Wednesday, April 24, 2013

TAIFA STARS KUSHIRIKI MICHUANO YA COSAFA

Kim Poulsen kocha mkuu wa Taifa Stars.
Hii ni taarifa iliyotolewa na TFF kuwa Taifa Stars imealikwa kushiriki mashindano ya COSAFA na taarifa yenyewe ni hii hapa:-
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itashiriki michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) itakayofanyika Julai mwaka huu nchini Zambia.

Taifa Stars inashiriki michuano hiyo ya timu za Taifa za nchi wanachama wa COSAFA ikiwa timu mwalikwa. Nchi wanachama wa COSAFA ni Afrika Kusini, Angola, Botswana, Comoro, Lesotho, Madagascar, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Namibia, Shelisheli, Swaziland, Zambia na Zimbabwe.

Michuano hiyo itafanyika kuanzia Julai 6 hadi 21 mwaka huu katika miji ya Lusaka, Ndola na Kabwe. Ratiba ya makundi ya michuano hiyo itapangwa Mei 3 mwaka huu jijini Lusaka.

Mara ya mwisho michuano hiyo ilifanyika miaka mitatu iliyopita. Hii itakuwa mara ya pili kwa Tanzania kushiriki michuano hiyo baada ya kucheza ya kwanza iliyofanyika mwaka 1996 nchini Zimbabwe.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inatarajia kuingia kambini mwishoni mwa mwezi ujao kujiandaa kwa mechi ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech.

Juni 16 mwaka huu Taifa Stars itacheza na Ivory Coast jijini Dar es Salaam katika mechi nyingine ya mchujo ya Kombe la Dunia wakati Juni mwishoni na Julai mwanzoni itacheza mechi ya Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) dhidi ya Uganda.
Wakati huo huo, waandishi wa habari wanaotaka kuripoti michuano hiyo wanatakiwa kuwasilisha majina yao TFF kabla ya Aprili 27 mwaka huu ili maombi yao yatumwe COSAFA kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho (Accreditation).



Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

ZITTO KABWE NA BAJETI YA WIZARA YA MAJI.

 Ktika akaunti yake ya mtandao wa kijamii,Mh.Zitto Kabwe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kasikazini, kaelezea kwa ufupi mchanganuo na vipaumbele vya Wizara ya maji katika bajeti ya 2013/2014 na kuandika yafuatayo:-  
"Bungeni Leo na kesho Ni bajeti ya Wizara ya maji. Waziri ametaja mipango mingi sana kwenye hotuba yake. Hata hivyo ukiangalia pesa za bajeti unaona mipango mingi Ni porojo tu. Kwa mfano, kupitia mpango wa "tekeleza sasa Kwa matokeo makubwa" Serikali imepanga kufikisha maji Kwa wananchi 15.4m ifikapo mwaka 2016. Mpango huo utagharimu jumla ya tshs 1.5trn. Hata hivyo ukiangalia Bajeti nzima ya Wizara Ni tshs 398bn tu ambapo tshs 379bn Ni za maendeleo (hii Ni kudos maana Fedha za miradi Ni nyingi kuliko za matumizi ya kawaida). Hata hivyo tshs 241bn Ni kutoka Kwa wafadhili. Bajeti yote ya Wizara ya Maji Ni 2.2% ya Bajeti nzima ya serikali inayofikia takribani ths 18trn. Tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa Maji ndio tatizo kubwa zaidi linalokabili Watanzania. Wakati wa Bajeti ya Waziri Mkuu, wabunge wengi walichangia kuhusu matatizo ya maji katika maeneo yao kuliko suala lingine lolote lile. Ninaamini wabunge watajadili hotuba ya Waziri wa Maji Kwa kuzingatia unyeti wa suala hili ili kuwaondolea adha wananchi wa vijijini na hasa wanawake wanaohangaika kutafuta maji umbali mrefu sana. Maji Ni Uhai......"

SERIKALI YA UFARANSA WARUHUSU NDOA YA JINSIA MOJA.

Bunge la Ufaransa limeidhinisha ndoa za watu wa jinsia moja na kuruhusu wanandoa hao kupata watoto wa kupanga.Bunge hilo la Ufaransa lenye wabunge wengi wa kisosholisti liliupigia kura mswada huo  kwa kura 331 dhidi ya 225 ili kuidhinisha kuwa sheria.Sheria hiyo mpya inatarajiwa kuanza kutekelezwa kuanzia mwezi Juni mwaka huu.Baada ya kura hiyo wakereketwa wanaounga mkono ndoa za watu wa jinsia moja walisherehekea uamuzi huo wa bunge na kusema wanastahili kuwa na uhuru wa kufanya maamuzi ya jinsi ya kuendesha maisha yao na kuwa uamuzi huo wa bunge umewapa uhuru huo.Hata hivyo kumekuwa na upinzani wa kupitishwa kwa sheria hiyo mpya.Punde baada ya kuidhinishwa,wabunge kutoka vyama vya mrengo wa kulia walitangaza kuwa wataupinga kikatiba.Baraza litakuwa na mwezi mmoja kutoa uamuzi kamili.Ufaransa ni nchi ya 14 kuhalalisha ndoa za watu wa jinsia moja duniani.

