Wednesday, March 27, 2013

CHADEMA WAZIDI KUWAKOMALIA USALAMA WA TAIFA


 Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa ameanza kuisakama Idara ya Usalama wa Taifa kuwa wanatumia mbinu mbalimbali kuwahujumu na kwamba mbinu zinazofanywa na idara hiyo ni kueneza propaganda walizodai za uongo dhidi yao.

Akizungumza jana makao makuu cha chama hicho jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alisema: “Tumezibaini mbinu zinazofanywa na Usalama wa Taifa kwa kutumiwa na CCM kueneza propaganda za uongo dhidi yao kwa lengo la kukichafua chama, lakini haziwezi kufanikiwa kwani tayari tumegundua mbinu zao.”

“Chadema ni chama makini na hakiwezi kuyumbishwa na mtu yoyote wala idara yoyote inayotumiwa na baadhi ya watu ili kutaka kukizohofisha,” alisema Dk Slaa ambaye mara kwa mara amekuwa akilalamika kuchezewa rafu.

Hata hivyo, viongozi wanaohusika na idara hiyo akiwamo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika walipotafutwa na gazeti hili kwa nyakati tofauti ili kuzungumzia tuhuma hizo za Dk Slaa, hawakuwa tayari kuzizungumzia.

Waziri Mkuchika alisema asingeweza kuzungumzia tuhuma hizi kwa kuwa hakuwa amezisikia wala hafahamu ni ujumbe upi uliomo katika kauli ya Dk Slaa.

“Mimi nimeshinda kwenye Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala tangu asubuhi na sasa ndiyo natoka, kwa hiyo sijasikia hiyo kauli wala huo mkutano wa (Dk Slaa). Kwa hiyo siwezi kujibu chochote kwa sasa,” alisema Mkuchika na kuongeza:

“Nadhani tumeelewana na pengine tusubiri pindi nitakapofahamu ni kipi amekizungumza na nikafanyia uchunguzi tutaona kama kuna cha kujibu basi tutajibu wakati huo, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote.”

Mapema gazeti hili lilimtafuta Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Rashid Othman ili kuzungumzia madai hayo ya Chadema lakini mara zote simu yake ilikuwa haipatikani.

Baadaye Mwananchi iliwasiliana na Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Jacky Nzoka ambaye alijibu kwa kifupi na kukata simu: “Mimi siyo msemaji tafadhali.”

Hata hivyo, katika tuhuma hizo Dk Slaa alisema mifano hai ipo kwake kwani kila wakati amekuwa akizungukwa na watu wa idara hiyo kwa malengo yao binafsi, lakini malengo yao hayawezi kufanikiwa kwani wao wapo makini katika hilo.

“Mimi kila wakati Usalama wa Taifa wamekuwa wakinizunguka zunguka kwa mambo yao binafsi wanayoyafuatilia kwangu, lakini nataka niwaambie kwamba nimewagundua na mbinu zao haziwezi kufanikiwa ila nawataka wasichoke kunifutalia na waendelee tu,” alisema.

Chadema na Sh400 milioni
Dk Slaa alikiwakilisha Chadema kusaini mkataba wa ushirikiano na Chama cha Konservative cha Denmark ili kuinua uwezo wa vijana na wanawake kisiasa.

Chama hicho kimeahidiwa kupewa Sh400 milioni kwa ajili ya kutoa mafunzo ya kujiimarisha kisiasa kwa Baraza la Vijana la chama hicho (Bavicha) na lile la Wanawake (Bawacha).

“Sisi leo tunasaini mkataba huu, lakini hatuufanyi siri kama vyama vingine vinavyofanya kwani mkataba huu upo wazi na kwamba kila mtu atakayetaka kuona atapewa,” alisema.

Alisema mafunzo hayo yatatolewa kwa watu 900 wa Bavicha na 900 wengine kutoka Bawacha na yanatarajia kuanza siku chache zijazo hadi Desemba mwaka huu yakiwa na lengo la kuwajengea uwezo wa kisiasa vijana wa Chadema na wanawake ili kuhakikisha wanaimarika kisiasa Tanzania,” alisema Dk Slaa.

Akizunguza wakati wa kusaini mkataba huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kimataifa ya Chama cha Conservative, Rolf Aagaard-Svendsen alisema lengo la ushirikino wao ni kuwajengea uwezo wa kisiasa vijana ili washiriki vizuri katika medani za kisiasa.

