Monday, August 19, 2013

TAMKO LA VODACOM KUHUSU KUKOSEKANA KWA HUDUMA ZA MAWASILANO NCHINI.

 
Wapendwa wateja wetu na jamii kwa ujumla;

Tunaomba radhi kwa dhati kabisa kwa kutoweza kuwapa huduma za mawasiliano za mtandao wa Vodacom kuanzia jioni ya siku ya Ijumaa Agosti 16 mpaka Jumamosi asubuhi Agosti 17, 2013....

Hali hii ilisababishwa na moto uliozuka katika jengo lenye kitovu cha kuendesha (switch) mitambo yetu lililopo Dar es Salaam . Moto huo ulipelekea kuzimika kwa mtambo wetu na kukata huduma zetu zote nchini na hivyo kuwaathiri wateja wetu wa ndani na nje ya nchi pamoja na jamii kwa ujumla.

Tunatambua na kuelewa usumbufu uliosababishwa na kukosekana kwa huduma zetu, na tunapenda kuwashukuru kwa uvumilivu na uaminifu wenu kwa Vodacom katika kipindi hiki kigumu.

Tutawarejeshea gharama za vifurushi vya bidhaa zetu hususan, muda wa maongezi, SMS na huduma za intaneti , mlivyovinunua siku ya Ijumaa Agosti 16, na ambavyo hamukuweza kuvitumia kikamilifu kutokana na kutokuwepo kwa mawasiliano. Zoezi hili litakamilika Jumatatu Agosti 19, 2013.

Ninaomba niwahakikishie wateja wetu kwamba Vodacom ina dhamira ya dhati kabisa ya kuendelea kutoa huduma zenye ubora wa hali ya juu hapa nchini.

Aidha, ninaomba pia kuwashukuru wafanyakazi na washirika wetu wote waliofanya kazi bila kuchoka ili kuhakikisha kuwa huduma zetu zinarejea katika hali yake ya kawaida kufikia asubuhi ya Agosti 17, 2013. Kwa hakika jitihada zao, kujituma kwao na utendaji kazi wao kwa bidii, vilitoa mchango mkubwa sana katika zoezi hili.

Kwa mara nyingine ninaomba niwatake radhi kwa usumbufu na kuwashukuru kwa uvumilivu wenu.

Rene Meza
Mkurugenzi Mtendaji

Commonwealth Academic Fellowships for Mid-Career Academics in UK, 2014.

Each year, UK Department for International Development (DFID) funds academic fellowships for mid-career academics from developing Commonwealth countries. These fellowships enable fellows to spend three months to network and update knowledge and skills related to their academic subject and responsibilities at any approved UK university or higher education institution. The CSC also invites alumni who held Commonwealth Scholarships for PhD to apply directly to the CSC for a Commonwealth Academic Fellowship. All eligible alumni will be sent a letter with details of how to apply. All applications must be made through your nominating university/university body in applicants’ home country. The deadline for applications is 3 December 2013.
Study Subject(s): The purpose of the Academic Fellowships is to provide an opportunity for Fellows to network and update knowledge and skills related to their academic subject and responsibilities.
Course Level: The Fellowships are awarded for mid-career academics to spend three months at any approved UK university or higher education institution.
Scholarship Provider: UK Department for International Development (DFID)
Scholarship can be taken at: UK
Eligibility: To apply for a Commonwealth Academic Fellowship, candidates should:
-Be Commonwealth citizens, refugees, or British protected persons
-Be permanently resident in a developing Commonwealth country
-Be available to commence their Fellowship in the United Kingdom on 1 September 2014. Any other start date will only be permitted in exceptional circumstances
-Have been employed for at least five years as an academic staff member of a university in a developing Commonwealth country
-Be in the employment of the nominating university
-Hold a doctorate
-For awards to enhance clinical skills in the fields of medicine and dentistry, have qualified as a doctor or dentist before 1 October 2004.

MTAZAMO WA ZITTO KABWE JUU YA RASIMU YA KATIBA.

