Tuesday, April 16, 2013

BUNGENI DODOMA NI AIBU TUPU, JUMA NKAMIA AMRUKIA SUGU.

Mh.Juma Nkamia,mbunge wa Kondoa Kusini.
Katika vikao vya bunge vinavyoendelea Mjini Dodoma,mambo mbali mbali yanajitokeza siku hadi siku.

TABIA ya waheshimiwa Wabunge kurushiana matusi wakati wa mijadala ya Bunge, imezidi kushika kasi, baada ya tabia hiyo kuendelea tena jana wakati wa mjadala wa hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2012/13.

Pamoja na tabia hiyo kuendelea tena jana, wiki iliyopita Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu (CHADEMA), alisema Baraza la Mawaziri linaundwa na mawaziri wapumbavu.
Kwa siku ya jana, tabia hiyo ilianzia kwa Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM), kisha ikasisitizwa na Mbunge wa Kondoa Kusini, Juma Nkamia (CCM).

Wakati Nkamia akichangia bajeti hiyo na kueleza jinsi asivyokubaliana na vitendo vya udini vinavyodaiwa kuwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Sugu aliingilia kati bila kuruhusiwa na kusema, je Lwakatare.

Baada ya Sugu kusema neno hilo, Nkamia alikatisha kuchangia na akasema:

Sugu naomba unyamaze mimi ndiye nazungumza, mimi siongei na mbwa naongea na mwenye mbwa,” alisikika Nkamia.

MAOMBI YA LWAKATARE KUFUTIWA KESI YAZUA TAFRANI MAHAKAMANI, WAANDISHI WA HABARI WAFUNGIWA NJE.

Katika taarifa iliyokutwa katika mtandao wa kijamii wa CHADEMA ilikuwa hivi:-

"Uamuzi wa kusikiliza maombi hayo katika ofisi badala ya mahakama ya wazi ulizua manung’uniko na malalamiko kutoka kwa waandishi, wanachama wa Chadema na wafuasi wao, huku baadhi ya wafuasi wa Chadema wakiwaporomoshea matusi makali Polisi waliokuwa wakilinda usalama mahakamani hapo.


Hata hivyo, Machi 20, 2013, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), aliwafutia mashtaka, lakini muda mfupi baadaye walikamatwa na kufunguliwa mashtaka hayohayo katika kesi namba 6 ya 2013.
Mawakili wanaomtetea Lwakatare hawakukubaliana na uamuzi huo, hivyo waliwasilisha maombi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, wakiupinga. Pia waliiomba mahakama hiyo itengue uamuzi huo.
Maombi hayo yalisikilizwa jana na Jaji Lawrence Kaduri, lakini waandishi wa habari walizuiwa kuingia ofisini kwa Jaji Kaduri ambamo kesi hiyo ilifanyika.
Wanahabari walikuwa miongoni mwa watu waliofika mapema mahakamani hapo na kuungana na umati mkubwa wa wanachama na wafuasi wa Chadema kusubiri ukumbi wa mahakama ufunguliwe.
Baadaye walitangaziwa kuwa maombi hayo yatasikilizwa ofisini kwa Jaji Kaduri, hivyo askari Magereza waliwazuia waandishi wa habari kwa maelezo kuwa ofisi hiyo ni ndogo na kwamba tayari ilikuwa imejaa, hivyo hapakuwa na nafasi ya kuingiza watu zaidi.
Miongoni mwa waliopata nafasi ya kuingia katika ofisi ya Jaji Kaduri ni Lwakatare na Ludovick, mawakili wao watatu, mawakili wa Serikali watatu, mke wa Lwakatare na Karani wa Jaji Kaduri.
Wengine ni Mwenyekitiwa Chadema, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dk Willibrod Slaa na baadhi ya askari Magereza.Waandishi wa habari walipinga kitendo hicho na baada ya mvutano uliodumu dakika kadhaa, askari hao walimruhusu mwandishi mmoja tu kuwakilisha wanzake.

