Wednesday, January 30, 2013

UKAME MKALI WAIKUMBA MOROGORO

Bwawa la Mindu likiwa limekauka kwa ukame

Hali ya mji wa Morogoro inazidi kuwa mbaya baada ya kutonyesha mvua kwa muda mrefu.Ukame huu umepelekea maji katika bwawa la maji la Mindu kukauka na kupungua kina cha maji kwa meta 2 (2m)
Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Mjisafi na Usafi wa mazingira Morogoro wamefanya ziara ya kutembelea vyanzo vya maji na kujionea upungufu wa maji .
Wajumbe wa Balaza la Wakurugenzi wa MORUWASA pamoja na watendaji wakiwa wanaangalia jinsi bwawa lilivyokauka.

Katika kujumuisha ziara hiyo,Mwenyekiti wa Bodi hiyo ya Wakurugenzi MORUWASA Bibi Dynes Senyagwa amewasihi wananchi wote pamoja na wanasiasa kushirikiana katika suala zima la utunzaji wa mazingira.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa MORUWASA Bibi Dynes Senyagwa

Kwa upande wake Mkurugenzi wa MORUWASA Ndg.John K.Mtaita amesema suala hili la uharibifu wa Mazingira linasababisha "mgao wa maji ndani ya mgao" kutokana na upungufu huo wa maji.
Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA Ndg.John K.Mtaita







No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...