Friday, March 8, 2013

SIKU YA WANAWAKE YAFANA MOROGORO

Baadhi ya wanawake wa MORUWASA na Ofisi Za Bonde la Wami /Ruvu wakiwa tayari kuelekea kwenye maandamano.
Katika kusherehekea siku ya wanawake Duniani,mwandishi wa blogu hii amepita sehemu mbali mbali za mji wa Morogoro na kuwakuta wanawake wakiwa na furaha isiyokuwa na kifani.

Sehemu mojawapo ni katika ofisi za serikali MORUWASA na Ofisi za Bonde la Wami/Ruvu ambapo baadhi ya wanawake wa Ofisi hizo wamekutwa wakijiandaa kuelekea kwenye maandamano.

UHAMASISHAJI JUU UTUNZAJI WA RASILIMALI MAJI BONDE LA WAMI/RUVU

Afisa Maendeleo ya Jamii Bonde la Wami/Ruvu Bi.Nickbar Mwanana Ally akitoa mada wakati wa uelimishaji juu ya zana shirikishi katika usimamizi wa pamoja wa rasilimali maji katika Shule ya Msingi Kisemu-Mtamba Morogoro vijijini.
Katika kuhakikisha rasilimali maji inakuwa endelevu,Bonde la Wami/Ruvu linafanya jitihada za kuwahamasisha na kuwaelimisha wanchi wa Mikoa ya Dodoma,Morogoro,Pwani,Tanga na Dar es salaam juu ya utunzaji wa rasilimali hiyo.
Wakazi wa Morogoro vijijini kutoka vijiji 13 wakishiriki mafunzo katika shule ya msingi Kisemu-Mtamba

Ofisi ya Bonde la Wami/Ruvu inaendesha mpango wa ZANA SHIRIKISHI KATIKA USIMAMIZI WA PAMOJA WA RASILIMALI MAJI.Mpango huu unaendeshwa katika vijiji vyote na wananchi wanahamasishwa kushiriki katika shughuli za utunzaji vyanzo vya maji.
Miti jamii ya Misederea ambayo wakazi wengi wa Morogoro vijijini na Mvomero wameipanda kwa wingi karibu na vyanzo vya maji bila kuelimishwa wapi mahali bora pakupanda.Ukweli nikwamba miti hii ni hatari kuipanda karibu na vyanzo vya maji maana inanyonya maji kwa kasi sana.
Maofisa wa ofisi za Bonde la Wami/Ruvu wakichota maji katika moja ya chanzo cha maji Morogoro vijijini.Vyanzo vya maji vikitunza vizuri ni hazina ya sasa na kwa kizazi kijacho.

Wednesday, March 6, 2013

TFF YASALIMU AMRI KWA SERIKALI JUU YA KATIBA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewasilisha rasmi maombi ya kuonana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara ili kuzungumzia uamuzi wake wa kutengua usajili wa Katiba ya 2012.
Maombi hayo yaliwasilishwa rasmi Wizarani Machi 4 mwaka huu ambapo TFF imependekeza kikao hicho kifanyike Machi 7 mwaka huu) au Machi 13 mwaka huu.
Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Machi 2 mwaka huu kujadili tamko ya Waziri kutengua matumizi ya Katiba ya 2012 ndiyo iliyopendekeza kikao hicho kwa lengo la kusikiliza upande wa TFF katika suala hilo.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

WATAALAMU WA AFYA NCHINI SASA KUWASILIANA BURE

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika juhudi zake za kuboresha afya za wananchi imeanzisha mfumo mpya wa mawasilano kama taarifa ilivyotolewa kwenye vyombo vya habari.
 


Madaktari na wataalamu wengine wa afya kuanzia sasa wataanza kupata huduma ya kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi bila malipo yoyote kwa wataalamu wenzao popote nchini na kupokea taarifa, maelekezo na ushauri unaohitajika kupitia mtandao wa mawasiliano ya simu za mkononi wa Vodacom pekee.


Health Network Programme hii imeanzishwa mahsusi kwa lengo la kurahisisha utendaji kazi wa madaktari na kuboresha kiwango cha mawasiliano ya wao kwa wao, na kwamba usajili wa mtandao huo kuanzia sasa unatarajia kuhusisha wataalamu wa afya wapatao 9,000 nchi nzima, wakiwemo madaktari, madaktari wa meno, madaktari wasaidizi, madaktari wasaidizi wa meno, tabibu na tabibu wasaidizi kukote waliko, serikalini na wale wa binafsi.

Aidha ili daktari aweze kujiunga kwenye programu hiyo atahitajika kutumia simu yake ambayo itakuwa na kadi ya simu (simcard) ya Vodacom na kisha kupiga *149*24# na baadaye kupata maelekezo ya namna ya kujisajili.

