Wednesday, November 14, 2012

KINANA AUKWAA UKATIBU MKUU CCM

 KINANA AUKWAA UKATIBU MKUU CCM
 Mkutano mkuu wa 8 wa Chama Cha Mapinduzi NEC mjini Dodoma, ambao ndo uko ukingoni umempitisha Abdulhaman Kinana kuwa katibu mkuu wa chama  tawala.


Pia mkutano huo umemchagua kwa 100% Katibu Mkuu wa zamani, Philip Mangula, kuwa Makamu Mwenyekiti, akirithi mikoba ya Pius Msekwa.

Naye Mwigulu Nchemba amechaguliwa kuwa naibu katibu mkuu wa chama hicho upande wa bara na Vuai Ali Vuai upande wa Zanzibar.

Wengine waliofanikiwa kupita kwenye secretarieti ya chama hicho ni pamoja na Asha Rose Migiro ambaye amechaguliwa kushughulikia masuala ya kimataifa na Zakhia Meghji amechaguliwa kushika nafasi ya uweka hazina.

Nape Nnauye ameendelea kushikilia nafasi yake katibu na uenezi wa chama hicho.

HALI YA VITUO VYA AFYA MOROGORO





HALI YA VITUO VYA AFYA MOROGORO
Sabasaba ni kituo cha afya kilichofunguliwa 2.11.1973 na waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndg.Rasid M.Kawawa.Kituo hiki pia kina kambi ya kuhudumia waathirika wa ugonjwa wa mlipuko wa kipindu pindu ambao wanakuwa wanalazwa kwenye mahema yanayoonekana kwenye picha.
Swali langu ni je, leo kukitokea mlipuko wa kipindu pindu wagonjwa watalazwa kwenye mahema haya haya au kuna ujanja mwingine utafanyika?Nauliza hivyo kwasababu mahema yenyewe yana hali mbaya sana na hayako katika hali nzuri.

UKUAJI WA TEKNOLOJIA





UKUAJI WA TEKNOLOJIA
Ndg.wanamichezo,wabunifu wameweza kuwatolea simu ambazo zinaendana kimichezo.Hii ni simu ambayo inaumbile la mpira lakini inashika mtandao vizuri sana na ni rahisi kubebeka,ina nafasi ya kuweka line mbili.Yeyote atakayeihitaji tuwasiliane.

Tuesday, November 13, 2012

UBUNIFU.COM


Huu ni ubunifu uliopatikana mji kasoro bahari Morogoro,huyu kabadirisha piki pikiya tairi 2 na kuifanya daladala kwa kuiongezea kikapu nyuma na kuifunga turubai ili abiria wasiweze kunyeshewa mvua wala kupigwa jua.
Watanzania tunatakiwa kuendeleza vipaji tulivyikuwa navyo ili tuweze kuendelea.

Thursday, November 8, 2012

3R ENVIRONMENTAL MANAGEMENT.

3R ENVIRONMENTAL MANAGEMENT.
katika kuhakikisha kuwa mazingira yetu yanakuwa safi na salama na kupunguza milipuko ya magonjwa tunatakiwa tutumie" 3R principal" Maana yake ni Reduce,Reuse na Recycle.
Njia hii ikitumika tutajikuta mazingira yetu yanakuwa yakuvutia.Hii inazihirishwa na kama wakazi wa Manispaa ya Morogoro Msamvu walivyokutwa wamekusanya taka ngumu na kuzifungasha vizuri zikisubiri usafiri zisafirishwe kwenda kiwandani.

Tuesday, November 6, 2012

Y2K SOUND - WAZEE WA KUWAPOTEZA.

Y2K SOUND - WAZEE WA KUWAPOTEZA.
Kwa mahitaji ya muziki katika shughuri mbali mbali ikiwa ni pamoja na harusi,send off,kitchen party,graduations,tafrija,shughuri za kidini, kisiasa n.wasiliana ya Y2K SOUND MOROGORO watakuhudumia.
Mawasiliano: 0755674418/0714628954

USAFI WA MAZINGIRA MOROGORO.

USAFI WA MAZINGIRA MOROGORO.
Katika kuhakikisha kuwa mji wa Morogoro unakuwa safi Manispaa ya Morogoro inamiliki magari ya kunyonyea majitaka mawili na magari ya watu binafsi yako zaidi ya manne.
Magari haya hutumika kuwanyonyea wakazi wa Morogoro majitaka yakiwa yamejaa kwenye soak away pits.Majitaka hayo yakishanyonywa hutupwa katika mabwawa ya majitaka yaliyoko Mafisa yanayomilikiwa na MORUWASA ili kusiwepo na uchafuzi wa mazingira.
HATARI! HATARI! HATARI!
Hii ni hatari kwa wakazi wa Manispaa ya Morogoro wanaonunua maji kutoka kwenye magari yanayouza maji mitaani.Magari haya badala ya kununua maji katika vioski vya kuuzia maji vilivyo mjini yanaenda eneo la Mindu darajani na kuchota maji yasiyo tibiwa na kwenda kuwauzia wananchi.
Kibaya zaidi nikwamba magari hayo yameandikwa majisafi hivyo wananchi wanayaamini kumbe mambo ni tofauti.
Kulikuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi kuwa MORUWASA inasambaza maji yasiyosafi na salama baada ya kutumia maji kutoka kwenye magari hayo yanayowadanganya watu kuwa wamenunua maji kutoka MORUWASA.Mojawapo ni gari T 706 AAF lililoandikwa majisafi,naomba wahusika wafatilie suala hili kwa karibu ili kunusuru afya za wananchi.
KUPASUKA BOMBA.
Bomba kubwa linalotoa maji bwawa la Mindu kupeleka sehemu ya kutibia maji Mafiga lenye kipenyo cha inchi 24 (24") sawa na milimeta 600 (600mm) limepasuka sehemu mbili tofauti.Bomba hili ndo linalosambaza maji mjini Morogoro zaidi ya asilimia 75.
Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira inaendelea na juhudi za kulitengeneza bomba hilo kama inavyoonekana kwenye picha ili huduma ya maji ilejee haraka iwezekanavyo.
Matengenezo hayo yanatarajiwa kukamilika kabla ya yaa 12 jioni.
UZEMBE KAZINI.
Hapa ni mchezo wa makida unachezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro katika suala zima la utupaji wa taka ngumu.Jambo la kusikitisha nikwamba magari yanamwaga taka hadi barabarani baada ya kujizibia barabara ya kuingia dampo.
Swali langu ni,je,muhusika wa taka ngumu huwa anatembelea dampo hili? Na kama anatembelea ni  hatua gani kazichukua katika kutatua tatizo hili?
Jambo jingine la kusikitisha nikwamba magari haya ya takangumu yameanza kumwaga taka hizo nje ya uzio kwa uzunguka uzio huo na kuzichoma moto nje ya dampo.
Jamani,tujali afya za wananchi popote tulipo na tujenge utamaduni wa uhifadhi na utunzaji wa mazingira.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...