunyesha hiyo jana
Lakini pamoja na kunyesha kwa mvua hizo hali ya maji katika  bwawa la Mindu haikubadilika sana maana mpaka kufika leo saa 9.30 mchana maji yalikuwa yameongezeka kwa kiasi cha sentimeta sita (sm 6),lakini kiasi cha maji yanayoingia bwawani kinaweza kuwa kimebadilika na kuongezeka kufika kesho asubuhi maana mito inaendelea kuingiza maji bwawani.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...