Rasimu ya Katiba ibara ya 215 inasema vyanzo vya mapato ya Muungano, kikubwa, ni ushuru wa bidhaa. Wajumbe wa Tume wanasema walifanya hesabu sawa sawa na fedha hizo zitatosha kuendesha Muungano. Lazima aliyewafanyia hayo mahesabu ama aliwapotosha au hajui.
Mwaka 2012/13 Ushuru wa bidhaa (ndani na nje) uliingiza mapato ya tshs 1.5 trilioni tu. Fedha hii inatosha kuendesha Wizara ya Ulinzi peke yake!
Haitoshi hata kuhudumia Deni la Taifa (ambalo mkopaji ni Jamhuri ya Muungano). Huu muungano utaendeshwaje?
Rasimu inapaswa kufanyiwa kazi sana. Nahisi Tume ilikuwa na haraka na haikutafakari kwa kina baadhi ya masuala.
Mambo ya Muungano inabidi yaangaliwe upya kabisa ili kuboresha mfumo wa Serikali 3 unaopendekezwa ikiwemo kuzuia Washirika wa Muungano kuunda vikosi vyao vya kijeshi, Ulinzi na usalama. Suala la biashara ya kimataifa na hata suala la usimamizi wa maliasili (regulatory function).
Source:Zitto Social media.

Sunday, August 18, 2013

Djotodia aapishwa kama rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Kiongozi wa zamani wa waasi ambaye alifanya mapinduzi katika Jamhuri ya Afrika ya Kati Michel Djotodia ameapishwa kama rais.
Bwana Djotodia ameahidi kuandaa uchaguzi kufikia mwanzo wa mwaka ujao. Tangu achukue uongozi mwezi Machi kupitia kikundi cha waasi wa Seleka nchi hiyo imetajwa kutumbukia zaidi katika umaskini na utovu wa sheria.
Shirika la Umoja wa mataifa linakadiria kuwa zaidi ya thuluthi moja ya raia wa nchi hiyo wanahitaji msaada wa dharura.
Baraza la uslama la Umoja wa mataifa limeonya kuwa kuongezeka kwa ukatili na uvunjifu wa sheria katika Jamhuri ya Afrika ya Kati inatishia usalama na uthabiti wa eneo lote.
Msemaji wa rais wa zamani Francois Bozize ambaye aling'olewa madarakani na bwana Djotodia amemtaja kiongozi huyo mpya kama 'kibaraka'.
Msemaji huyo Levi Yakete, amenukuliwa katika Redio Ufaransa kusema:
'Bwana Djotodia, ambaye ameingia madarakani kwa njia ambazo sote tunaelewa, ni kibaraka tu wa Chad na Sudan. Aliingia madarakani kupitia njia ambazo hazikubaliki na watu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati. Alipindua utawala wa kisheria na katiba, ambao ulikuwa unaongozwa na Francois Bozize.'

Chanzo : BBC

VIDEO YA YAHAYA - LADY JAY DEE HII HAPA.

WAHAMIAJI HARAMU 8,666 WAREJEA MAKWAO MKOANI KAGERA, CHELSEA 2 - HULL 0.

Kutoka Kagera.
Serikali Mkoani Kagera imesema mpaka sasa wahamiaji haramu wapatao 8,666 wameshaondoka na kurejea nchini kwao ambapo kati yao 500 ni Waganda na silaha zipatazo 43 zimesalimishwa.

Kutoka Uingereza
 Katika Ligi kuu ya Uingereza,Tottenham 1 - Crystal Palace 0
wakati katika mtanange kati ya Chelsea vs Hull City matokeo ni Chelsea 2 - Hull 0

ALICHOKISEMA ZITTO KABWE LEO.