Kwa kawaida kesi za jinai na hasa zenye mvuto kwa umma kama ilivyo ya Lwakatare husikilizwa katika mahakama ya wazi na hata mawakili walikuwa wamejiandaa kusikiliza maombi hayo katika mahakama ya wazi, kwani walikuwa wamebeba majoho ambayo kwa kawaida huvaliwa kwenye mahakama za wazi.
Uamuzi wa kusikiliza maombi hayo katika ofisi badala ya mahakama ya wazi ulizua manung’uniko na malalamiko kutoka kwa waandishi, wanachama wa Chadema na wafuasi wao, huku baadhi ya wafuasi wa Chadema wakiwaporomoshea matusi makali Polisi waliokuwa wakilinda usalama mahakamani hapo.
Maombi yasikilizwa
Wakili wa Serikali Mkuu, Prudence Rweyongeza akisaidiana na wenzake Peter Maugo na Ponsiano Lukosi alisema DPP alifuta mashtaka ya Lwakatare na mwenzake kwani kesi ya awali ilifunguliwa katika masjala isiyostahili.
Rweyongeza alidai kuwa kesi ya kwanza ilisajiliwa katika kitabu cha kesi zinazosikilizwa na Mahakama za chini, badala ya kitabu cha kesi zinazosikilizwa na Mahakama Kuu.
Aliitaja sababu nyingine kuwa, mahakama ilikosea kwa kuwaruhusu washtakiwa kujibu mashtaka ambayo husikilizwa na Mahakama Kuu pekee.
Katika hoja zao, wadai wakiongozwa na Wakili Peter Kibatala, walisema DPP alikosea kuchukua uamuzi huo kwa kuwa madaraka yake yana mpaka na kwamba hapakuwa na sababu wala mazingira yanayoelezwa katika sheria ya DPP kuchukua uamuzi huo.
Pia Wakili Kibatala akisaidiana na Wakili Tundu Lisu walihoji uhalali wa mashtaka hayo ya ugaidi wakidai kuwa hakuna maelezo yanayoonyesha kuwa mashtaka yanayomkabili Lwakatare na mwenzake ni ya ugaidi. Hivyo waliiomba Mahakama Kuu iyatupilie mbali mashtaka hayo.
Hata hivyo, Rweyongeza alidai ni mapema kutoa hoja za uhalali wa mashtaka kwa kuwa kesi hiyo bado iko katika hatua ya uchunguzi na kwamba baada ya uchunguzi inaweza kuwa na mabadiliko yoyote.
Hatima ya maombi hayo imebaki mikononi mwa Jaji Kaduri ambaye baada ya kusikiliza hoja za pande zote aliahirisha shauri hilo hadi atakapotoa uamuzi wake kwa tarehe ambayo atawajulisha wahusika wa kesi hiyo."

Sunday, April 14, 2013

VITA YA CHADEMA NA CCM IMECHUKUA SURA MPYA,CHADEMA WATOA TAMKO

TAMKO LA CHADEMA KUHUSU NJAMA ZA KUKICHAFUA ZINAZOFANYWA NA GENGE LA VIONGOZI WAKUU WA CCM NA VYOMBO VYA DOLA, LIMETOLEWA JIJINI DAR ES SALAAM LEO, APRILI 14, 2013 NA MJUMBE WA KAMATI KUU NA MWANASHERIA WA CHAMA, MH. MABERE NYAUCHO MARANDO

Ndugu waandishi wa habari;
LEO tumewaita hapa ili kuwaomba mtufikishie ujumbe kwa Watanzania, kwamba nikiwa mwanasheria na mtu ambaye nimepata ujuzi wa kazi za ushushu, nimefanya uchunguzi matukio haya ya utekaji na utesaji na kugundua mambo mengi mno.

Uchunguzi huu nimeufanya kabla na baada ya kukamatwa kwa Mkurugenzi wetu wa Ulinzi na Usalama, Willifred Muganyizi Lwakatare, ambaye hivi sasa anashitakiwa mahakamani kwa tuhuma za kupanga ugaidi.