Habari hii ni kwa hisani ya Mwananchi,Jumatano,Machi 27,2013.

Tuesday, March 26, 2013

JOB VACANCY MANAGING DIRECTOR - DUWASA



 
DODOMA URBAN WATER SUPPLY AND SANITATION AUTHORITY
(DUWASA)           

TEL:  026 – 2324245              Website: www.duwasa.or.tz                                  P.O. BOX 431

FAX:  026 - 2320060                            E-mail:duwasatz@yahoo.com                                                      DODOMA     
 
JOB OPPORTUNITY FOR MANAGING DIRECTOR
Dodoma Urban Water Supply and Sanitation Authority (DUWASA) was established under section 3(I) of Cap. 272 of 1997 as repealed by section 60 of Water Supply and Sanitation Act No. 12 of 2009. DUWASA is an autonomous entity charged with the overall operations and management of water supply and sewerage disposal services in Dodoma Urban of the Municipality. The authority seeks to employ the services of a competent Managing Director to be stationed in Dodoma.

Applications are invited from suitably qualified, dynamic, experienced and performance driven Tanzanians male and female, to fill in the above mentioned vacancy.

1.0 Purpose of the Job
This job is a managerial position in which the holder is required to oversee all operations and systems of the authority and ensure they are in conformity with internal manuals and external guidelines such as Memorandum of understanding - MoU with the Ministry of Water and EWURA; performance Agreement targets, WHO and TBS Water and Waste water Standards and ISO 9001 Quality Management System requirements.

2.0 Main Duties and Responsibilities
Managing Director is the Chief Executive Officer responsible for managing, planning and coordinating Authorities’ activities. Among others he/she will be responsible for;
1.          Ensuring effective overall management and supervision of the Authority’s activities.
2.          Directing the formulation of policy proposals for consideration by the Board in relation to     physical and financial functions of the Authority.
3.       Interpreting policies laid down by the Board and ensure internal regulations and procedural instructions thereof.
4.        Implement and Monitor decisions and directives of the Board of Directors and duly report on the implementation.
5.       Prepare and submit to the Board, Authority’s annual plans,  budgets and priorities for approval.
6.       Be responsible for the implementation of the Performance Agreement as signed between the Board of Directors, Ministry of Water and EWURA; and ensuring that the Authority meets yearly goals, objectives and targets as stipulated in the agreements.
7.       Establishing and maintaining collaboration and link with key stakeholders such as the Ministry responsible for Water, EWURA, Regional Authorities, Media and Development partners to promote sustainable water and sewerage services as well as water projects investments and development of the Authority.
8.       Manage and control the Authority's financial and other resources in an efficient and cost effective manner in consultation with Board, EWURA and the parent Ministry.
9.       To oversee the organization's human resources and ensure that appropriate management structures and policies are developed and properly implemented.
10.   Reviews regularly, actual performance against plans and budgets and submits reports to the Board detailing performance with recommendations for actions necessary to correct adverse variance.
11.   Makes recommendations to the Boards for staffing level required by the Authority and ensures that effective procedures are established for recruitment, training and development of staff at all levels.
12.   Acting as the final authority for management decisions within the Authority, safeguards the Authority’s financial position and ensures that it discharges its financial obligations.
13.   Ensures that the Authority prepares and carries out an effective programme of public relations, water conservation & water protection and pricing policies.
14.   Ensuring that the Authority’s activities conform to the law, rules and regulations.
15.   Overseeing the planning and execution of new water & sewerage projects.
16.   Making recommendations to the Board for fixing water and sewerage tariffs and collect revenue thereof.
17.   Ensuring all Authority’s financial transactions are authorized and controlled in accordance with agreed procedures and the proper system of internal controls are maintained.
18.   Carrying out the functions of the Authority with due diligence
19.   Performing any other duties as may be assigned by the Board of Directors, Parent Ministry and Energy and Water Utilities Regulatory Authority (EWURA).

3.0 Minimum job requirements
3.1 Qualifications
v      The applicant must be a Tanzanian, with a Masters Degree from a recognized University in the fields of; Engineering, Water Resource Management, Economics, Finance, Commerce or Business Administration.  Management experience in water sector and administration is an added advantage.



3.2 Working experience
v      Possess at least 5 years experience in water supply and sanitation in a reputable organization of which 3 years should be in a senior position.

