Monday, October 21, 2013

SIMBA TIMU BORA KATIKA MECHI YAKE NA MTANI WA JADI YANGA.

Simba ikiwa chini ya kocha wake mkuu King Kibandeni imeonekana kuwa timu bora baada ya kuweza kusawazisha goli 3 alizokuwa ameshafungwa na mpinzani wake Yanga zilizofungwa katika kipindi cha kwanza.
Young Africans ilitoka sare ya mabao 3-3 na Simba SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom uliofanyika jana katika dimba la uwanja wa Taifa ambapo mchezo huo umeshuhudia mabao yote sita yakifungwa katika upande wa kusini mwa uwanja.
Baada ya kosa kosa ya Hamis Kiiza dakika ya tisa ya mchezo, Mrisho Ngassa aliipatia Young Africans bao la kwanza dakika ya 14 ya mchezo akimaliza pasi ya Kiiza aliyewatoka walinzi wa Simba SC na Ngassa kuukwamisha mpira wavuni.
Didier Kavumbagu alikosa bao la wazi kufuatia mpira aliopiga kutoka seintimeta chache langoni kabla ya tik tak ilyopigwa na Ngassa kupaa pia juu ya lango la Simba SC liliokuwa chini ya Abeid Dhaira
Hamsi Kiiza aliipatia Young Africans bao la pili dakika ya 35 ya mchezo, akimalizia pasi ya Mrisho Ngasa aliyemtoka mlinzi wa Simba SC Nassoro Maoud Chollo na mpira huo kumkuta mfungaji aliyeukwamisha wavuni.
Dakika ya 45 ya mchezo, Hamis Kiiza tena aliipatia Young Africans bao la tatu baada ya pira uliorushwa na Mbuyu Twite kuguswa na kichwa cha Didier Kavumbagu na kumkuta Kiiza ambaye alifanya kazi yake ya kuukwamisha mpira wavuni.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika, Simba SC 0 -3 Young Africans.
Kipindi cha pili kilianza kwa Simba kufanya mabadiliko, ambapo mabadiliko hayo yaliwaongezea uhai katika dakika ya 55 uzembe wa Nadir Haroub 'Cannavaro' ulimpelekea mshambuliaji wa Betram Mombeki kuipatia timu yake bao la kwanza.

Dakika tatu baadae kona iliyopigwa na nahodha wa Simba Chollo ilimkuta mlinzi wa kati wa Joseph Owino akiwa peke yake na kuukwamisha mpira wavuni na kuhesabu bao pili kwa wekundu wa msimbazi.
Young Africans ilionekana kupotea kabisa kipindi cha pili, kwani soka walilolionyesha kipindi cha kwanza halikuoneka tena hali iliyopelekea Gilbert Kaze kuipatia timu yake bao tatu la kusawazisha kwa kichwa kufuatit mpira wa adhabu uliopigwa na Nassoro Masoud kumkuta mfungaji akiwa peke yake.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Simba SC 3 -3 Young Africans.
Mara baada ya mchezo kocha mkuu wa Yanga amesema amesikitishwa na matokeo ya mchezo huo na hasa kipindi cha pili timu yake haikucheza vizuri, na lawama akizitoa kwa wachezaji wake kuridhika na matokeo ya kipindi cha kwanza hali ambayo ndio iliyowagharimu kipindi cha pili.
Young Africans: 1.Barthez, 2.Mbuyu, 3.Luhende, 4.Nadir, 5.Yondani, 6.Chuji, 7.Niyonzima, 8.Domayo, 9.Kavumbagu, 10.Ngassa, 11.Kiiza/Msuva
Subs: Deogratia Munisi, Juma Abdul, Oscar Joshua, Simon Msuva, Rajab Zahir, Jerson tegete, Nizar Khalifan Simba SC: 1.Dhaira, 2.Chollo, 3.Shamte, 4.Kaze, 5.Owino, 6.Mkude, 7.Singano, 8.Humud/Ndemla, 9.Mombeki/Pazi, 10.Tambwe, 11.Chanongo/William
Subs: Abuu Hashim, Hassan Khatir, Issa Rashid, Zahoro Pazi, Amri Kiemba, Said Hamisi, William Lucian

No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...