Nimefanya hivyo kwa kuangalia maslahi mapana ya taifa langu na chama changu. Katika uchunguzi wangu huo, nimegundua mambo mengi ikiwamo kuwapo kwa genge la watu ndani ya serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaopanga mipango hii ya kishetani na kisha kuwasingizia watu wengine.

Angalieni mfano huu: Unaoitwa na polisi na Mwigulu Nchemba, “mkanda wa Lwakatare” unadaiwa uliwasilishwa jeshi la polisi Desemba mwaka jana. Lakini jeshi hilo halikumkamata yoyote wala kumhoji, hadi pale Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda, alipovamiwa na kuumizwa. 

Aidha, Nchemba amedai kumiliki video ile Desemba mwaka jana, lakini rekodi hiyo iliwekwa kwenye mitandao ya kijamii (YouTube na Jamii Forum) baada ya kutekwa kwa Kibanda. Hapa mtu makini anaweza kujiuliza, hiki kimelenga nini? 

Kwamba genge hili la kina Nchemba na wenzake, walipanga kumteka Kibanda, wakatimiza lengo lao hilo, baadaye wakaingia kwenye plani B ya kutaka kuihusisha Chadema. Wakamtumia Ludovick Joseph Rwezahula ambaye ni mshitakiwa wa pili katika kesi ya Lwakatare, kufanikisha mkakati wao huu wa kishetani. 


Ndugu waandishi wa habari;
Huu ni mchezo mchafu na wahatari mno ambao kwa vyovyote vile, haupaswi kuvumiliwa. Kuanzia sasa nimeamua kwa dhati kabisa, kukomesha mchezo huu ambao unahatarisha uhai wa taifa letu.

Kwa kuanzia, kesho Jumatatu, nitaongoza jopo la mawakili sita wa Chadema kumtetea Bw. Lwakatare. Wenzangu wengine katika kesi hii, ni Profesa Abdallah Safari, Tundu Lissu, Edson Mbogoro, Peter Kibatara na Nyaronyo Kicheere. Huko mbele tutaongeza mawakili wengine, akiwamo mmoja anayewekwa na familia ya Lwakatare. 

Ndugu waandishi wa habari;
Mnaweza kujiuliza, kwa nini Chadema kimechukua uamuzi huu wa kuweka kundi kubwa la wanasheria katika kesi hii ya Lwakatare? Jibu ni kwamba tumegundua kuwa kesi hii imefunguliwa kwa lengo maalum la kuidhoofisha Chadema na kuinusuru CCM ambayo inakabiliwa na dhahama ya kushindwa katika uchaguzi mkuu ujao kutokana na kushamiri kwa makundi. 

Hivyo wameamfungulia kesi Lwakatare, kwa lengo la kutaka kuaminisha umma kuwa Chadema ni chama cha magaidi, kinapanga ugaidi na hivyo kichukiwe. Hilo ndilo lengo lao. Basi!

Ndugu waandishi wa habari; 
Pili, nitakwenda mahakamani kuwasilisha ombi maalum la kuomba amri ya mahakama kuagiza makampuni ya simu za mkononi kuwasilisha mahakamani statement za simu za watu kumi (10) ili kusaidia mahakama kutenda haki na jamii kujua ukweli wa mambo haya. 

Watu ambao nitaomba mahakama itoe amri ya kuletwa taarifa zao simu 
na meseji (sms) ni Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa nchini (TISS), Jack Zoka, anayetumia simu Na. 255756809535, Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Lameck Nchemba, anayetumia simu tano zikiwamo 0754 008888, 0757 946223, 0714 008888 na 0787 513446 na Ludovick Joseph Rwezahula, ambaye simu zake ni,0715 927100 na 0753 927 100.

Mwingine ambaye mawasiliano yake yanahitajika, ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Emmanuel Nchimbi, anayetumia simu Na. 0754 003388, Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Mwananchi, Dennis Msaky anayetumia simu mbili, 0655 331010 na 0764 331010 na Bw. Sinbad Mwagha, ambaye ni afisa wa idara ya usalama wa taifa, anayetumia simu 0754 006355. 

