Thursday, January 17, 2013

HUU NI UZEMBE KAZINI USIO VUMILIKA.
Hiki ni kituo cha Afya cha Saba saba katika Manispaa ya Morogoro ambacho ni mojawapo ya ofisi za Serikali.Tarehe 13/11/2012 nilifika katika kituo hiki na kukuta BENDERA YA TAIFA ikiwa inapepea mida ya saa 1 usiku,nikasema labda yule mlinzi mwenye wajibu wa kuishusha anadharula.Lakini kitu cha kushangaza jana  tarehe 16/01/2013 usiku minamo saa 1 usiku pia bendera hiyo imekutwa bado inapepea wakati najua fika kuwa bendera inatakiwa kushushwa saa 12 jioni.

Nimekaa pale mpaka bendera hiyo imekuja kushushwa saa 1.28 usiku.


SWALI langu,ni je,taratibu za kushushwa kwa bendera zimebadilika au ni uzembe tuu wa watu wasiojali kazi zao.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...