CHANZO:IDHAA YA KISWAHILI YA UJERUMANI.

CHADEMA WAFUNIKA IRINGA,WAFANYA MKUTANO MKUBWA UKIONGOZWA NA DR.SLAA


Dr.Slaa akiwahutubia wakazi wa Iringa.
Jana CHADEMA walifanya mkutano mkubwa katika Manispaa ya Iringa kwa kutekeleza ahadi ya wabunge wa chama hicho waliyoitoa wakati wakiwahutubia wakazi wa Jiji la Mwanza kuwa watatembelea majimbo kadhaa ili kuwaeleza wananchi nini kilichotokea bungeni mpaka wabunge 6 wa chama hicho wakasimamishwa kuhudhulia vikao 5 vya Bunge.
Hapa ni picha mbali mbali kuhusiana na ziara hiyo ya Mkoani Iringa.
Msafara ukielekea Iringa.

Msafara ukiwa Mkoani Iringa.

Sugu akiwahutubia wakazi wa Iringa.
Dr.Slaa akiwa na Mbunge wa Ubungo Mh.John Mnyika.




RAIS UHURU KENYATTA AANZA KUTANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameanza mchakato wa kuunda serikali mpya ambapo ametangaza majina ya mawaziri wanne. Mawaziri hao ni pamoja na Dkt. Fred Okeng'o Matiangi ambaye ni waziri mteule wa Teknolojia na Mawasiliano, Henery Rotich ameteuliwa wizara ya Fedha, James Wanaina Macharia ndiye Waziri mteule wa Afya na Balozi Amina Mohammed ametangazwa Waziri wa mambo ya kigeni.
Ilitarajiwa kwamba Rais Kenyatta angewataja mawaziri wote 18, lakini amesema wengine watatangazwa baadaye na kuomba taifa kuwa na subira. Huku haya yakiarifiwa Bunge la Kenya limeidhinisha kamati maalum ambayo itawachuja mawaziri watakaoteuliwa na Rais.Kamati hiyo inaoongozwa na Spika wa Bunge Justin Muturi.
Chini ya katiba ya Kenya sharti bunge lipitishe majina ya maafisa wakuu wa serikali, wakiwemo Mawaziri, Mabalozi na wakuu wa tume za kikatiba.

Chanzo:BBC

Tuesday, April 23, 2013

DIAMOND KUFANYA SHOO KUBWA UINGEREZA...!!

Diamond anatarajia kufanya shoo kubwa nchini Uingereza kuanzia tarehe 27 mwezi 4.Hii ni kwa mujibu wa habari alizozitoa Diamond katika mtandao wake wa kijamii na Diamondi ameandika hivi:-
 

"Napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru mwenyezi mungu kwa wingi wa rehema zake na mapenzi yake kwangu mpaka nuda na saa hii nipo hapa nilipo.....
Napenda kuchukua nafasi hii kuwataharifu mashabiki zangu wote...Hususani Mashabiki zangu wa Nchini Uingereza kuwa bado siku 6 tu toto la kimanyema.....kutoka Tandale .Ntakuwa nchini Uingereza Nikianza na show ya tarehe 27 mwezi wa 4....
Ntakuwa na Silaha zangu mbili za maangamizi.Nikizungumzia Dancers wangu wawili machachari na wazawa kutoka wasafi...Dumi Utamu na Mose Iyobo....!!
Nakuja kuweka Historia Mpya Uingereza....Ntahakikisha kuwa naididimiza ardhi ya Malkia kwa Michezo ya kuringa ringa na Mashetani ya Kimanyema yatakapopanda....Ts Gona Be Crayz Usikose....Asikudanganye mtu tarehe London ntakuwepo
tarehe 27 april na reading ntakuwepo Tarehe 5may.....!! 

Thats official me....
Njoo tulewe kwa pamoja kisha kesho muone ntampeleka nani kwa Bi Sandrah Nchini Tanzania.....Hii si yakukosa....!!

WASAAAAAAFIIIIIIII"


 Kila la heri Diamond, keep it up!!!!!