Wengine, ni Bw. Shaali Ali, afisa mwinge wa usalama wa taifa anayetumia simu Na. 0716990099, Saumu K. Malungu, mwenye kutumia simu 0719 541 434 na 0789 614 629, simu mbili zinazotumiwa na mtuhumiwa mkuu wa utekaji wa Dk. Steven Ulimboka, Bw. Ramadhani Abeid Igondo ikiwamo 0713 760 473, simu za Bw. Ridhiwani Kikwete ambazo ni 0754 566299, 0784 566 299, simu ya Dr. Steven Ulimboka, ambayo ni 0713 0713 731 610, pamoja na simu zote tatu za Willifred Lwakatare, ambazo ni 0786 774697, 0713 237869 na 0758 417169.
Ndugu waandishi wa habari; 
Mtu mwingine muhimu nitakayeomba mahakama itoe amri ya kutolewa kwa taarifa zake, ni mwandishi wa habari na mpigapicha wa magazeti ya serikali, Muhidini Issa Michuzi. Mwandani huyu wa Ikulu, ndiye aliyeandika ujumbe kwa njia ya emeili kuipongeza ofisi binafsi ya rais (OBR) na usalama wa taifa kwa kupata video ya Lwakatare. 

Pongezi za Michuzi kwa TISS ndizo zinanisukuma kuiomba mahakama kuagiza kupatikana taarifa zake. Michuzi anaipongeza TISS kwa kuibua njama za wahalifu, lakini mimi ninajua TISS ikipata njama za aina hiyo haraka inapeleka ushahidi polisi, lakini huu wa Lwakatare ulipelekwa Youtube, badala ya kwenye vyombo vya sheria.

Maneno ya Michuzi kwamba ni TISS imeibua hiyo video yanathibitisha ushiriki wa TISS kwenye mchezo huo mchafu, na kwamba Chadema kinajua kuwa Michuzi alishirikiana na watu wa usalama wa taifa katika kazi hiyo chafu. Software za video (editing) walizotumia zilitoka kwake. Fedha ya kuandaa hiyo video zilitoka usalama na Ikulu. Tunajua kuwa wale vijana wa Ada Estate na yule jamaa anayempelekea kigogo wa Jamii Forum, walilalamika sana kwa mmoja wa wamiliki wa JF. 

Ndugu waandishi wa habari;
Chadema kinajua kuwa mmoja wa watuhumiwa hawa, Mwigulu Nchemba anafanya mipango na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom ili kumsaidia kufuta taarifa zake. Nachukua nafasi hii, kuionya kampuni hiyo kuacha kucheza mchezo huo kwa kuwa ni kinyume cha sheria za mamlaka ya mawasiliano (TCRA).

Tunahitaji mawasiliano haya kwa kuwa Mwigulu – zinaonyesha mtuhumiwa huyo akifanya mawasiliano mfululizo na Ludovick, yakiwamo yale ya tarehe 4 Machi 2013. Hii ilikuwa siku moja kabla ya Kibanda kutekwa.

Ndugu waandishi wa habari;
Hawa niliowataja ni watu muhimu sana katika upangaji wa mkakati wa utengenezaji wa video ya Lwakatare na vitendo vya kihalifu vya utekwaji wa Kibanda na tukio la kutekwa na kisha kutupwa msutuni kwa mwenyekiti wa Jumuiya ya madaktari nchini, Dr. Steven Ulimboka.

Kwa mfano, simu ya Mwigullu Nchemba, namba 0714 008888, 0756 008888 na 0757 946223, zimefanya mawasiliano mara kadhaa na Ludovick Joseph, Saumu K. Malungu, Jack Zoka, Ali Shaali na Ramadhani Ighondo. Mawasiliano hayo yalifanyika katika kipindi ambacho mgomo wa madaktari ulishamiri; baadaye yakarudi tena kati ya 26 Desemba mwaka jana na 15 Machi mwaka huu.