3.3 Key Competencies
v      He / She must have good inter-personal communication, computer skills and team work spirit
v      Must have demonstrated good leadership qualities and good financial management skills.
v      Must have ability to handle diverse human resource with prudence.
v      Must possess high levels of Initiative, Integrity, Enthusiasm, Accountability and Creativity.

3.4 Age limit
v      The applicant should be within the age between 35 and 50 years.

4.0 Terms of Employment
According to the Water Supply and Sanitation Act of 2009 section 17 sub-section 1, terms of employment will be 3 years renewable basing on the work performance.

5.0 Remunerations
This post attracts a salary at DOWA 14-15 scale and other fringe benefits of housing, transport, residential security, electricity and health insurance – depending on qualifications of the candidate.

6.0 Mode of Application
Applications are invited from candidates who meet the above mentioned requirements. Both electronic and hard copies are acceptable, attached with curriculum vitae, certified copies of academic transcripts and certificates, Names of 3 professional referees enclosing their recommendation letters and recent passport size photos. Hard copy applications can be posted or hand – delivered at the Authority’s offices. Applicants should clearly indicate their telephone numbers and email addresses for feedback. Applications should reach the undersigned not later than 4th April 2013 at 4.00 pm. Only short listed candidates will be contacted.

Applications should be marked “Application for the post of MD” on the envelope and addressed to;

Board Chairperson,
Dodoma Urban Water Supply and Sanitation Authority,
P.O. Box 431,
DODOMA.


Email Address: duwasatz@yahoo.com 

WANANCHI WA KIBAHA WALIGOMEA GARI LA HALMASHAURI LISIMWAGE TAKA

Wakazi wa Kibaha kwa Mfipa wakilisimamia gari lisimwage taka.
Wakazi wa Kibaha kwa Mfipa waliligomea gari la Halmashauri ya Mji Kibaha lenye nambari za usajili SM 3231 lisimwage taka katika eneo lao kutokana na kuwa taka hizo zinamwagwa juu ya calvat na zinasababisha kuzibisha calvat hilo na kufanya maji yajae kwenye makazi ya watu.
Gari la H/Mji lililozuiliwa kumwaga taka na wakazi wa Kibaha kwa Mfipa.
 Wakazi hao wamefikia hatua hiyo baada ya gari hilo kushindwa kwenda machimbo eneo ndiko yanakomwaga taka hizo baada ya barabara ya kwenda huko kujazwa vifusi na kusababisha magari yasiweze kupita.
Calvat la maji ya mvua
 Uchunguzi wa blogu hii umebaini kuwa maji katika calvat yanasafiri kwa taabu sana baada ya taka ngumu kujaa katika mkondo wa maji.

Monday, March 25, 2013

GARI LAFUNGA BARABARA YA DAR - MORO KWA MASAA KADHAA RUVU BAGAMOYO

Askari polisi wakisimamia usalama
Gari roli lenye namba za usajiri T451ARW liligongana na roli lenye namba za usajiri T475BNA eneo la Ruvu Wilaya ya Bagamoyo na kusababisha foleni kwa magari yanayotoka chalinze kwenda Dar na kutoka dar kwenda Chalinze.Foleni hiyo ilidumu kwa takribani muda usiopungua masaa matatu.
Foleni baada ya gari kuziba barabara
Kivutio zaidi ni pale vijana wapao 7 waliokuwa wakipakiza chokaa huku wakiwa hawana hata mask za kuzuia vumbi lisiwadhuru.
Vijana wakipakia chokaa




MAN UNITED YAFANIKIWA KUMSAINISHA BEKI WA KATI EZEQUIEL GARAY KUTOKA BENFICA.

Timu ya Manchester United imwfanikiwa kumsainisha Ezequiel Garay kutoka Benfica kwa kitita cha Paundi Mil.17.Man U na Benfica zimekubaliana kuwa Garay atahamia Old Traford majuma machache yajayo ili aweze kuichezea timu hiyo wakati wa kiangazi.

Garay mwenye umri wa miaka 26 aliyezaliwa Bosario tarehe 10.10.1986 amekuwa akizungumziwa mara kwa mara kuwa anawaniwa na Mashetani wekundu.