Mbali ya kupiga simu bure wanachama wa mtandao huo kwa kushiriki katika programu hiyo watakuwa na uwezo wa kutuma ujumbe mfupi ‘sms’ 50 bure kila mwezi kuwasiliana na wenzao waliojisajili ndani ya programu.

Mpango huo utakwenda mbali zaidi na kupanua wigo wa fursa kwa sekta hiyo katika kukabiliana na changamoto zake kwa haraka ili kukidhi matakwa ya Watanzania walio wengi.

Switchboard kwa utaratibu kama huu pia imefaulu kuwaunganisha karibu madaktari wote wa nchi za Ghana na Liberia, na kwamba zaidi ya simu milioni 4 zimepigwa kutoka mwaka 2008 hadi sasa ambapo madaktari wamekuwa wakisaidiana katika kuboresha huduma stahiki anazohitaji mgonjwa.

Kwa sasa madaktari karibu wote wa nchi hizo ni sehemu ya Mtandao wa Afya unaowawezesha kupata huduma za bure za mawasiliano sambamba na wao kwa wao kushirikiana na kusaidiana kitaalamu katika kila pembe ya nchi hizo kwa manufaa yao na wagonjwa.

Programu hiyo inadhaminiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Switchboard na Kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom.

Kwa wale watakaojisajili wanaombwa kutoa kibali kwa Timu ya Tafiti ya Mpango huu ya Switchboard yaani Programme Research Team (PRT) na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, kuweza kutathmini matumizi ya simu zao za mkononi ili kujua imeleta mabadilko kiasi gani katika sekta ya afya kupitia programu hiyo.

PRT na Vodacom hawatavujisha wala kujihusisha na taarifa zako zozote binafsi za mawasiliano kupitia simcard yako na kwamba kushiriki ni hiari yako, na unaweza kujitoa kwenye programu wakati wowote ukihitaji na hautatozwa wala kulipishwa gharama yoyote,”

Kupitia programu hiyo, Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imeiomba Switchboard kuratibu na kuweka mpangilio mzuri wa mchakato wote wa programu husika kwa manufaa ya wataalamu wa afya na ustawi wa tiba nchini.

UBORA WA MAJI WALETA KIZAAZAA MORO,MBUNGE AITEMBELEA MORUWASA KUJIONEA HALI HALISI.

Mbunge wa Morogoro Mjini Mh.Azizi Abood.
Wakazi wa Manispaa ya Morogoro jana walimvamia Mbunge wao Mh.Azizi Abood wakilalamikia ubora wa maji yaliyosambazwa mtaani kwao kuwa yalikuwa chini ya kiwango.Kutokana na malalamiko hayo ilimlazimu mbunge wa Morogoro Mjini kufanya ziara ya ghafla katika ofisi za Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira MORUWASA ili kujua kulikoni.
Gari la Mh.Mbunge alipowasili MORUWASA.
Akielezea sababu zilizopelekea kupungua ubora wa maji Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA Ndg.John K.Mtaita alisema hali hiyo ilitokana ukarabati wa sehemu ya kutibia maji Mafiga na usafishaji wa machujio ya maji.Hata hivyo,mkurugenzi huyo aliwaahidi wakazi wa Morogoro kuwa ubora wa maji utaimarika maradufu baada ya mradi wa ukarabati wa miundombinu utakapokamilika.
Mafundi wakiendelea na matengenezo ya bomba Msamvu stendi ya Dodoma.
 Hata hivyo,mbunge huyo aliweza kutembelea hata eneo la Msamvu ambapo bomba linatengenezwa ili wakazi wa Kihonda waweze kupunguziwa adha ya ukosefu wa maji.

Monday, March 4, 2013

MAKADINALI WA KANISA KATOLIKI WAKUTANA KUMCHAGUA PAPA

Baadhi ya Makadinali wanaoshiriki kikao hicho
Makadinali wa Kanisa Katoliki kutoka mataifa yote duniani wamekusanyika mjini Roma Italia kuanza mkutano wa awali wa faragha wa kumchagua mrithi wa Papa Benedict XVI.
Ikumbukwe kuwa siku chache kabla ya Papa Benedict XVI kujiuzulu alibadilisha katiba na kusema uchaguzi wa papa ufanyike siku chache baada ya Papa kufa au kujiuzulu.