Miongoni mwa mawasiliano ambayo tunaona yanahusika na ujambazi huu, ni yale ya 28 Desemba, siku ambayo mkanda wa Lwakatare umerekodiwa; tarehe 4 hadi 6 Machi 2013, siku moja kabla ya Kibanda kutekwa na yale ya usiku wa manane (saa 8:17) wa 13 Machi 2013, ambako mchana uliofuata Lwakatare alikamatwa. 
Huyu Mwagha ndiye aliyekuwa anatumika kuwasiliana na Saumu Malungu, ambaye tulimtaja kuwa ndiye aliyekuwa amepewa kazi na Mwigulu na usalama wa taifa, kurubuni vijana wetu kwa fedha ili kutoa ushahidi wa uongo juu ya video ya Lwakatare.

Vilevile, mawasiliano ya Mwiguluna Mwagha, katika kipindi hicho nayo tunayahitaji. Kwa sababu, huyu Mwagha anayetumia simu 0754006355, mbali na kuwasiliana na Mwigulu, ndiye aliyekuwa anawasiliana na mmoja wa waliomteka Ulimboka; na ndiye aliyewasiliana na Saumu kati ya 20Januari na Machi 6 mwaka huu.

Ndugu waandishi wa habari;
Ludovick alifanya mawasiliano ya mwisho na Joyece Agustine, ambaye anatumia simu Na. 0717 559210, mawasiliano ambayo yalifanyika saa 5:13 usiku. Hiyo ndiyo ilikuwa simu yake ya mwisho usiku huo; katika siku hiyo Ludovick aliwasilisna na Joyce mara tisa kuanzia saa 12: 54 asubuhi.

Kwa mujibu wa taarifa za kwenye mtandao wa Jamii Forum, ambako video ya Lwakatare ilitumwa, Ludovick alikamatwa Machi 15 mwaka huu. Hata hivyo, rekodi katika simu yake Na. 0715 927100 inaoyesha 17 Machi Ludovick alifanya mawasiliano na Joyce Augustino. Mawasiliano hayo yalifanyika saa 8: 9 usiku, wakati inadaiwa na polisi alishakamatwa.

Naye mhariri wa Mwananchi, Bw. Msaky ambaye anatajwa kutaka kutekwa na Ludovick na Lwakatare, amekuwa na mawasiliano kadhaa na Ludovick – mtu anayepanga kumteka. Ludovick na Msaky walifanya mawasiliano mfululizo kati 27 Desema 2012, siku moja kabla ya video ya Lwakatare haijarekodiwa na 7 Machi siku moja baada ya Kibanda kutekwa. 

Msacky alitumia simu zake hizo mbili (0764 331010 na 0655 331010) kuwasiliana na Ludovick, huku Ludovick akitumia 0753927100. Mawasiliano ya 31 Desemba yalifanyika Ludovick akiwa Tegeta, jijini Dar es Salaam. Mawakala hawa wawili wa usalama wa taifa (Ludovick na Msaky), walikutana 31 Desemba 2012, katika hoteli ya Tamal, Mwenge jijini Dar es Salaam.

Ndugu waandishi wa habari;
Baada ya kupitia taarifa hizi za mawasiliano ya simu za Mwigulu Nchemba, Ludovick Joseph, Ramadhani Ighondo na Saumu Malungu tumegundua yafuatayo: Kwamba, Ramadhani Ighondo, amefanya mawasiliano mara nyingi na Mwigulu, Mwagha na Zoka; naye Mwagha amefanya mawasiliano na Mwigulu na Saumu; naye Saumu amefanya mawasiliano na Mwagha, Mwiguluna Shaali Ali, ambaye ni afisa usalama wa taifa.

Tumegundua vilevile, kuwapo mawasiliano kadhaa kati ya Ludovick na Msaky; Ludovick na Mwigulu; Msaky na Nchimbi; Msaki na Mwagha, Samu na Mwagha na Ramadhani Ighondo Abeid, anayetuhumiwa kumteka Dk. Ulimboka na Mwanga na Mwigullu.

Tumegundua pia kuwapo mawasiliano kati ya Ulimboka na Ramadhani; Zoka na Ighondo na Ridhiwani na Ighondo. Mawasiliano haya yalifanywa mfululizo usiku wa Juni 2012 siku ambayo Dk. Ulimboka alitekwa.

