Showing posts with label SIASA. Show all posts
Showing posts with label SIASA. Show all posts
Sunday, October 13, 2013
LEO NI LEO IGUNGA, ZITTO KABWE KUTAJA MSHARA WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.
Kama alivyoahidi Mbunge wa Kigoma Mashariki Mh.Zitto Zuberi Kabwe, leo anafanya mkutano na wakazi wa Wiraya ya Igunga na ameeleza kuwa miongoni wa mambo anayotarajia kuyaongelea leo ni pamoja na mshahara wa Rais na haya nai maneno yake mwenyewe:-
Friday, October 11, 2013
Speech by Dr Slaa at The University of Samford, USA .
Mr.
President, the faculty, staff, students, invited guests and
the public at large. Allow me to express my gratitude, for the cordial
welcome
at your lovely campus. It is one of a kind, and If I could, I would have
stayed
much longer to learn more on your success that I could take back to our
young
people. The environment and the surroundings are as beautiful as the
people
themselves. Along the way, I have met great people with great hearts,
and I
thank you for that
Likewise, receive greetings from the people of Tanzania. I was quite impressed with your level of research, and the homework you have done trying to know Tanzania, I was also particularly touched by some of you in the audience that knew the geography of my country; and even trying to challenge me . Mrs. Macquire, “People of Mto wa Mbu” are definitely proud of
you for being such a good Ambassador. We thank
you, and Tanzania needs more of you that will help in exposing it to the
people
of America
Likewise, receive greetings from the people of Tanzania. I was quite impressed with your level of research, and the homework you have done trying to know Tanzania, I was also particularly touched by some of you in the audience that knew the geography of my country; and even trying to challenge me . Mrs. Macquire, “People of Mto wa Mbu” are definitely
Thursday, October 10, 2013
Wednesday, October 9, 2013
NIA YA ZITO KABWE KUTAJA MSHAHARA WA RAIS NA MAKAMU WA RAIS, TAR. 13.10.2013 HUKO IGUNGA.
Mishahara ya Viongozi wa Umma lazima iwe wazi kwa umma.
Sheria za Mishahara ziweke wazi kabisa kuwa mishahara hii itakuwa wazi na itakatwa kodi. Juzi Mpanda nimewaambia wananchi Mshahara wa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa mwezi.
Nikiwa Igunga mnamo tarehe 13 Oktoba tutawaambia wananchi mshahara wa Rais na Makamu wa Rais.
Iwapo Rais wa marekani mshahara wake na mapato yake ni wazi na unakatwa kodi, iweje Rais wa nchi ndogo kama Tanzania. Wameifungia Mwananchi kwa kutaja viwango vya mishahara ya watumishi wa Umma. Wamfungie Mbunge kama wanaweza.
cHANZO: Zitto Kabwe Social Media.
Tuesday, October 8, 2013
Monday, September 30, 2013
NIA YA ZITTO KABWE JUU YA KUFANYA MAREKEBISHO YA SHERIA YA MAGAZETI.
Nimetoa taarifa rasmi kwa katibu wa Bunge kwa mujibu
wa kanuni za Bunge kwamba katika mkutano ujao wa Bunge nitawasilisha
muswada binafsi wa sheria kufanya marekebisho ya sheria ya magazeti kwa
lengo la kuifuta kabisa sheria hiyo.
Madhumuni ya muswada huo ni;
“kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 kwa sababu inakizana na
Katiba ya Nchi kuhusu haki za Raia kupata habari na kwamba iliorodheshwa
na tume ya Nyalali ni sheria kandamizi’
...
Muswada wenyewe nitauwalisilisha siku ya ijumaa ili uchapwe kwenye
gazeti la Serikali uweze kuingia kwenye shughuli za Bunge zitakazoanza
tarehe 15 Oktoba 2013 kwa ngazi ya kamati.
September 30, 2013
Source : Zitto social media.
Wednesday, September 11, 2013
Monday, September 9, 2013
Rais JK aonja nguvu ya CHADEMA Mwanza.
ISHARA YA VIDOLE
VIWILI, PEOPLES POWER VYATAWALA
RAIS Jakaya
Kikwete jana alipata wakati mgumu, baada ya kukutana na nguvu ya Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jijini Mwanza katika ziara yake,
huku Waziri wake wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, naye akijikuta akizomewa
mbele yake.
