Monday, December 31, 2012

HERI YA MWAKA MPYA 2013.

MWENYEZI MUNGU MWENYE KUWEZA KILA JAMBO,AMEWEZA KUKUONGOZA VIZURI MPAKA SASA UNAPUMUA. Una kila sababu ya kumshukuru kwa kila jambo.Niwengi waliuanza huu mwaka wa 2012 lakini katikati safari zao zikakatishwa na uhai wao kuweza kuchukuliwa.

Jiulize kwa mwaka 2012 umefanya nini la kumtukuza mwenyezi mungu,umefanya nini la kuisaidia jamii.Ukishafanya tathimini hiyo jipe jibu na kuweza kujikosoa.

Wengi tunalalamika kuwa hatuna kitu,lakini kusaidia ni moyo sio utajiri.Mtu mwingine unaweza kumsaidia mawazo na akaweza kukwamuka kimaisha.

Nawaomba tupendane wote madamu tunaishi,sote ni ndugu.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...