Tumepata kufahamu pia kwamba baadhi ya watu waliotajwa na gazeti la MwanaHALISI kuwa waliwasiliana na Ighondo usiku wa Juni 26, mwaka 2012, wamefanya mawasiliano pia na Mwigulu, Mwagha na Shaali Ali.

Ndugu waandishi wa habari;
Mwagha ni afisa usalama wa taifa anayefanyakazi makao makuu ya idara hiyo. Ndiye yule anayetumika kuendesha michezo ya kuhonga wanasiasa wa CCM na upinzani. Ni Mwagha anayepanga wabunge na kuwapanga waongee nini kwa maslahi ya CCM. Ushenzi wote anaoongea Mwighulu bungeni, hupewa na Mwagha kwa maelekezo ya Jack Zoka.

Naye Shaali ndiye aliyekutana na afisa wetu wa usalama, Ahmed Sabula na mwenzake, Machi 29 mwaka huu katika hoteli ya See Cliff jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo kati ya Sabula, kijana wetu wa usalama na afisa usalama wa serikali Bw. Shaali alitaka Sabula akubali kutumika kwa kutoa taarifa za vikao vya chama, kuwasilisha kwake nyaraka za kamati kuu na kueleza mipango ya chama katika kesi ya Lwakatare. 

Kwenye mpango huu, afisa huyo wa usalama wa taifa ambaye ninamfahamu vizuri, alimuahidi Sabula kiasi cha Sh. milioni 30 na kwamba fedha hizo angelipwa wiki iliyopita. Aliahidiwa pia kwamba kila nyaraka atakayopeleka atalipwa ujira. 

Aidha, Sabula aliahidiwa kulipwa shilingi 500,000 (laki tano) kila mwezi; afisa wetu huyu ameripoti tukio hilo kwa viongozi wake wa chama. Yule mwenzake aliandaliwa kuwa shahidi wa kesi ya Lwakatare; aliambiwa akikubali dili hiyo atalipwa kila mwezi Sh. 500, lakini akaombwa kuwa mvumilivu kwa kuwa atalazimika kupotea kwa miezi kama mitano hadi sita.

Ndugu waandishi wa habari;
Kitendo cha Mwigulu kuwasiliana Ramadhani Ighondo, Mwigulu kuwasiliana na Ludovick, Saumu kuwasiliana na Mwigulu, Ighondo kuwasiliana na Ulimboka, Zoka kuwasiliana na Ighondo, tena katika muda uleule ambao Ighondo amewasiliana na Ulimboka na Saumu kuwasiliana na Mwagha, ni uthibitisho tosha kwamba usalama wa taifa wako nyuma ya mipango hii ya michafu ya kupanga utekaji na kisha kutaka kukichafua Chadema.

Aidha, kitendo cha Ludovick kuwasiliana Msaky; Ighondo kuwasiliana na Mwagha, Ridhiwani Kikwete kuwasiliana na Ighondo, tena kila baada ya Ighondo kuwasiliana na Ulimboka na Jack Zoka, ni uthibitisho mwingine kuwa genge hili la wahalifu linashirkiana na baadhi ya watu kutaka kuangamiza taifa.

Ni uthibitisho tosha kwamba hawa ndiyo wanaowahonga wanachama wa Chadema na watu wengine ili watoe ushahidi feki dhidi ya Lwakatare, na kwamba ni usalama wa taifa walioandaa ile video uchwara inayopigiwa chapuo na Mwigulu.

Ndugu waandishi wa habari;
Chama Cha Mapinduzi kinajua kwa hali ya sasa hakiwezi kushinda uchaguzi wa mwaka 2015 huku Chadema ikiwa katika hali nzuri ya kisiasa tunayoiona sasa. Wanajua kabisa CCM imegawanyika, kundi lolote litakalopita ndani ya CCM, litahujumu kundi jingine. Ni kama ilivyotokea uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki.