Mbunge wa
Nyamagana, Ezekia Wenje, alivunja mwiko baada ya kujiunga katika msafara
huo wa raia akiwa na gari lenye alama za Movement for Change (M4C)
lililokuwa limefungwa bendera mbili za CHADEMA.
Hata hivyo
maofisa usalama walipata wakati mgumu kulizuia gari hilo lisiwepo katika
msafara huo, jambo lililozua tafrani kidogo katika uwanja wa Furahisha
ambapo Kikwete alikuwa akihutubia mkutano wa hadhara.
Awali wakati
wa uzinduzi wa wodi ya wazazi iliyoko eneo la Butimba, Rais alilazimika
kumpa Wenje nafasi ya kuwasalimia wananchi baada ya Mkuu wa Mkoa,
Evarist Ndikilo, kutaka kufanya hila ya kumnyima haki hiyo kama mbunge
wa jimbo husika.
Baada ya
viongozi wote kutambulishwa bila Wenje kutajwa, wananchi walianza kupaza
sauti wakitaka mbunge wao naye atambulishwe.
Wenje baada ya
kusimama alimshukuru Rais Kikwete kwa kumpa nafasi hiyo lakini
akamwomba amvumilie kidogo atoe salamu maalumu ya wana Mwanza.
Kama kawaida
ya CHADEMA kwenye salamu yao, Wenje aliwaomba wananchi wakunje ngumi
kisha akawasalimu kwa kibwagizo cha peoples… nao wakamwitikia power!
Akiwa katika
viwanja vya Furahisha ambapo Rais Kikwete alichelewa kuanza mkutano
wake, Wenje alifika hapo na kushangiliwa kwa nguvu na wananchi huku
polisi wakiwazuia bila mafanikio.
Ilipofika saa
12 jioni kabla Rais hajaingia uwanjani, wananchi hao walimtaka Wenje
awahutubie huku wakidai bendera ya taifa ishushwe kwani muda wake
ulikuwa umefika.
Kikwete
aliingia uwanjani hapo saa 12:10 akiongozana na viongozi mbalimbali wa
chama na serikali lakini wananchi hawakuonyesha kumshangilia badala yake
walikuwa wakimwonyesha alama ya vidole viwili inayotumiwa na CHADEMA
wakiimba ‘peoples…power’.
Katika hatua
ya kushangaza wananchi hao walimshangilia kwa nguvu mbunge wa Ilemela,
Highness Kiwia, aliyekuwa ameongozana na Rais huku wakiwazomea Meya wa
Manispaa ya Ilemela, Henry Matata, ambaye hakufika kabisa mkutanoni
hapo.
Matata
alionekana mapema wakati Rais Kikwete akisomewa taarifa ya maendeleo
makao makuu ya wilaya hiyo lakini hakufika uwanjani kabisa katika viti
vya mbele alionekana naibu wake, Swila Dede.
Baadhi ya
wananchi hao walisikika wakisema chini kwa chini kuwa Matata ni mwizi
hawataki kumsikia lakini shangwe na nderemo zikajiri pale
walipotambulishwa Wenje na Kiwia.
Rais Kikwete
akiwa wilaya ya Ilemela, wananchi wengi waliokuwa wamesimama njiani
walimwonyesha vidole viwili ikiwa ni alama CHADEMA.
Hata hivyo,
hali hiyo ilionekana kumkera kiongozi huyo wa nchi pamoja na maofisa wa
usalama, ambapo wana usalama wakiwemo polisi walionekana wakiwatisha na
kuwazuia wananchi kunyoosha vidole viwili.
Magufuli
azomewa
Waziri wa
Ujenzi, Dk. Magufuli, alikumbana na jinamizi la kuzomewa mbele ya Rais
baada ya kusimama jukwaani na kutaja jina la Matata, ambapo wananchi
wengi walimzomea kwa miluzi huku wakimnyooshea vidole viwili.
Adha Magufuli
alizomewa pia aliposema wabunge wa Ilemela na Nyamagana jijini hapa ni
wana CHADEMA lakini ndani ya roho zao ni wana CCM.
Pia aliendelea
kuzomewa aliposema kuwa iwapo Rais angehitaji kupokea kadi za CHADEMA
zilizorudishwa angepokea nyingi.
“Mheshimiwa
Rais, nampongeza Meya Matata (akazomewa), lakini pia wabunge wa Ilemela
na Nyamagana wanachapa kazi vizuri, nje CHADEMA lakini ndani wao CCM
(akazomewa).”