LEO NI LEO,BARCELONA vs BAYERN MUNICH


Vita kusaka tiketi ya kusafiri kwenda jijini London kwenye mchezo wa fainali wa klabu bingwa barani Ulaya inaanza usiku huu kati ya Mabingwa wa soka nchini Ujerumani dhidi ya inayotajwa kuwa timu bora kwa vilabu vya soka duniani kwa wakati huu FC Barcelona.
Kocha wa Bayern Munich, Jupp Heynckes amesema haogopeshwi na urejeo wa nyota wa Barcelona, Lionel Messi kuelekea mchezo huo wa kwanza wa nusu fainali ya klabu bingwa barani Ulaya.
Messi hajacheza mchezo wowote wa Barcelona toka alipoingia kama mchezaji wa akiba na kuisaidia timu yake kufuzu nusu fainal katika mchezo robo fainali dhidi ya Paris St-Germain ya Ufaransa. Lakini kuna kila dalili Muanjetina huyo mwenye umri wa miaka 25 ambaye ndiye mchezaji bora wa dunia kwa sasa,akajumuishwa kwenye kikosi cha Barcelona kwenye mchezo wa usiku wa leo.
Mwezi uliopita Messi aliweka rekodi kwenye ligi ya Hispania kwa kuwa mchezaji aliyezifunga timu zote zinazoshiriki ligi kuu nchini humo maarufu kama La Liga kwa misimu miwili mfululizo.
Barcelona inapambana kutaka kutwaa taji la tatu la klabu bingwa barani Ulaya ndani ya miaka mitano,Huku Bayern Munich ambao msimu ujao watakuwa chini ya aliyekuwa kocha wa Barcelona, Pep Guardiola, wao wanapambana kutafuta nafasi ya kucheza fainali yao ya tatu ndani ya miaka minne.
Kocha wa Bayern Munich, Jupp Heynckes ambaye aliwahi kuwafundisha mahasimu wa Barcelona, Real Madrid amesema licha ya kumheshimu mrithi wake wa kiti cha ukocha kwenye timu hiyo lakini hajaomba ushauri wowote kutoka kwa Guardiola na amejiandaa kwa kila namna kuhakikisha anaifunga Barcelona usiku huu. Aliongeza kwa kusema anaijua vizuri sana timu yake kuliko mtu yeyote na anafahamu soka ya Hispania na Barcelona wenyewe kwa undani mkubwa.
Wakati Barca wakiwa hawajaweka wazi kama watamuanzisha Messi au la, Baadhi ya wachezaji wa Barcelona akiwemo Xavi Hernandez alinukuliwa siku ya jumatatu akisema, kombe la ligi kuu nchini Hispania, La Liga lina umuhimu mkubwa kuliko klabu bingwa barani Ulaya.
Mechi hiyo itachezwa kwenye uwanja wa Allianz Arena mjini Munich nchini Ujerumani,majira ya saa nne kasorobo usiku kwa saa Afrika Mashariki.

UBALOZI WA UFARANSA NCHINI LIBYA WASHAMBULIWA.

Bomu limelipuka nje ya ubalozi wa Ufaransa katika mji mkuu wa Libya, Tripoli na kuwajeruhi walinzi wawili huku ikisababisha uharibifu mkubwa.
Mlipuko huo ulisababisha uharibifu katika sehemu moja ya ofisi hizo na pia kuharibu nyumba jirani.
Mwandishi wa BBC mjini Tripoli, Rana Jawad anasema kuwa inaaminika kuwa mlipuko huo ulisababishwa na gari lililokuwa na mabomu.
Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, aliitaka serikali ya Libya kuchukua hatua za haraka kukabiliana na waliosababisha shambulio hilo.
Aliongeza kwamba shambulizi hilo lililenga nchi za kigeni zinazopambana dhidi ya ugaidi.
Balozi za kigeni nchini Libya zimewahi kushambuliwa katika siku za nyuma, lakini hili ndilo shambulizi la kwanza kubwa dhidi ya ubalozi wa kigeni mjini Tripoli.
Shambulizi liliwahi kufanywa dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini Benghazi mwezi Septemba mwaka jana na kusababisha kifo cha balozi Christopher Stevens pamoja na maafisa wengine wamarekani .
Shambulio la leo lilifanyika muda wa saa kumi na moja alfajiri katika mtaa wa kifarahari mjini Tripoli.
Wakazi wa eneo hilo walighadhabishwa sana na shambulizi hilo na kulalamikia ukosefu wa ulinzi mzuri wa sehemu hiyo.
Waziri wa mambo ya nje wa Libya, Mohammed Abdel Aziz alilaani vikali shambulizi hilo, ingawa hawajaeleza ni nani wanayemshuku kulifanya shambulizi hilo.