Ndiyo maana wanapanga kila mbinu kutaka kuiangamiza Chadema. Nasi tunasema katu hatutakubali kuona Chadema kinakufa. Tutapambana usiku na mchana. Juna na mvua. Hadi tushinde hila hizi.Tunawaambia wanachama wetu na wale wanaotuunga mkono, Chadema ni chama kikubwa. Kina mtandao kila mahali, kuanzia Ikulu hadi polisi; na hivyo hakitakufa au kuzorota kwa mambo ya kupikwa.

Ni imani yangu kwamba amri ya mahakama itawafichua wote hawa ni kuirudisha Tanzania katika amani yake. Ni lazima tufikike mahala watu hawa wafahamike mbele ya umma, tunataka wafahamu kuwa maisha ya mwanadamu yana thamani kuliko siasa chafu na ufisadi wanaouendeleza. 

Nawashukuru kwa kunisikiliza.

Mabere Marando,
Dar es Salaam

Saturday, April 13, 2013

YANGA YAIVUA RASMI SIMBA UBINGWA WA LIGI KUU YA VODACOM NA KUICHAPA OLJORO 3

 Katika mchezo wa ligi kuu ya vodacom kati ya Yanga na JKT Oljoro uliomalizika muda si mrefu Yanga imeshinda kwa jumla ya magoli 3 na oljoro hawakupata kitu.
Goli la kwanza la lilifungwa dakika ya 5 na nahodha Nurdin Kanavaro,goli la pili limefungwa na Simon Msuva dakika ya 19 na la tatu limefungwa na Hamis Kiiza dakika ya 34.

MATATIZO YA KIUFUNDI YASABABISHA KUTOONESHWA "LIVE" MECHI ZA LIGI KUU TANZANIA BARA LEO

 
Afisa Habari wa TFF Boniface Wambura
Kutokana na habari aliyoitoa Afisa Habari wa TFF, ni kwamba  mechi zilizokuwa zioneshwe hii leo na kesho hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.Taarifa kamili hii hapa:-

"Mechi tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya kiufundi.

Kwa mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.

Mechi hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba, Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17 mwaka huu jijini Tanga.
Tatizo hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi hiyo ya Kenya.

Tshunungwa amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo. SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.

Pia TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport watakuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa.


Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)"

MWANAFUNZI CHUO KIKUU CHA RUAHA (RUCO) AJINYONGA


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Fulgence Ngonyani
WATU wawili wamefariki dunia katika matukio tofauti mkoani Njombe, akiwemo mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCO), mkoani Iringa kufariki dunia, baada ya kujinyonga kwa kutumia waya wa simu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Fulgence Ngonyani alisema tukio hilo limetokea juzi katika mtaa Iwawa, Makete mjini.

Alimtaja mwanafunzi huyo, kuwa ni Albarth Osward (27), mkazi wa kata ya Iwawa na kwamba mwili wake ulikutwa ukining'inia juu ya mti kando ya mto uliopo mtaa wa Ikuru.

Alisema chanzo cha mwanafunzi huyo kuamua kujiua hakijajulikana kwa madai kuwa hakuacha waraka wowote, na kwamba jeshi hilo linaendelea na uchunguzi.

Katika tukio jingine, mkazi wa Kijiji cha Banawanu Wilaya ya Wanging'ombe, Lutan Mbeni (40) ameuawa kwa kukatwa shoka sehemu mbalimbali za mwili wake, baada ya kuvamiwa na kundi la watu wanaosadikiwa kuwa majambazi.

Kamanda Ngonyani, alisema tukio hilo, limetokea juzi usiku baada ya watu hao kubisha hodi nyumbani kwa marehemu wakijifanya wanaomba msaada.

Alisema baada ya hodi hiyo, mke wa marehemu alifungua mlango akidhani ni watu wema ndipo walipomtaka awaonyeshe alipo mume wake.

Watu hao, walifanikiwa kupora fedha Sh 800,000, kisha kumuua kwa kumkata shoka na kutokomea kusikojulikana.

Alisema jeshi la polisi, linaendesha msako mkali ili kuwakamata watu hao wafikishwe mahakamani.