Akizungumza
katika mkutano huo, Rais Kikwete alimpongeza mbunge wa Nyamagana kwa
uchapakazi mzuri hasa kusimamia sekta ya elimu na kwamba wabunge wa
namna hiyo wanastahili kuigwa.
Hata hivyo,
alisema serikali yake imejipanga vizuri kuhakikisha usafiri wa reli,
ndege, majini na barabara za lami vinaboreshwa maradufu kwa ajili ya
maendeleo ya wananchi.
“Serikali
yangu imeweka nguvu kubwa katika kuboresha sekta ya uchukuzi, ujenzi na
nyinginezo. Hii ni kutaka kuwaletea wananchi wetu maendeleo ya kisekta,”
alisema.
Baadhi ya
mawaziri walioongozana na Rais mbali na Magufuli ni Naibu Waziri, Ofisi
ya Makamu wa Rais, Charles Kitwanga, Waziri wa Kilimo, Chakula na
Ushirika, Christopher Chiza, Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe,
Naibu Waziri wa Ujenzi na Dk. Charles Tizeba.
Friday, September 6, 2013
HIVI NDIVYO MH.MBOWE ALIVYOONDOLEWA BUNGENI JANA.
Hatua hiyo ilitokana baada ya wabunge hao kupiga kura za kukubali au kukataa kuhusu kupitishwa kwa kujadili Mswaada wa Katiba uliopelekwa Bungeni hapo na Serikali ili kuweza kujadiliwa na bunge hilo.
Wabunge hao wa kambi ya upinzani wakiongozwa na Freeman Mbowe walipinga matokeo hayo na kuamua kusimama na wakati huo huo Spika Ndugai aliwataka kukaa chini ili kuendelea na kuchangia hoja za msingi za kujadili mswaada huo.
Ndugai aliwataka wabunge hao kukubaliana na matokeo yaliyotokea na kwa pamoja waweze kujadili mswaada huo ambao ni faida kwa taifa lakini mbali na ombi hilo kambi ya upinzani walikaidi ndipo Spika alitoa dakika tano kwa za kiongozi huyo kutoka ili bunge liendelee,ambapo hata hivyo kiongozi huyo alikaidi amri hiyo.
Baada ya mabishano hayo ndipo Spika alipotumia kiti chake na kuwataka askari wamtoe kwa nguvu nje ya ukumbi wa bunge, amri ambayo ilizua taflani na hekeheka kupelekea wabunge wa kambi ya wapinzani kuungana na kuwatunishia misuri askari hao wakimkingia kiongozi huyo kutolewa nje.
Tukio hilo lililochukua dakika zaidi ya 30 lilipelekea Bw. Job Ndugai kuwatolea macho askari hao akiwaamuru kutumia mabavu ili kuweza kumtoa nje ya ukumbi Bw. Mbowe.
Sakata hilo lilifanikiwa baada ya askari hao kutii amri ya Naibu Spika huo kwa kutumia mabavu kumtoa nje kiongozi wa kambi ya upinzani ambapo aliungwa mkono na wabunge kutoka nje ya ukumbi na kususia kikao hicho.
Katika tukio hilo Mwenyekiti wa vyama vyenye wabunge wengi bungeni na Mbunge wa Jimbo la Vunjo Mkoani Kilimanjari Agustino Mrema alisema kuwa kitendo kilichofanywa na wabunge wezake si cha kungwa na na kinaleta fedheha kwa jamii na taifa kwa ujumla.
Alisema yeye kutokutoka kwake nje haimaanishi kuwa ni kibaraka wa CCM na si ndicho alichotumwa kufanya na wananchi wake,hivyo haungi mkono hata kidogo na haeleweke hivyo kuhusu msimamo wake.
"Hatoki mtu hapa nitakaa ndani ya bunge mpaka kieleweke na mnielewe kwamba mimi ndiye kiongozi wao vyama vyote tisa,hivyo nastahili kuheshimiwa na sikubaki humu ndani kwa sababu mimi ni kibaraka wa CCM bali kinachopiganiwa ni maslahi ya taifa na ndicho nilichotumwa na wananchi wangu sikutumwa nije kutoka nje au kususia bunge."alisema Mrema.
Naye, Mbunge wa Same Mashariki na Bi Anne Kilango Malecella aliitaka Serikali kusimama imara na isiogope vitisho vinavyotolewa na wasioitakiwa mema nchi katika kupigania maslahi ya taifa.
