Monday, January 28, 2013

HABARI ZILIZOVUNJIKA:LULU APEWA DHAMANA


Habari zilizopatikana hivi punde kutoka mahakamani zinasema kuwa Lulu amepewa dhamana na Mahakama kuu ya Tanzania baada ya mawakili wanaomtetea Lulu kuwasilisha ombi la dhamana mahakamani hapo.
Mawakili hao ambao ni Peter Kibatala, Kennedy Fungamtama na Fulgence Massawe waliiomba mahakama hiyo itoe dhamana haraka kwakuwa mteja wao amekaa mahabusu kwa zaidi ya miezi saba na kwamba kosa lake linaweza kupewa dhamana.
Ikumbukwe kuwa Elizabeth Michael anakabiliwa na kosa la kumuua mwigizaji mwenzake Kanumba bila kukusudia tukio lililotokea mnamo 07/04/2012

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...