Thursday, March 21, 2013

KIKAO CHA KAMATI YA MAZINGIRA CHAFANYIKA CHINI YA NAIBU SPIKA UBELGIJI

Mheshimiwa Naibu Spika akiwasilisha taarifa kwenye kikao kinachoendelea Ubelgiji.
 Naibu spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Jobu Ndugai ameongoza kikao cha kamati ya mazingira na masuala ya jamii ya Mabunge ya Afrika, Carribian na Pacific (ACP) kinachoendelea kufanyika huko Brussels Ubelgiji.
Katika taarifa yake Mh.Ndugai amezungumzia ongezeko kubwa la watu Duniani pamoja na ukosefu wa rasilimali za kuwahudumia.
Picha na Said Yakub

WACHIMBA MADINI NA WAVUVI HARAMU WASABABISHA MAPIGANO MOROGORO

Mkuu wa kituo cha polisi cha kati Morogoro ,Mkuu wa Upelelezi Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa MORUWASA wakiwa eneo la tukio bwawani Mindu
 Katika hali isiyokuwa ya kawaida wavuvi na wachimba madini haramu katika bwawa la Mindu walizua tafrani jana jioni baada ya wachimba madini watatu Andrea Michael, Juma Hassani na Yusuph Abdallah kukamatwa na Maaskari wa kampuni ya Mputa Security wanaolinda bwawa hilo.
Wachimba madini haramu waliokamatwa Mindu kutoka kulia Yusuph Abdallah,Juma Hassan na Andrea Michael
 Askari mmoja alipigwa na wavuvi baada ya kwenda kuwaondoa katika eneo lisiloruhusiwa kuvuliwa samaki, katika kujitetea wavuvi hao waliwapigia simu wenzao ambao walikuja na mapikipiki yapatayo 6 na kila pikipiki ikipakiza watu watatu watatu.
 Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA ilimbidi aende polisi kuchukua maaskari ili kuweza kuimarisha usalama katika bwawa hilo na wakati maaskari wanafika eneo la tukio wavamizi hao walikuwa wameshakimbia lakini walifanikiwa kupata mchimba madini mmoja aitwaye Juma Hassani na kwendanaye kituoni.
Awali Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA Ndg.John K.Mtaita akiongelea swala la kuzima mitambo ya maji na kusababisha mji karibu mzima kukosa maji alisema wamefikia hatua hiyo baada ya maji yaliyokuwa yakiingia kituo cha kutibia maji kuwa machafu sana na yananuka kutokana na mvua kuingiza maji machafu bwawani Mindu.
Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA akiongea na Chief Kingalu katika eneo la Mindu.

Waandishi wa habari wakiwahoji wachimba madini haramu waliokamatwa bwawani Mindu.


Wednesday, March 20, 2013

MVUA ZASABABISHA MITAMBO YA KUSAFISHA NA KUTIBIA MAJI KUZIMWA MOROGORO

Maji yakiwa yanamwagwa eneo la kutibia maji Mafiga.
 Mvua zinazoendelea kunyesha zimesababisha wataalam katika kituo cha kutibu na kusafisha maji Mfiga iliyochini ya Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Morogoro (MORUWASA) kuzima mitambo na kumwaga maji yaliyokuwa yanaingia mitamboni hapo kutoka katika bwawa la Mindu kutokana na maji hayo kuwa machafu sana kwa kujaa tope.
Sampuli ya maji yaliyokuwa yanatoka bwawa la Mindu na kuja sehemu ya kutibia maji Mafiga.
 Hali hii ilizidi zaidi kutokana na mvua iliyonyesha jana jioni hadi usiku iliyoingiza tope jingi sana kwenye mdomo wa bomba la kuchukulia maji katika bwawa la Mindu.Hata hivyo wataalamu hao wamesema watawasha mitambo tu mara hali ya maji itakaporejea katika hali yake ya kawaida.
Kuzimwa kwa mitambo hiyo kumeathiri wakazi wa Maorogoro wanaotegemea chanzo cha Mindu kukosa maji ambao ni zaidi ya 70%.
Bi.Getrude Salema Afisa Uhusiano wa MORUWASA.
 Akiongea na Blogu hii Afisa Uhusiano wa MORUWASA Bi. Getrude Salema amesema hali hii ni changamoto kwa MORUWASA. Hata hivyo amewasihi wakazi wa Morogoro kuwa wawe wavumilivu na kuwa maji yatakayowafikia yatakuwa salama pale tu watakapokuwa wamewasha hiyo mitambo na kuruhusu maji yaanze kuingia na kutibiwa.
Mkondo wa maji ya mvua unaongiza tope bwawa la Mindu.
Blogu hii imefanya ziara hadi Mitambo ya kutibia maji Mafiga, Bwawa la Mindu na Sehemu ambako maji ya mvua yanavuka barabara ya Iringa na kuingia bwawa la Mindu.Kilichoonekana ni uchimbaji wa madini karibu na bwawa,mifugo kutifua ardhi pamoja na kilimo ndo sababu zilizochangia tope kuwa jingi.
Maji ya mvua yakiwa yametuama kando kando ya barabara ya Iringa eneo la Mindu
Hata hivyo,kando kando ya barabara ya Iringa kumeonekana madimbwi mengi ya maji yakiwa yametuama kutokana na makaravati yanayopitisha maji ya mvua kuziba kiasi cha kusababisha maji kukaa kwa muda mrefu na mvua zinaponyesha zinasomba hayo maji hadi bwawa la Mindu.