Habari hii ni kwa mujibu wa Mtanzania

Breaking news: GARI LA MASAMA LAPATA AJARI ENEO LA WAWI NA MTU MMOJA AFARIKI DUNIA

Habari zilizotufikia hivi punde, gari la kampuni ya Masama limepata ajari na mtu mmoja ameripotiwa kufa na wengine kupatata majeraha kadhaa.
Habari kamili tutawaletea kadiri tutakavyokuwa tunazipata.

VITA KALI BUNGENI TUNDU LISU vs MWIGULU MCHEMBA


Mh.Mwigulu mchemba.
Mh.Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Tanzania Bara) aliishambulia hotuba ya Mbowe akieleza kuwa hakuna haja ya kuhangaika na suala la ugaidi kwa kuwa Chadema ndiyo wanahusika nalo kwa kupanga kumdhuru mwandishi wa habari.

 “Watu wanapanga ugaidi halafu wanaachiwa tu, nashukuru Mbowe hayuko hapa nadhani atakuwa amekamatwa pamoja na katibu wake kwa kuwa wao ndio wamekuwa wakiwasiliana na aliyekuwa amepanga ugaidi,” alisema Nchemba.

Naye Tundu Lissu.
Mh.Tundu Lissu.
MBUNGE wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), akichangia hoja hiyo ya ugaidi, “...Kuna mheshimiwa humu ndani aliwasiliana na gaidi,” alisema Lissu kabla ya Anne Abbdalah kumtaka athibitishe na Lissu alisema: “Ushahidi upo kama Anna Abadallah anataka, kwani malipo yalifanywa na magaidi waliopo humu ndani..”

Pia Lissu amekuja juu na kusema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, anatakiwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa kuwa ameshindwa kumwajibisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa.

Amesema kitendo cha Waziri Mkuu kushindwa kumwajibisha Dk. Kawambwa kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka jana, hakiwezi kuvumiliwa na hivyo wabunge wanatakiwa kumwajibisha Waziri Mkuu.

Lissu aliyasema hayo bungeni jana, alipokuwa akichangia bajeti ta Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha wa 2013/2014.

Pamoja na kutaka hatua hiyo ichukuliwe, Lissu alisema tangu Rais Jakaya Kikwete aingie madarakani mwaka 2005, ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne umeshuka ikilinganishwa na hali ilivyokuwa enzi za Rais Benjamin Mkapa.

Kwa mujibu wa Lissu, mwaka jana Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, ilitoa ripoti ya takwimu za ubora wa elimu nchini kuanzia mwaka 2007 hadi mwaka juzi ikionyesha kushuka kwa ufaulu nchini.

Alisema ripoti hiyo, inaonyesha katika kipindi cha miaka mitano ya mwisho ya utawala wa Serikali ya awamu ya tatu iliyoongozwa na Rais mstaafu Benjamin Mkapa, ufaulu wa wanafunzi ulipanda.

FATAKI AKWAA KISIKI KATIKA HARAKATI ZAKE KWA WANAFUNZI.

Watoto wetu wote wangekuwa hivi,tabia hii chafu ingekomeshwa.

Friday, April 12, 2013

UKWELI KUHUSU LADY JAYDEE KUANZISHA KITUO CHA REDIO


Kutokana na uvumi na taarifa mbali mbali kuhusu mpango wa Lady Jaydee kuanzisha kituo cha redio kiitwacho KWANZA FM leo mhusika (Jidee) kaweka mambo hazarani na kusema kuwa kwanza taarifa hizo zilikuwa ni uzushi kutokana na tarehe hiyo zilipotoka kuwa ni siku ya wajinga.

Ameweka bayana maneno hayo usiku wa leo wakati akifanya mahojiano (Interview) katika kituo cha televisheni cha Channel ten. Mahojiano hayo yalikuwa ni kati ya Jay dee na Dj Tass. Lakini lady Jaydee amesema kutokana na mwitikio aliouona kwa watu ameamua kuwa na mpango huo wa kuanzisha kituo hicho cha redio.

Kuhusu wimbo wake wa Joto hasira, amesema ameutunga na kuuimba kwa kumlenga mtu ambaye hakuwa tayari kumtaja.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...