Alisema kuwa kitendo kilichofanywa na wapinzani bungeni hakina nia njema katika kupata katiba mpya na wajumbe 156 waliopiga kura wanavigenzo vya kuweza kuchangia Mswaada huo kujadiliwa.
Vurugu za bunge hilo ziliaza toka awali katika kipindi cha muongozo wa Spika ambapo vijembe,kashifa kwa wabunge kuzungumza bila kufuata utaratibu ilimradhimu Naibu Spika Job Ndugai kusimama mara kwa mara kujaribu kurejesha utulivu katika matukio yaliyotawala Ukumbini humo.
Mara baada ya kutolewa mwongozo ulioombwa na wabunge juzi wakidai Muswada wa Mabadiliko ya rasimu ya katiba umeingizwa vipengele kinyemele, na Zanzibar kutoshirikishwa kikamilifu, wabunge wa kambi rasmi ya upinzani bungeni na wale wa CCM walikuwa wakituhumiana kusema uongo kuhusiana na hatua hiyo ya uandaaji wa mchakato wa Rasimu wa Katiba mpya.
Thursday, September 5, 2013
KATIBU MKUU WA CCM TAIFA KUFANYA ZIARA KATIKA MIKOA YA SHINYANGA,MARA NA SIMIYU.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahaman Kinana septemba 10 anatarajiwa kuanza ziara ya kawaida katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara.
Ziara hiyo itaanzia katika mkoa wa Shinyanga septemba 10 mpaka 13 mwaka huu, kwa kutembelea wilaya zote nne za mkoa huo na kufuatiwa na mkoa mpya wa Simiyu kuanzia Septemba 14 mpaka septemba 19 kwa kutembelea wilaya zote tano Kabla ya kuhitimisha ziara hiyo kwa kutembelea wilaya Sita za mkoa wa Mara kuanzia Septemba 20 Mpaka 25 mwaka huu.
Katika ziara hiyo Katibu Mkuu wa CCM ataambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM anayeshughulikia Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye.
Kwa mujibu wa Ratiba ya ziara hiyo, Wajumbe hao wa sekretarieti watakagua uhai wa Chama ikiwa ni pamoja na kupokea wanachama wapya sanjari na kuhamasisha wananchi kujituma katika shughuli za uzalishaji ili Kuleta tija katika maisha Yao na ya taifa kwa ujumla.
Aidha watakagua maendeleo ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010/2015 hasa katika miradi ya kimaendeleo Kama vile Ujenzi wa majosho kwa ajili ya wafugaji, maendeleo ya maboresho ya kilimo cha Pamba, uvuvi wenye tija pamoja na maboresho ya sekta za Afya, elimu na miundombinu zikiwemo Barabara.
Katika ziara hiyo Katibu Mkuu atapata fursa ya kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kwa kushauriana na serikali kutafuta namna ya kuzitafutia ufumbuzi.Katibu mkuu pia atafanya mikutano ya ndani, na ya hadhara katika kila wilaya za mikoa hiyo.
Imetolewa na;
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi
05/09/2013
Nape Moses Nnauye
Katibu wa Itikadi na Uenezi
05/09/2013
MAONI YA MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA SHERIA NA KATIBA, MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA MAREKEBISHO YA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA, YA MWAKA 2013
(Kanuni ya
86(6) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2013)
UTANGULIZI
Mheshimiwa
Spika,
Huu
ni Muswada wa marekebisho ya pili ya Sheria
ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ya Sheria za Tanzania. Kama
Bunge lako
tukufu litakavyokumbuka, Sheria hii ilifanyiwa marekebisho ya kwanza kwa
kupitishwa kwa Sheria ya Marekebisho ya
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Na. 2 ya mwaka 2012, mwezi Februari
ya
mwaka jana. Mabadiliko hayo ya kwanza yalihusu Sehemu ya Tatu na ya Nne
ya
Sheria hii, na yalilenga vifungu mbali mbali vinavyohusu Tume ya
Mabadiliko ya
Katiba na utekelezaji wa majukumu yake.
