Monday, January 28, 2013

LULU ARUDISHWA RUMANDE


Lulu akiwa na mwigizaji mwenzake Ray kabla ya kwenda mahabusu.

Katika hali isiyo ya kwawaida mwigizaji Elizabert Michael a.k.a Lulu amerudishwa rumande baada ya taratibu za dhamana kutokamilika. 
Lulu akipanda gari kurudishwa rumande
Lulu akitoka mahakamani

Kwa mujibu wa mhabarishaji aliyekuwa mahakamani hapo amesema Lulu amerudi rumande leo kutokana na kwamba  watumishi wawili wa Mahakama ambao wanahusika na sehemu ya dhamana hiyo kwa upande wa sahihi za kimahakama, hawakuwepo Mahakamani hapo,hivyo dhamana yake inaweza kuwezekana keho.
Awali,Mahakama Kuu ya Tanzania iliweka wazi masharti ya dhamana ya msanii 
  huyo ambayo ilikuwa ni pamoja na:
  • Kuwasilisha au kukabidhi hati yake ya kusafiria(passport)
  • Kutosafiri nje ya Dar es salaam.
  • Kuripoti mahakamani kila siku ya kwanza ya kila mwezi
  • Kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja atamdhamini kwa shilingi milioni 20 za kitanzania.

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...