Katika moja ya maazimio ya Kamati za Bunge za mahesabu ya Umma (Kamati ya Hesabu za Serikali, Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa na Kamati ya Bajeti) iliamuriwa kuwa Serikali ianze utaratibu wa kukusanya maduhuli yake kwa kutoa risiti za kielektroniki. Azimio hilo linasema
“Maduhuli ya Serikali sasa yakusanywe kwa kutumia risiti za elektroniki. Serikali Kuu, Serikali za Mitaa na Mashirika ya Umma yaanze kutumia risiti za eletroniki mara moja ili kudhibiti upotevu wa mapato ya serikali yanayotokea hivi sasa katika kutumia risiti zinazoandikwa kwa mkono. Pia ofisi za serikali zifanye manunuzi yake kwa wafanyabiashara wanaotumia mashine za kielektroniki.”
Nimepitia Mpango wa Serikali wa Mapato (Volume I – Financial Statement and Revenue Estimates 2013/14) na kugundua kuwa mapato yasiyo ya kikodi yamekadiriwa kuwa ni shilingi bilioni 741 kutoka Wizara, Idara na Mikoa na shi...lingi bilioni 383 kutoka kwenye Halmashauri za Wilaya, Miji na Manispaa. Sikuweza kupata mapato ya Mashirika ya Umma maana hayaletwi kwenye Bajeti za Serikali.
Wizara 10 zinazoongoza kwa Mapato (mapato kwenye mabano ni Wizara ya Nishati na Madini ( 220 bn), Wizara ya Fedha (126bn), Wizara ya Ardhi (100 bn), Wizara ya Maliasili (84 bn), Wizara ya Mambo ya Ndani – Uhamiaji (92 bn), Wizara ya Mifugo (19 bn), Wizara ya Mambo ya Nje (16 bn) na Wizara ya Mambo ya Ndani – Polisi (17 bn), kati ya hizi shilingi 16 bilioni ni kutoka idara ya Trafiki (traffic notification fees).
Kutokana na mafanikio ya makusanyo ya VAT ambapo inaonyesha kuwa mapato ya Serikali yameongezeka kwa asilimia 60 (kutoka 500 bn mpaka 800 bn), na kutokana na rekodi mbalimbali za Serikali zinazoonyesha kuwa zaidi ya asilimia 50 ya makusanyo ya Serikali hayafiki Serikalini, ni dhahiri kuanzishwa kwa makusanyo kwa risiti za kielektroniki kutapandisha mapato ya Serikali zaidi ya mara mbili. Idara ya Usalama barabarani peke yake inasemekana kuwa makusanyo ya sasa ni theluthi tu ya makusanyo stahili kutokana na rekodi za ‘notifications’ barabarani.
Risiti za elektroniki kwa kukusanya maduhuli ya Serikali yanaweza kuongeza mapato ya Serikali maradufu na kuepuka mtindo wa Serikali wa kupandisha kodi kwenye bidhaa muhimu kwa wananchi. Uamuzi wa Kamati za Bunge za Mahesabu wa kuitaka Serikali kukusanya maduhuli yake kwa kutumia risiti za elektroniki unapaswa kuungwa mkono na kila Mtanzania.
 
Zitto Kabwe

Einstein Postdoctoral Fellowship Program for International Applicants in USA, 2014.

The National Aeronautics and Space Administration (NASA) are funding ten Einstein postdoctoral fellowship programs for pursuing research that is broadly related to the science goals of the NASA Physics of the Cosmos program. International applicants are eligible for this postdoctoral fellowship. The duration of funding is about three years which covers annual stipend, plus health insurance, relocation costs and provides funding for research related travel, computing needs and other research costs. The fellowship is awarded on the basis of the applicant’s research proposal as well as the curriculum vitae, list of publications, summary of previous and current research and three letters of reference. The online application should be submitted by November 7, 2013.
Study Subject(s): The fellowship provides an opportunity for highly qualified, recent postdoctoral scientists to conduct independent research that is broadly related to the science goals of the NASA Physics of the Cosmos program.
Course Level: This fellowship is awarded for pursuing a postdoctoral program at Host Institutions in USA.
Scholarship Provider: The National Aeronautics and Space Administration (NASA)
Scholarship can be taken at: USA
Eligibility:- Applicants must have received a Ph.D., Sc.D., or equivalent doctoral-level research degree in astronomy, physics, or a related discipline after January 1, 2011.
-Applicants who have not yet formally received their degree must present evidence of having completed the academic requirements before commencing the Fellowship.
-Einstein Fellowships are open to citizens of the United States and to English-speaking citizens of other countries.
-Non-US applicants should read the VISA requirements under the “Additional Information” section below before applying. [Note: The United States is defined as the 50 states and the District of Columbia.] Qualified applicants will receive consideration without regard to race, creed, color, age, sex, or national origin.
-Women and minorities are strongly encouraged to apply.