Muswada
huu wa sasa unalenga kufanya marekebisho katika Sehemu ya Tano ya Sheria
inayohusu ‘Kuitisha Bunge Maalum.’ Sambamba na mapendekezo haya, kuna
mapendekezo ya kufanya marekebisho katika Sehemu ya Sita kwa kufuta
vifungu vya
32 hadi 36 vya Sheria vinavyohusu utaratibu wa kura ya maoni kwa ajili
ya
kuhalalisha ‘Katiba Inayopendekezwa.’ Marekebisho haya yamewekwa katika
aya ya
57 ya Muswada wa Sheria ya Kura ya Maoni,
2013. Mapendekezo ya Muswada huu ni muhimu lakini yana utata mkubwa.
Mheshimiwa
Spika,
Katika
kutekeleza majukumu yake ya kuuchambua Muswada huu, Kamati ya Bunge lako
tukufu
ya Katiba, Sheria na Utawala ilikutana na wadau wengi mbali mbali.
Hivyo, kwa
mfano, Kamati ilipata maoni ya taasisi za kidini na za kiraia; taasisi
za elimu
ya juu na za kitaaluma; vyama vya siasa na asasi nyingine. Kwa sababu
ambazo
Kamati haikuelezwa vizuri na uongozi wa Bunge hili tukufu, mapendekezo
ya
Kamati kwenda Zanzibar kwa lengo la kukusanya maoni ya wadau wa Zanzibar
juu ya
Muswada huu muhimu kwa mustakbala wa Jamhuri ya Muungano yalikataliwa.
Kwa
maana hiyo, ni muhimu Bunge lako tukufu lifahamu ukweli huu kwamba wadau
pekee
walioshirikishwa kutoa maoni yao juu ya Muswada ni Watanzania Bara tu.
Wazanzibari hawakupatiwa fursa hiyo na hawakushirikishwa kabisa, licha
ya
Sheria yenyewe kuwa na mambo mengi yanayoihusu Zanzibar. Kwa vile wadau
wa
Zanzibar walishirikishwa kikamilifu kutoa maoni yao kuhusu Muswada
uliopelekea
Sheria hii kutungwa mwaka 2011, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inataka
kujua
ni kwa nini uongozi wa Bunge na wa Serikali umeona si busara na sahihi
kuwapatia Wazanzibari fursa ya kutoa maoni yao kuhusu Muswada huu wa
kurekebisha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambayo inawahusu pia
Wazanzibari na
nchi yao.
URAIS
WA KIFALME KWA MARA NYINGINE TENA!!!!
Mheshimiwa
Spika,
Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni imepigia kelele jitihada za serikali hii ya
CCM
kudhibiti mchakato wa Katiba Mpya kwa kuendeleza kile tulichokiita miaka
miwili
iliyopita, “... kivuli kirefu cha Urais
wa Kifalme katika mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya.”[i]
Hapo tulikuwa tunazungumzia mamlaka ya Rais ya uteuzi wa Wajumbe na
watendaji
wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, na tulisema kwamba mamlaka hayo
yalikuwa na
lengo moja tu: “kuhakikisha kwamba
matokeo ya kazi ya Tume hiyo ni yale tu yanayotakiwa na Rais na Serikali
yake
na chama chake cha CCM.”
Mheshimiwa
Spika,
Katika
Maoni yetu wakati wa kutungwa kwa Sheria hii mwezi Novemba mwaka 2011,
Kambi
Rasmi ya Upinzani ilipinga vikali mapendekezo ya kumwezesha Rais kuteua
Wajumbe
wa Bunge Maalum wasiotokana na Bunge lako tukufu na Baraza la
Wawakilishi
Zanzibar. Tulisema yafuatayo kuhusiana na jambo hili: “... wajumbe
... wanaopendekezwa kuteuliwa kwenye Bunge la Katiba kwa
mujibu wa ibara ya 20(2)(e) na (4) ya Muswada Mpya sio, na hawawezi
kuwa,
wawakilishi wa wananchi. Kwanza, hawajachaguliwa na mtu yeyote na wala
taasisi
zao kuwawakilisha katika Bunge la Katiba kwa sababu Muswada Mpya
unapendekeza
wateuliwe na Rais.”
Kwa
sababu ya upinzani huo, mapendekezo ya kumfanya Rais kuwa mteuzi wa
wajumbe wa
Bunge Maalum wasiokuwa wabunge na Wawakilishi yaliondolewa katika
Muswada huo
wa Sheria hii. Badala yake, kifungu cha 22(1)(c) cha Sheria iliyotungwa
na
Bunge lako tukufu kiliweka wazi kwamba “wajumbe mia moja sitini na sita
[watateuliwa]
kutoka ...” taasisi zilizotajwa katika kifungu hicho.