CHANZO: BBC

KIKWETE:AFRIKA TUNAWEZA KUJISIMAMIA,TUMESHAKUA

Rais Jakaya Kikwete, amesema Bara la Afrika limepitia kwenye kipindi kigumu cha kukabiliana na utawala wa kikoloni ulioendesha mambo kwa kuzikandamiza nchi za Kiafrika, lakini sasa bara hilo limepiga hatua na linaweza kuzitafutia ufumbuzi changamoto za kiusalama pasipo kutegemea msaada wa nje.

Rais Kikwete ambaye alikuwa akizungumza wakati akifungua kikao cha siku moja kilichowajumuisha mawaziri wa Baraza la Usalama na Amani la Umoja wa Afrika (AU), alisema kuwa, Afrika imefanikiwa kujitambulisha kwenye duru la kimataifa kuwa ni bara linaloweza kujiamulia mambo yake bila kuingiliwa.

Alisema Umoja wa Afrika utaendelea kuwa mstari wa mbele kutetea masilahi ya wananchi wa Kiafrika hasa katika kipindi hiki ambacho alisema kuwa kiwango cha migogoro kimeanza kupungua.

“ Kwa kweli hadi kufikia hapa Afrika imepiga hatua, tumeweza kuishughulikia na kuitatua migogo mingi iliyolikumba bara letu,tutaendelea kufanya hivyo katika siku za usoni na kwa kweli sasa tumedhamiria kupambana na viongozi wanaoingia madarakani kwa mapinduzi ya kijeshi” alisema Rais Kikwete.

Alisema yale yanayoendelea kushuhudiwa sasa katika nchi za Mali, Jamhuri ya Kati ni matukio yasiyovumilika na kwamba suala la kutumia nguvu za kijeshi kwa ajili ya kurejesha utulivu na amani ni suala lisiloepukika.

“Nataka niwakumbushe pia wakati nikiwa mwenyekiti wa AU, tulifanikiwa kurejesha utawala wa kidemokrasia nchini Comoro baada ya Kanali Bacar kujaribu kutaka kuteka moja ya kisiwa,na sasa haya tunayoyashuhudia Mali na Jamhuri ya Afrika ya Kati hayawezi kufumbiwa macho pindi itapolazimika sisi kwa umoja wetu tutalazimika kufanya hivyo hivyo “alisema.

Mbali ya kupigana kijeshi kisiwani Comoro, Tanzania inatazamia kushiriki operesheni ya kivita Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa ajili ya kuwafurusha wanamgambo wa kundi la M23 ambao wamedhibiti eneo la Mashariki mwa nchi hiyo.

Tanzania imeitikia wito wa Umoja wa Mataifa ambao hivi karibuni ulipitisha azimio lilitoa fursa kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) kushiriki operesheni ya kivita kama moja ya hatua ya kukabiliana na waasi hao.

Kuhusu hali ya kisiasa nchini Madagascar, Rais Kikwete alisema nchi za Sadc zitaendelea kufuatilia jinsi wanasiasa wa taifa hilo wanavyotekeleza makubaliano yaliyofikiwa baada ya upatanishi wa muda mrefu ulioongozwa na aliyekuwa Rais wa Msumbiji, Joachim Chissano.

Mkutano huo wa mawaziri wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika ulikuwa na agenda ya kujadili hali ya kisiasa nchini Madagascar kabla ya uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Julai mwaka huu.

CHANZO:MWANANCHI

Monday, April 22, 2013

HATRICK YA ROBIN VAN PERSIE YATOSHA KUWAPA UBINGWA MAN UNITED.

Robin van persie akifunga goli la 3 (Hatrick)
Ilikuwa ni dakika ya kwanza RVP alipoipatia timu ya Man United goli la kwanza dhidi ya timu ya Aston Villa katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza mchezo uliopigwa katika uwanja wa Old trafford.
Ni dakika ya 12 Van Persie tena akaipatia timu yake goli la pili.Goli la tatu lilifungwa na Van persie tena ikiwa ni dakika ya 32.Magoli yote yalipatikana katika kipindi cha kwanza.Kutokana na kufunga magoli hayo matatu,Van Persie alitoka uwanjani na mpira baada ya kupiga Hatrick.
RVP akishangilia goli.
Van Persie alionekana kuwa mwimba katika ngome ya Aston  Villa baada ya kuwasumbua vyakutosha mabeki wa timu hiyo.
Na huu ndo msimamo baada ya matokeo hayo hapo juu:-

Club Pld Pts
Man Utd 34 84
Man City 33 68
Arsenal 34 63
Chelsea 33 62
Tottenham 33 61
Everton 34 56
Liverpool 34 51
West Brom 33 45
Swansea 33 42
West Ham 34 42
Fulham 34 40
Southampton 34 39
Norwich 34 38
Sunderland 34 37
Stoke 34 37
Newcastle 34 37
Aston Villa 34 34
Wigan 33 31
QPR 34 24
Reading 34 24

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...