MBOWE AWAKARIBISHA CHADEMA MADIWANI WALIOTIMULIWA CCM MKOANI KAGERA, AWAPA MBINU

MADIWANI wanane wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Kagera waliofukuzwa uanachama wiki iliyopita wamekaribishwa kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, ndiye aliyewakaribisha madiwani hao wanaosubiri kufukuzwa rasmi na vikao vya Kamati Kuu ya CCM, vinavyotarajiwa kufanyika wiki hii mkoani Dodoma.
Madiwani waliofukuzwa na kata zao kwenye mabano ni Richard Gaspar (Miembeni), Murungi Kichwabuta (Viti Maalumu), Alexander Ngalinda ambaye pia ni naibu meya (Buhembe), Yusuf Ngaiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya (Kashai), Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga), Robert Katunzi (Hamugembe), Samwel Ruhangisa (Kitendagulo) na Dauda Kalumuna (Ijuganyondo).
Akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Uhuru wa Bukoba Mjini, Mbowe alisema CCM imewachakachua madiwani hao wanane na hata wakibaki huko chama chao hakitawaona wa maana, kwa sababu chama hicho kinalea ufisadi.
Mbowe alisema CHADEMA wako tayari kuwapokea madiwani hao waliofukuzwa na kuwafundisha siasa za mageuzi.
“Tutasimama nao katika kujenga Bukoba mpya isiyo na ufisadi kama unaofanywa na Meya wa manispaa hiyo iwapo wataamua kuja kwetu, milango ipo wazi nawakaribisha,” alisema.
Mbowe alisema CHADEMA kinamuunga mkono Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Hamis Kagasheki (CCM), anayepinga ufisadi unaofanywa na meya kutoka chama chake, Anatory Amani.
Alisema CHADEMA itashirikiana na kiongozi yeyote kutoka CCM atakayekuwa tayari kupambana na ufisadi ulioshamiri kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.
“CHADEMA katika mambo ya ufisadi ina msimamno unaoeleweka na kwamba katika kupinga ufisadi kipo tayari kumuunga mkono yeyote bila kujali itikadi,” alisema Mbowe na kusisitiza kwamba hata kama meya angekuwa mwanachama wa CHADEMA kingeunga mkono afukuzwe.
“Hatuna masilahi ya kisiasa na Kagasheki lakini katika suala hili tunamuunga mkono. Nawapongeza madiwani wetu wa CHADEMA walioungana na mbunge huyo kupinga ufisadi wa meya na kusimamia masilahi ya wananchi wa Bukoba Mjini,” alisema Mbowe.
Mbowe aliikejeli CCM kuwa haiwezi kuwafukuza madiwani hao kwa sababu itakuwa imejimaliza na hawana uhakika wa kuzirejesha kata hizo ukiitishwa uchaguzi.
Alisema kutokana na hofu hiyo Makao Makuu ya CCM yaliamua kuwarejesha madiwani hao wanane waliofukuzwa na CCM Mkoa wa Kagera.

Thursday, August 15, 2013

KAULI YA ZITTO KABWE JUU YA VIONGOZI KUWEKA WAZI MALI NA MADENI YAO.

Mbunge wa Kigoma kaskazini mh.Zitto Kabwe katoa maoni yake juu ya uhakiki wa mali na madeni ya viongozi kama ifuatavyo:-
" 'Uwazi wa mali na madeni ya viongozi ni moja ya hatua muhimu kupambana na ufisadi' nimemwambia leo Mama Salome Kaganda wa Sekretariat ya Maadili ya Umma.
Wanasiasa tunajaza fomu kutangaza mali na madeni yetu. Fomu hizo haziwekwi wazi kwa wananchi. Utajuaje kama Kiongozi kasema uwongo? Utawezaje kupambana na uzushi na uwongo dhidi ya viongozi waadilifu lakini wanachafuliwa na wapinzani wake kisiasa? Suluhisho moja tu. UWAZI. Daftari la mali na madeni ya viongozi liwe wazi kwa wananchi. Fomu za mali na madeni ya viongozi wa umma ziwe online. Kiongozi asiyetaka mali na madeni yake kujulikana, akauze vitumbua aache uongozi, hakuna atakayemgusa!
"
Source:Zitto Social media.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...