Mheshimiwa
Spika,
Ni
kweli kwamba kifungu cha 22(1)(c) kama kilivyotungwa kilileta giza
badala ya
mwanga katika suala la uteuzi wa wajumbe hao. Kama tulivyoieleza timu ya
wataalamu wa Serikali kufuatia mkutano wetu na Rais Jakaya Kikwete
uliofanyika
Ikulu tarehe 26 Novemba, 2011: “Toleo la
Kiswahili la Sheria linasema kwamba wawakilishi wa makundi mengine
‘watakaoteuliwa kutoka’ kwenye makundi yaliyoorodheshwa. Toleo la
Kiingereza
linasema wajumbe hao watakuwa ‘drawn from’ (kwa tafsiri ya Kiswahili
‘watachukuliwa kutoka’). Maana za maneno haya hazifanani na wala hayako
wazi
kuhusu nani ‘atakayewateua’ au ‘kuwachukua’ wajumbe hao kutoka kwenye
taasisi
zao.”[ii]
Kwingineko
katika mkutano wetu na Rais Kikwete tulimweleza kwamba: “Wajumbe 166
wengine wanaowakilisha taasisi nje ya Wabunge na
Wawakilishi hawajachaguliwa na mtu yeyote na wala na taasisi zao kwani
Sheria
haisemi ni nani atakayewateua na/au kuwachagua.” Kwa sababu hiyo,
tulipendekeza kwamba “Sheria iweke wazi
kwamba wajumbe hawa ‘watateuliwa na’ taasisi zilizotajwa. Hii itaondoa
utata
juu ya uwakilishi wao na juu ya mamlaka yao ya uteuzi.”[iii]
Thursday, August 29, 2013
Tuesday, August 27, 2013
TAARIFA KUHUSU KUFUKUZWA KWA MBUNGE WA KIEMBESAMAKI NA KUTEULIWA KWA MAKATIBU WAKUU WAPYA CCM.
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya
Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyomalizika leo imejadili kwa kina Masuala
mbalimbali likiwemo pendekezo la Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa
Magharibi - Zanzibar la kumvua
uanachama Ndugu Mansoor Yussuf Himid, Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa
Kiembesamaki.
Baadhi ya tuhuma za Ndugu Mansoor Yussuf
Himid ni pamoja na:-
1.
Kushindwa
kusimamia malengo ya CCM na kutekeleza masharti ya uanachama.
2.
Kushindwa
kutekeleza wajibu wa mwanachama na kukiuka Maadili ya Kiongozi wa CCM.
3.
Kuikana
Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010-2015 na kuisaliti CCM.
Baada ya kujiridhisha vya kutosha na tuhuma
dhidi ya Ndugu Mansoor Yussuf Himid, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC)
imeridhia uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Magharibi Zanzibar wa
kumfukuza uanachama. Kwa uamuzi huo wa kumvua uanachama wa CCM Ndugu
Mansoor
Yussuf Himid, yeye kwa sasa sio Kiongozi tena wa CCM.
Imetolewa na:
Nape Moses Nnauye,
KATIBU
WA NEC ITIKADI NA UENEZI CCM TAIFA
26/08/2013
MAKATIBU WA CCM WA WILAYA WALIOTEULIWA NA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA TAIFA TAREHE 23/08/2013.
Monday, August 26, 2013
Thursday, August 22, 2013
ALICHOKISEMA ZITTO KABWE LEO.
Kimsingi Serikali ilidanganya Bunge ili Bunge
lipitishe bajeti ya Wizara ya Ujenzi mwaka 2011/12. Mawaziri Magufuli na
aliyekuwa Naibu yake Mwakyembe na Waziri wa Nchi Lukuvi kwa nyakati
tofauti walidanganya Bunge ili kupitisha jumla ya shilingi 252 bilioni.
PAC imeamua mawaziri hawa Waende kamati ya maadili ya bunge ili
kujieleza na kuadhibiwa kwa uwongo wao.
Magufuli - 'tunaomba
fedha tshs 252 bilioni kwa ajili ya KUANZA kazi za ujenzi wa barabara' -
2011...
Mwakyembe - 'fedha hizi zitachangia
miradi ya wafadhili' 2011
Lukuvi - 'hizi ni fedha kwa ajili ya
counterpart fund' 2011
2013
CAG - 'hizi fedha za miradi
hewa na kasma kivuli'.
