Friday, December 28, 2012

UZURI NA MAAJABU YA BUKOBA

Bukoba ni sehemu mojawapo ambayo kila mmoja anapenda akaishi kutokana na uzuri wake.Kihistoria,Bukoba ni sehemu miongoni mwa sehemu barani Afrika ambayo ilitawaliwa na Utawala wa Machifu (WAKAMA).Miongoni mwa machifu hao ni Mukama Lukamba ambaye alikuwa "Chief" wa Kyamutwara makao makuu yake ni Kabale,kata ya Karabagaine.

Nyumbani kwa Mukama Lukamba.



Kwa Wakama  hawa kulikuwa na mahakama (GOMBOLOLA) ambazo zilikuwa zinatumika kuhukumu waarifu wote waliokuwa wanaletwa mahakamani hapo.

Chief Lwaijumba local court
Mahakama ya Mukama Lwaijumba ambapo waarifu walikuwa wanahukumiwa.
Hata hivyo baada ya hukumu hiyo wote waliokuwa wanaadhibiwa kwa kunyongwa sehemu inayoitwa Mlima wa Lyankumbi ulioko Itahwa walipokuwa wanaachiwa na kuporomokwa hadi bondeni.
Mlima Lyankumbi ampako waarifu walikuwa wanaanyongwa.

Pamoja ni hayo,Kabale kuna pango ambalo lilitumika kwa wananchi kujificha wakati wa vita ya Kagera.Pango hilo lina urefu usiopungua kilometa 3.Pango hili la maajabu lipo katika mlima Rwamrumba.
Picha zifuatazo ni picha zinazoonesha pango la maajabu.




Mnamo miaka ya 1977 hadi 1979 kulikuwa na vita ya Kagera,vita hivi vilifanyika hasa maeneo ya Mutukura,Bunazi na Kyaka.Miongozi mwa uharibifu uliofanyika wakati wa vita ni Kuunguzwa kwa kiwanda cha sukari cha Kagera,Kuunguzwa kwa makanisa pamoja na mashule.
Picha zifuatazo ni baadhi tu ya picha zinazoonesha uharibifu uliofanywa na Nduli Iddi Amini -DADA kwa kuunguza kanisa la Kyaka.


Kanisa la Kyaka lililoungua.







No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...