MRADI WA USAFI WA MAZINGIRA NA AFYA MOROGORO



Mtafiti mkuu wa mradi Profesa Jamidu Katima akisaini kitabu cha wageni wakati wa utambulisho wa mradi.
Manispaa ya Morogoro imepata bahati ya kujengewa mradi wa uondoshaji wa majitaka na uhifadhi wa mazingira unaojengwa na Chuo kikuu cha Dar es salaam kitivo cha Uhandisi (COET) unaofadhiliwa na COSTECH ambao ni mradi wenye thamani ya zaidi ya Milioni 200 unaojengwa Mafisa katika mabwawa ya majitaka ya MORUWASA.

Bwawa litakalo kuwa linatumika kutibu majitaka.
Mradi huo ujulikanao kama Constructed wetlands and fish ponds.Katika mradi huo ambao malengo yake ni utafiti juu ya matumizi ya majitaka baada ya kutibiwa na kujenga mabwawa ambayo ni ya bei nafuu.
Bwawa la kufugia samaki katika mradi huu.
Katika mradi huo utahusisha ujenzi wa mabwawa ya samaki na kilimo cha umwagiliaji ili kuweza kuthibitisha kama majitaka hayo baada ya kutibiwa yanaweza kutumika kwa ufugaji wa samaki na umwagiliaji.

Utafiti juu ya kilimo gani kitafaa kulimia kutumia maji hayo,hapa ni Mpunga,nyanya na Chinese.
 Akiongelea juu ya baadhi ya faida za mradi huo ,mtafiti mkuu wa mradi huo profesa Jamidu Katima alisema kuwa ni gharama ndogo za ujenzi,hupunguza adha ya harufu mbaya,maji yake yanaweza kutumika katika kujikwamua kiuchumi.

NEEMA YA MAJI MOROGORO YAANZA KUONEKANA

Mafundi wakiwa kazini katika jitihada za kutengeneza bomba hilo.
 Ni kwa kipindi kisichopungua miezi mitatu sasa tangu bomba kubwa lenye kipenyo cha 16" sawa na 400mm lilipopasuka eneo la Msamvu maarufu kama Stendi ya Dodoma kwenye ukuta wa Tanesco tarehe 19.12.2012.
 
Kupasuka kwa bomba hili kulipelekea maeneo karibia yote ya Kihonda kukosa maji jambo ambalo lilipelekea hadi wakazi wa eneo hilo kufikia hatua ya kufunga barabara na kuzuia magari yasipite wiki mbili zilizopita.
 
Katika hali ya kutia moyo na kufurahisha,sasa bomba hilo limeanza kushughurikiwa na kutengenezwa baada ya kupatikana mitambo maalum ya kutoboa barabara kuu ya Dodoma.
 
Kukamilika kwa bomba hilo kutapunguza upungufu wa maji uliokuwa unawakumba wakazi wa maeneo ya Kihonda.
Mafundi na wataalam mbali mbali wakiwa wanapeana mawazo nini cha kufanya.

Friday, March 1, 2013

MSAKO MKALI WA UCHIMBAJI WA MADINI KANDO MWA BWAWA LA MINDU.

Ndg.Christopha Evarist Bengu aliyekamatwa akichimba madini kando mwa Bwawa la Mindu.

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa mazingira Morogoro (MORUWASA) inaendelea na zoezi la kuhifadhi mazingira katika vyanzo vyake vya maji kwa wakazi wa Morogoro.Katika kuhakikisha hilo leo Maaskari wanaolinda Bwawa la Mindu wameweza kuwakimbiza watu zaidi ya kumi (10) waliokuwa wanachimba madini lakini wakafanikiwa kumkamata mchimbaji mmoja.

Ndg.Christopha Evarist Bengu akiwa chini ya ulinzi
Akiongea na Blogu hii Mkurugenzi Mtendaji wa MORUWASA Ndg.John K.Mtaita amesema mtuhumiwa huyo aitwaye Ndg.Christopha Evaristi Bengu anapelekwa Polisi kwa kuweza kupelekwa Mahakamani.
Mkurugenzi mtendaji wa MORUWASA Ndg.John K.Mtaita.
Ikumbukwe kwamba wakazi wa Morogoro mpaka sasa wana uhaba mkubwa wa maji kutokana na ukame unaosababishwa na uchafuzi wa mazingira unaofanywa na wakazi wa Morogoro.

MKURUGENZI TAZARA AACHIA NGAZI

Aliyekuwa Mtendaji mkuu wa TAZARA Bw.Akashambatwa Mbikusite
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na zambia Bw. Akashambatwa Mbikusita-Lewanika ameachia ngazi baada ya kampeni zake za kuendelea kwa kipindi kingine cha miaka 3 kushindikana.
Inasemekana muda wa kuiongozwa TAZARA kwa Bw.Akashambatwa uliisha rasmi mwishoni mwa Januari 2013 lakini uliongezwa kutokana na ombi maalum la uongozi wa nchi ya Zambia.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...