Magufuli - ' tulilipa madeni'
Katibu Mkuu 'tulilipa madeni'
PAC ' kwanini mlidaganya
Bunge'? Mliomba fedha za kuanza miradi maalumu. Hamkuomba fedha za
madeni? Kwanini mliunda kasma kivuli na kuifuta baada ya pesa kulipwa?
Uamuzi
CAG akague fedha zote za kasma hii hewa na
kuripoti fedha hizi zimekwenda kwa wakandarasi gani na kutoa taarifa
kwenye kamati mwezi oktoba.
Mawaziri wote waliodanganya
Bungeni watashtakiwa kamati ya maadili na kudanganya bunge kwa lengo la
kupitisha bajeti ya tshs 252 bilioni kufadhili miradi hewa.
Source:Zitto Social Media.
Monday, August 19, 2013
MTAZAMO WA ZITTO KABWE JUU YA RASIMU YA KATIBA.
Rasimu ya Katiba ibara ya 215 inasema vyanzo vya
mapato ya Muungano, kikubwa, ni ushuru wa bidhaa. Wajumbe wa Tume
wanasema walifanya hesabu sawa sawa na fedha hizo zitatosha kuendesha
Muungano. Lazima aliyewafanyia hayo mahesabu ama aliwapotosha au hajui.
Mwaka 2012/13 Ushuru wa bidhaa (ndani na nje) uliingiza mapato ya tshs
1.5 trilioni tu. Fedha hii inatosha kuendesha Wizara ya Ulinzi peke
yake!
Haitoshi hata kuhudumia Deni la Taifa (ambalo mkopaji ni
Jamhuri ya Muungano). Huu muungano utaendeshwaje?
Rasimu inapaswa
kufanyiwa kazi sana. Nahisi Tume ilikuwa na haraka na haikutafakari kwa
kina baadhi ya masuala.
Mambo ya Muungano inabidi yaangaliwe upya
kabisa ili kuboresha mfumo wa Serikali 3 unaopendekezwa ikiwemo kuzuia
Washirika wa Muungano kuunda vikosi vyao vya kijeshi, Ulinzi na usalama.
Suala la biashara ya kimataifa na hata suala la usimamizi wa maliasili
(regulatory function).
Source:Zitto Social media.
Sunday, August 18, 2013
ALICHOKISEMA ZITTO KABWE LEO.
Katika moja ya maazimio ya Kamati za Bunge za
mahesabu ya Umma (Kamati ya Hesabu za Serikali, Kamati ya Hesabu za
Serikali za Mitaa na Kamati ya Bajeti) iliamuriwa kuwa Serikali ianze
utaratibu wa kukusanya maduhuli yake kwa kutoa risiti za kielektroniki.
Azimio hilo linasema
“Maduhuli ya Serikali sasa yakusanywe kwa
kutumia risiti za elektroniki. Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na
Mashirika ya Umma yaanze kutumia risiti za eletroniki mara moja ili
kudhibiti upotevu wa mapato ya serikali yanayotokea hivi sasa katika
kutumia risiti zinazoandikwa kwa mkono. Pia ofisi za serikali zifanye
manunuzi yake kwa wafanyabiashara wanaotumia mashine za kielektroniki.”
Nimepitia Mpango wa Serikali wa Mapato (Volume I – Financial Statement
and Revenue Estimates 2013/14) na kugundua kuwa mapato yasiyo ya kikodi
yamekadiriwa kuwa ni shilingi bilioni 741 kutoka Wizara, Idara na Mikoa
na shi...lingi bilioni 383 kutoka kwenye Halmashauri za
Wilaya, Miji na Manispaa. Sikuweza kupata mapato ya Mashirika ya Umma
maana hayaletwi kwenye Bajeti za Serikali.
Wizara 10 zinazoongoza
kwa Mapato (mapato kwenye mabano ni Wizara ya Nishati na Madini ( 220
bn), Wizara ya Fedha (126bn), Wizara ya Ardhi (100 bn), Wizara ya
Maliasili (84 bn), Wizara ya Mambo ya Ndani – Uhamiaji (92 bn), Wizara
ya Mifugo (19 bn), Wizara ya Mambo ya Nje (16 bn) na Wizara ya Mambo ya
Ndani – Polisi (17 bn), kati ya hizi shilingi 16 bilioni ni kutoka idara
ya Trafiki (traffic notification fees).