Wafanyakazi wa MORUWASA wakiwa wameenda kujionea halihalisi ya mikondo inayoingiza maji ya  mvua bwawani.

SAMAKI WA MAJITAKA WAHISIWA KUUZWA KWA WATU MJINI MOROGORO


Katika hali ya kushangaza na kusikitisha, nikwamba vijana wenyeji wa Manispaa ya Morogoro wamekutwa wakikusanya samaki aina ya kambale katika mabwawa ya majitaka yanayotolewa tope ya Mafisa.
 Walipoulizwa wakasema wanaenda kula lakini uwalakini unakuja pale walipoonekana kukazana kukusanya samaki wengi na kwenda kuwasafisha.
 Wito wangu kwa wakazi wa Morogoro kuweni makini na samaki wanaouziwa na watu mitaani na kwa wale wenye mabucha kuweni waaminifu kwa kutonunua samaki watakao letwa kwao na vijana wa mtaani.
Na maafisa afya kuweni makini kwa kukagua samaki wanaouzwa kwenye mabucha na mitaani.

Monday, March 18, 2013

WAZIRI MKUU PINDA AONGOZA HARAMBEE MAGOMENI



WAZIRI MKUU Ndg.Mizengo Pinda ameongoza harambee ya papo kwa papo na kufanikiwa kukusanya sh. milioni 31.5 zikiwa ni ahadi na fedha taslimu kwa ajili ya ukarabati wa Kanisa Katoliki la Mashahidi wa Uganda la Magomeni, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waumini wa Kanisa hilo Jumapili asubuhi, Machi 17, 2013 kabla ya kuendesha harambee hiyo, Waziri Mkuu aliusifu uongozi wa Kanisa Katoliki la Magomeni kwa kuamua kufanya upanuzi wa kanisa hilo ili liweze kuhudumia waumini wengi zaidi.
“Nia yao ni nzuri sana na wameona mbali mapema. Magomeni hii ya leo si ya wakati ule, na wala haitakuwa hivi katika miaka mingine 50 ijayo. Zamani usingeweza kuona hata ghorofa moja hapa Magomeni lakini sasa hivi maghorofa hayahesabiki,” alisema.
Aliwasisitiza waumini hao kujitoa kwa ajili ya kazi ya Bwana kwa sababu hakuna sadaka ambayo ni ndogo. “Hakuna sadaka iliyo ndogo mbele ya Mungu, kikubwa ni dhamira tu. Kanisa ni letu na litajengwa na sisi waumini ili mradi kila mmoja wetu aseme Kansa hili nitalijenga,” alisisitiza.
Mapema akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na waumini hao, Baba Paroko wa kanisa hilo, Padri Sixfrious Rwechungura alisema wameanza kazi ya ukarabati tangu Agosti 15, 2011 na kwamba hadi sasa wamekwishakusanya sh. milioni 350 iliyotokana na nguvu za waumini wenyewe bila msaada wa kutoka nje.
Alisema wanahitaji kiasi cha sh. milioni 300 ili kukamilisha kazi hiyo ambayo inapaswa kukamilika katika miaka miwili ijayo ili iendane na maadhimisho ya miaka 50 ya kanisa hilo.
Katika harambee hiyo, Waziri Mkuu na mkewe Mama Tunu Pinda waliahidi kuchangia sh. Milioni 10 na kutoa sh. Milioni mbili za kianzio. Pia aliendesha mnada wa mbuzi aliyenunuliwa kwa sh. 600,000/- na mkoba ulionunuliwa kwa sh. 150,000/-.
(mwisho)

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...