Kutokana na mafanikio ya
makusanyo ya VAT ambapo inaonyesha kuwa mapato ya Serikali yameongezeka
kwa asilimia 60 (kutoka 500 bn mpaka 800 bn), na kutokana na rekodi
mbalimbali za Serikali zinazoonyesha kuwa zaidi ya asilimia 50 ya
makusanyo ya Serikali hayafiki Serikalini, ni dhahiri kuanzishwa kwa
makusanyo kwa risiti za kielektroniki kutapandisha mapato ya Serikali
zaidi ya mara mbili. Idara ya Usalama barabarani peke yake inasemekana
kuwa makusanyo ya sasa ni theluthi tu ya makusanyo stahili kutokana na
rekodi za ‘notifications’ barabarani.
Risiti za elektroniki kwa
kukusanya maduhuli ya Serikali yanaweza kuongeza mapato ya Serikali
maradufu na kuepuka mtindo wa Serikali wa kupandisha kodi kwenye bidhaa
muhimu kwa wananchi. Uamuzi wa Kamati za Bunge za Mahesabu wa kuitaka
Serikali kukusanya maduhuli yake kwa kutumia risiti za elektroniki
unapaswa kuungwa mkono na kila Mtanzania.
Zitto Kabwe
MBOWE AWAKARIBISHA CHADEMA MADIWANI WALIOTIMULIWA CCM MKOANI KAGERA, AWAPA MBINU
MADIWANI
wanane wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Kagera waliofukuzwa
uanachama wiki iliyopita wamekaribishwa kujiunga na Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (CHADEMA).
Mwenyekiti wa
CHADEMA, Freeman Mbowe, ndiye aliyewakaribisha madiwani hao wanaosubiri
kufukuzwa rasmi na vikao vya Kamati Kuu ya CCM, vinavyotarajiwa
kufanyika wiki hii mkoani Dodoma.
Madiwani
waliofukuzwa na kata zao kwenye mabano ni Richard Gaspar (Miembeni),
Murungi Kichwabuta (Viti Maalumu), Alexander Ngalinda ambaye pia ni
naibu meya (Buhembe), Yusuf Ngaiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa
wilaya (Kashai), Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga), Robert Katunzi
(Hamugembe), Samwel Ruhangisa (Kitendagulo) na Dauda Kalumuna
(Ijuganyondo).
Akihutubia
katika mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Uhuru wa Bukoba Mjini, Mbowe
alisema CCM imewachakachua madiwani hao wanane na hata wakibaki huko
chama chao hakitawaona wa maana, kwa sababu chama hicho kinalea ufisadi.
Mbowe alisema
CHADEMA wako tayari kuwapokea madiwani hao waliofukuzwa na kuwafundisha
siasa za mageuzi.
“Tutasimama
nao katika kujenga Bukoba mpya isiyo na ufisadi kama unaofanywa na Meya
wa manispaa hiyo iwapo wataamua kuja kwetu, milango ipo wazi
nawakaribisha,” alisema.
Mbowe alisema
CHADEMA kinamuunga mkono Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Hamis Kagasheki
(CCM), anayepinga ufisadi unaofanywa na meya kutoka chama chake, Anatory
Amani.
Alisema
CHADEMA itashirikiana na kiongozi yeyote kutoka CCM atakayekuwa tayari
kupambana na ufisadi ulioshamiri kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.
“CHADEMA
katika mambo ya ufisadi ina msimamno unaoeleweka na kwamba katika
kupinga ufisadi kipo tayari kumuunga mkono yeyote bila kujali itikadi,”
alisema Mbowe na kusisitiza kwamba hata kama meya angekuwa mwanachama wa
CHADEMA kingeunga mkono afukuzwe.
“Hatuna
masilahi ya kisiasa na Kagasheki lakini katika suala hili tunamuunga
mkono. Nawapongeza madiwani wetu wa CHADEMA walioungana na mbunge huyo
kupinga ufisadi wa meya na kusimamia masilahi ya wananchi wa Bukoba
Mjini,” alisema Mbowe.
Mbowe
aliikejeli CCM kuwa haiwezi kuwafukuza madiwani hao kwa sababu itakuwa
imejimaliza na hawana uhakika wa kuzirejesha kata hizo ukiitishwa
uchaguzi.
Alisema
kutokana na hofu hiyo Makao Makuu ya CCM yaliamua kuwarejesha madiwani
hao wanane waliofukuzwa na CCM Mkoa wa Kagera.
Subscribe to:
Posts (Atom)